Ticker

6/recent/ticker-posts

ILI KUBOMOA MISINGI YA UKATILI, NI LAZIMA KUWALEA WATOTO KATIKA MAZINGIRA YA UTU,UPENDO NA MAADILI MEMA: ASKOFU SANGU

 

Na Mapuli Kitina Misalaba 

Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu, amewasihi wazazi, walezi na jamii nzima kuhakikisha wanawalea watoto katika misingi ya utu, upendo na maadili mema, ili vitendo vya ukatili visiendelee kutokea.

Askofu Sangu ametoa wito huo wakati wa mahubiri yake, katika Misa ya kumbukumbu ya watoto Watakatifu wafiadini, ambayo imefanyika kijimbo katika Kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga, tarehe 28 Desemba 2022, ambapo kupitia maadhimisho hayo, amepata nafasi ya pekee ya kusali, kuzungumza na kula chakula pamoja na watoto kutoka Parokia na Parokia teule zote za jimbo.

Askofu Sangu amewataka Waamini Wakatoliki pamoja na jamii nzima kuungana kwa pamoja kukabiliana na vitendo vyote vya ukatili kwa watoto, kwa kuwa vina madhara makubwa kwa kizazi cha sasa na kijacho.  “Ili Kubomoa misingi ya Ukatili, ni lazima kuwalea watoto  katika mazingira ya Utu,Upendo na Maadili Mema”. Askofu Sangu amesisitiza.

Akifafanua zaidi amebainisha kuwa, watoto wanaolelewa katika mazingira ya ukatili huendeleza vitendo hivyo pale wanapokuwa watu wazima, kwa sababu mbegu ya ukatili itakuwa imepandikizwa na kukua ndani mwao tangu utotoni.

Aidha, Askofu Sangu ametumia nafasi hiyo kuwaasa watoto kuwaheshimu wazazi kama njia ya kumtangaza Kristo, ambaye ni upendo, pamoja na kuwapenda na kuwatendea mema watu wengine.

Awali, Askofu Sangu alipokea maandamano ya watoto ambayo yalianzia katika Kanisa la Moyo Safi wa Maria Parokia ya Shinyanga mjini na kuishia katika makazai ya Askofu yaliyopo Kanisa kuu la Ngokolo, ambayo yalikuwa yamebeba ujumbe maalum wa kupinga ukatili kwa watoto.

Akielezea juu ya umuhimu wa maadhimisho hayo, Askofu Sangu amesema kuwa, Kanisa Katoliki Jimbo la Shinyanga limeamua kuunganisha maadhimisho hayo ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe 28 Desemba, ili kukumbuka watoto waliouawa kikatili na Mfame Herode zaidi ya miaka elfu mbili iliyopita akiwa na lengo la kumwangamiza mtoto Yesu, hivyo kinyume na Mfalme Herode Kanisa Katoliki Shinyanga limeamua kupaza sauti likiwa na  ujumbe maalum wa kupinga ukatili kwa watoto, ikiwa ni hatua ya kuunga mkono Juhudi za kukabiliana na vitendo hivyo zinazofanywa na Serikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan pamoja na wandamizi wake.

 Kwa mujibu wa maandiko matakatifu, Mfalme Herode alitoa amri ya kuuawa kwa watoto wote wa kiume wa kuanzia umri wa miaka  miwili, kama njia ya kulinda ufalme wake wa Yudea kwa kuamini kuwa, huenda mtoto Yesu aliye tajwa kuwa mfalme na wataalam wa nyota (Mamajusi) kutoka Mashariki angemnyang’anya ufalme wake.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Shinaga ACP Janeth Magomi ambaye alikuwa mgeni maalumu katika maadhimisho hayo, amewakumbusha wazazi, walezi na jamii nzima kuhakikisha watoto wanalindwa dhidi ya maovu wanayofanyiwa, pamoja na kuwapa haki sawa bila kuwabagua kwa misingi ya kijinsia.

Maadhimisho hayo ya kumbukumbu ya Watoto watakatifu wafiadini yamewashirikisha watoto zaidi ya 2,000 kutoka Parokia 37 na Parokia  teule 3 za jimbo la Shinyanga wakiwemo Mapadre, Watawa na Waamini.

Kaulimbiu ya maadhimisho hayo kijimbo  inasema kuwa “UKATILI KWA WATOTO SASA MWISHO”

Maandamano ya watoto yenye ujumbe unaounga mkono Juhudi za Serikali za kupinga ukatili kwa watoto wakiwa wamebeba bango la Picha ya kiongozi mkuu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu
Maandamano ya watoto yenye ujumbe unaounga mkono Juhudi za Serikali za kupinga ukatili kwa watoto wakiwa wamebeba bango la Picha ya kiongozi mkuu wa nchi Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan
Maandamano yanaendelea
Askofu Sangu akipokea maandamano ya watoto yenye ujumbe maalum wa kupinga ukatili kwa watoto katika makazi yake
Askofu Sangu akizungumza baada ya kupokea maandamano ya kupinga ukatili kwa watoto
Maandamano ya Mhashamu Baba Askofu sangu, Mapadre na Mafratel kuingia Kanisa kwa ajili ya kuanza adhimisho la Misa takatifu
Maandamano ya kuingia Kanisani yakiendelea
Askofu Sangu akiwa Kanisani wakati Misa takatifu ikiendelea, aliyekaa kushoto ni Katibu wa Askofu Padre Deusdedith Kisumo na Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mawasilano Jimbo Padre Anatoly Salawa
Baadhi ya Mapadre wakiwa katika adhimisho la Misa takatifu, wa kwanza kushoto ni Paroko msaidizi wa Parokia ya Shinyanga mjini Padre Briton Mange, wa pili ni Paroko msaidizi wa Parokia ya Lubaga Padre Paul Mahona, wa tatu ni Paroko wa Parokia ya Mt.John-Bariadi na Mkurugenzi msaidizi wa Shirka la Kipapa la utoto Mtakatifu wa Yesu Jimbo Padre Peter Mkunya, wa nne ni Paroko wa Parokia ya Ngokolo Padre Aldof Makandagu na wa mwisho ni Paroko wa Parokia ya Buhangija Padre Simon Maneno
Watumikiaji pamoja na Mapadre wakiwa katika adhimisho la Misa, wa kwanza kulia ni Paroko msaidizi wa Parokia ya Sayusayu Padre Martine Jilala, wa pili ni Paroko wa Parokia ya Mipa na Mkurugenzi wa Shirika la Kipapa la utoto Mtakatifu wa Yesu Jimbo Padre Francis Kamani na anayefuatia ni Paroko wa Parokia ya Busanda na Mkurugezni wa utume wa Walei Jimbo Padre Josephat Mahalu
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi ambaye alikuwa ni mgeni maalum akiwa katika adhimisho la Misa takatifu
Watawa na Mabinti wa malezi ya kitawa wakiwa Kanisani
Wanakwaya wakiimba Kanisani
Watoto wakiwa Kanisani
Mafratel wa wakiwa Kanisani
Askofu Sangu akitoa Sakramenti ya Kipaimara kwa watoto ambao wamesimamiwa na Familia ya Bwana na Bibi Mwl.James Msimbang’ombe
Askofu Sangu na Mapadre wakisali sala maalum ya kumwomba Mungu roho Mtakatifu awashukie Waimarishwa ambao walikuwa wanapewa Sakramenti ya kipaimara
Askofu Sangu akizungumza na Watoto, Mapadre, Watawa na Waamini waliohudhuria Misa
Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi akitoa ujumbe maalum juu ya kukomesha vitendo vya ukatili kwa watoto baada ya kupewa nafasi mara baada ya Misa iliyofanyika Kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga.
Askofu Sangu akiwa katika picha ya pmaoja na Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Shinyanga ACP Janeth Magomi pamoja na mwakilishi wa viongozi wa Serikali

Post a Comment

0 Comments