Ticker

6/recent/ticker-posts

DIWANI KATA YA NDALA ZAMDA SHABAN AFANYA MKUTANO WA HADHARA NA WANANCHI WAKE, VIONGOZI MBALIMBALI WAHUDHURIA

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Diwani wa kata ya Ndala Manispaa ya Shinyanga mheshimiwa Zamda Shaban amefanya mkutano wa hadhara uliolenga kutoa taarifa za shughuli za maendeleo pamoja na kusikiliza changamoto zinazokwamisha maendeleo katika kata hiyo.

Mkutano huo umefanyika kwenye uwanja uliopo mtaa wa Mlepa kata ya Ndala ambapo wadau na viongozi mbalimbali wa mkoa, wilaya na ngazi ya kata wamehudhuria kwa ajili ya kupokea na kutolea ufafanuzi kero za wananchi.

Katika mkutano huo Wakazi wa kata ya Ndala wakiwemo wazazi na walezi wametakiwa kushirikiana kwa pamoja kuondoa changamoto zinazoikabili kata hiyo ikiwemo changamoto zilizopo kwenye shule ya msingi Msufini pamoja na Ndala sekondari ili kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

Hayo yameelezwa na walimu wa shule hizo katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Diwani wa kata ya Ndala Manispaa ya Shinyanga Zamda Shaban kwa lengo la kutoa taarifa za shughuli za maendeleo na kusikiliza changamoto zinazoikabili kata hiyo.

Mariam Salungi ni mwalimu wa shule ya msingi Msufini pamoja na makamu mkuu wa shule ya sekondari Ndala Alphonce Deya wameeleza changamoto huku wakiomba ushirikiano wa pamoja kwa wananchi ili kutatua changamoto hizo.

Shule ya msingi Msufini inakabiliwa na changamoto ya walimu ambapo idadi ya walimu katika shule hiyo ni 11 huku zaidi ya wanafunzi  elfu moja mianane ishiringi wanaendelea na masomo.

Mwalimu Mariam Salungi amesema hali hiyo inachangia wanafunzi wengi kutofaulu na  shindwa kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza

Akizungumza diwani wa kata ya Ndala Zamda Shaban ameendelea kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Luluhu Hassan kwa kuleta fedha za maendeleo katika kata ya Ndala ambapo amesema hakuna changamoto iliyokwamisha miradi hiyo.

Mheshimiwa Zamda jina maarufu Tausi  amewaomba wazazi na wananchi kwa ujumla wa kata ya Ndala  kuendelea kushirikiana katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

“Niwaombe wazazi tushirikiane na walimu ili shule iendelee kufanya vizuri shule ya msingi Msufini bado ni tatizo Mwaka huu wamefeli watoto 50 kwa umliwalionao wataenda wapi na watafanya kazi gani hawa bado watoto wadogo sana Watoto 50 kwenye kata yetu ni wengi sana lakini ni kwa sababu ya miundombinu mibovu na hili swala tulishalileta kwenu angalau tuweze kupata shule ya awali Msufini B”.amesema Diwani Zamda

“Pamoja na jitihada zote za serikali isiwe sababu ya sisi wananchi kuacha kuchangia maendeleo ya watoto wetu tutakapoanzisha boma letu serikali itakuja kutuunga mkono na walimu tutaletewa wapya kwahiyo niwaombe sana wazazi na wananchi wa kata ya Ndala tushirikiane kwa pamoja kuondoa changamoto hii ya watoto wetu”.amesema Diwani Zamda

Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, mratibu wa TASAF Manispaa hiyo Octavina Kiwone naye amewasisitiza wananchi wa kaya ya Ndala kuwa na utaratibu wa kuungana kwa pamoja katika utatuzi wa changamoto shughuli ya  kuboresha miundombini.

Mkutano huo wa hadhara ambao uliandaliwa na Diwani wa kata ya Ndala Zamda Shaban kwa ajili ya kutoa taarifa za shughuli za maendeleo na kusikiliza kero za wananchi huku akiahidi kuendelea na utaratibu huo kila baada ya mienzi mitatu ambapo wananchi wamepata nafasi ya kuuliza maswali juu ya changamoto zinazowakabili.

Baadhi ya wakazi wa kata ya Ndala wameonekana kutolidhishwi na huduma zinazotolewa na shirika la umeme Mkoa wa Shinyanga pamoja na huduma za bima ya Afya katika kituo cha afya Kambarage.

Wananchi hao wameeleza kuwa bado hawalidhishwi na huduma zinazotolewa na TANESCO Mkoa wa Shinyanga huku huduma za CHF zikitajwa kuwa ni changamoto kwa baadhi ya wananchi.

Moja ya changamoto zilizotajwa ni wananchi wanaoomba kuunganishiwa umeme wengi hushindwa kupata kwa wakati na wengine kutopata kabisa hali ambayo inaendelea kurudisha nyuma maendeleo ya baadhi ya wakazi wa kata ya Ndala.

 

Kaimu meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga Kurwa  Mangara ameahidi kushughulikia changamoto zote zilizowasilishwa na wananchi kupitia mkutano huo wa hadhara.

 Naye mganga mkuu wa Manispaa ya Shinyanga Dkt. Elisha Robert ameeleza juu ya huduma za bima ya afya katika kituo cha afya Kambarage mjini Shinyanga ambapo amesema kituo hicho kinatoa huduma nyingi za bure hali inayochangia dawa zinazolewa kuisha mapema.

Aidha mtendaji wa kata ya Ndala Joshua Masengwa wakati akisoma taarifa fupi ya shughuli za maendeleo kwa robo 2 ya Mwaka wa fedha 2022\2023 kuanzia Septemba hadi Desemba 2022, amesema kwa sasa kata hiyo inakituo kimoja cha afya cha mtu binafsi ambacho kinahudumia wananchi.

“Kwa sasa kata ya Ndala inakituo kimoja cha afya cha binafsi ambacho kinahudumia wananchi kiitwacho Inspire lakini pia wananchi wameendelea na huduma za afya kupitia kituo cha afya cha Kambarage pamoja na Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga”.

“Moja ya mpango mkuu kwa Mwaka huu wa fedha ni kuanza kujenga kituo cha afya katika eneo la mtaa wa Mlepa ambalo kwa sasa liko chini ya ofisi ya mkurugenzi wa Manispaa baada ya wananchi waliokuwa kwenye eneo hilo kuliptwa fidia”.amesema Mtendaji Masengwa

Diwani wa kata ya Ndala Manispaa ya Shinyanga mh: Zamda Shaban amefanya mkutano wa hadhara Desemba 30,2022 kwa lengo la kutoa taarifa za shughuli za maendeleo na kusikiliza kero za wananchi mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali wakiwemo wakuu wa idara katika Manispaa ya Shinyanga.

Baadhi ya wakazi wa kata ya Ndala wamempongeza Diwani huyo Zamda Shaban kwa kuendelea na utaratibu wa kufanya mkutano kusikiliza kero zao kila baada ya mienzi mitatu ambapo wamesema hali hiyo inawasaidia kupata ufumbuzi zaidi juu ya changamoto zilizopo.

Diwani wa kata ya Ndala Manispaa ya Shinyanga mheshimiwa Zamda Shaban akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara.

Mwakilishi wa mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, mratibu wa TASAF Manispaa hiyo Octavina Kiwone akizungumza kwenye mkutano huo.

Mwakilishi wa mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, mratibu wa TASAF Manispaa hiyo Octavina Kiwone akizungumza kwenye mkutano huo.

mtendaji wa kata ya Ndala Joshua Masengwa akizungumza katika mkutano huo wa hadhara.

Mwalimu wa shule ya msingi Msufini Mariam Salungi akieleza changamoto zinazokwamisha maendeleo kitaaluma shuleni hapo. 

makamu mkuu wa shule ya sekondari Ndala Alphonce Deya 

akieleza mafanikio na changamoto zilizopo katika shule ya sekondari Ndala.
M

ganga mkuu wa Manispaa ya Shinyanga Dkt. Elisha Robert 

akijibu maswali katika mkutano wa hadhara kata ya Ndala.

Kaimu meneja wa TANESCO Mkoa wa Shinyanga K

urwa Mangara akijibu maswali mbalimbali yaliyoulizwa na wananchi katika mkutano wa hadhara kata ya Ndala.
Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na  Diwani wa kata ya Ndala mheshimiwa Zamda Shaban.Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na  Diwani wa kata ya Ndala mheshimiwa Zamda Shaban.Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na  Diwani wa kata ya Ndala mheshimiwa Zamda Shaban.Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na  Diwani wa kata ya Ndala mheshimiwa Zamda Shaban.Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na  Diwani wa kata ya Ndala mheshimiwa Zamda Shaban.Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ulioandaliwa na  Diwani wa kata ya Ndala mheshimiwa Zamda Shaban.Mkutano wa hadhara ukiendelea katika kata ya Ndala ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Zamda Shaban.Mkutano wa hadhara ukiendelea katika kata ya Ndala ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Zamda Shaban.















Post a Comment

0 Comments