Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Jumla ya watoto 11
wamezaliwa katika mkesha wa krismass katika kituo cha Afya cha kambarage katika
Manispaa ya Shinyanga, kati yao wakike
ni 4 na wakiume 7 wote wakiwa na afya njema
Misalaba Blog imetembelea
na kuzungumza na muuguzi wa Wodi ya wazazi katika kituo cha afya Kambarage
Onesmo Godwin Mwamafupa ambaye amesema
kuwa jumla ya watoto hao 11 wamezaliwa katika mkesha wa kristmass
katika kituo hicho.
Mwamafupa ameeleza kuwa
watoto hao wamezaliwa wakiwa na uzito wa
kawaida na kwamba hakuna changamoto juu yao.
Aidha Misalaba Blog pia imefika katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga ambapo Muuguzi wa Wodi ya wazazi Mariam Abdallah ameeleza kuwa hakuna Mtoto aliyezaliwa katika mkesha wa sikukuu ya krismasi.
kuzungumza na muuguzi wa Wodi ya wazazi katika kituo cha afya Kambarage Onesmo Godwin Mwamafupa akizungumza na Misalaba Blog.
0 Comments