Ticker

6/recent/ticker-posts

MIAKA 20 JELA KWA USAFIRISHAJI HARAMU WA BINAADAMU MKOANI TABORA

 

………………………….

Na Lucas Raphael,Tabora

Mahakama ya hakimu mkazi ya Mkoa wa Tabora Imemuhumu kwenda jela miaka 20 Adam  Frank {31} baada ya kumtia hatiani kwa kosa la usafirishaji haramu wa binaadamu  kinyume cha sheria .

  

Akitoa hukumu hiyo jana Hakimu Mkuu Mkazi wa Mkoa wa Tabora Gabriel Ngaeje alisema hukumu hiyo iwe fundisho kwa watu wengine wenye ni kama hiyo ya kusafirishaji wa binadamu jambo ambalo likiachiwa litaku sugu .

Alisema kuwa vitendo vya kusafirisha binadamu naona linataka kuwa kubwa hivyo sharia zipo lazima kila mtu anatakiwa kuzifuata na kuacha utumikishwaji na usafirishaji wa binadamu ukomeshwe

Alisema kwamba mtuhumiwa huyo alijulikana baada ya gari alilokuwa akisafirishia raia 3 wa Kisomali kupata ajali na kuacha njia na kupinduka katika kijiji cha Makomero Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora.

Alisema mahakama imemuona mshitakiwa kuwa na  hatia kwa kosa la kusafirisha binadamu ambao ni Raia  wa Kisomali  Abdullahi Mohamesi {28} ,Zakaria Zekele {18} ,Deka Haile {27}  kinyume cha sheria za nchi.

Hakimu  Ngaeje alisema kwamba mpaka sasa Raia hao wamekwisha kudishwa kwa kwao baada ya kulipa  faini ya Laki tano kila mmoja  kwa kosa la kuingia nchini bila kibali.

Wakili wa Uhamiaji Octavian Kilatu aliiambia Mahakama hiyo kwamba tukio hilo liltokea februal 25 mwaka jana wakati mshitakiwa alikuwa akiwasafirisha Raia hao kinyume na utaratibu wa uhamiaji ambapo dereva wa Adamu Frank  akiwa anawasafirisha kwenye gari hilo  mali ya Subira Charles majira ya jioni .

Wakili huyo aliambia mahakama hiyo kuwa chanzo  cha ajali hiyo ni mwendo kasi  na kusabisha gari hilo kuacha  njia kisha kupinduka na raia hao kupata majeraha na kupelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu.

Raia hao wa Somalia walikiri kufanya kosa hilo na kutozwa faini ya laki 5 kila mmoja na ndugu zao walifika mahakamani hapo na kutoa fedha hizo ,hivyo wamerudishwa kwao.

Katika kesi hiyo mshitakiwa alitakiwa  kulipa faini ya shilingi million 20   au kwenda jela miaka 20  ambapo mshitakiwa alishindwa kulipa fedha kiasi kilichotaja na mahakama hiyo na hivyo  kupelekwa jela kutumika kifungo chake .

Post a Comment

0 Comments