ASKOFU SANGU AWASHUKURU WAZAZI NA WALEZI SHINYANGA
Misalaba0
Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu, amewashukuru wazazi na walezi ambao wamekubali watoto wao wayatolee maisha yao kwa ajili ya kumtumikia Mungu na Kanisa, kupitia shirika jipya la kijimbo la Mtakatifu Bikra Maria Mama mwenye Huruma.
Askofu Sangu ametoa shukrani hizo katika Misa ya kufunga nadhiri za kwanza za kitawa kwa Wanovisi sita na kurudia nadhiri kwa Masister wawili wa Shirika hilo la Jimbo la Shinyanga, iliyofanyika Januari 1, 2023, katika Kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga.
Amesema hayo yamewezekana kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na wazazi pamoja na walezi ya kuwalea katika misingi ya imani, uadilifu na maadili mema, hatua ambayo imewasaidia watawa hao wapya kutambua karama na wito wao wa kumtumikia Mwenyezi Mungu.
Amewataka wazazi na walezi kuendelea kupalilia misingi ya miito, ili Kanisa la Mungu liweze kuendelea kupitia miito na karama mbalimbali pamoja na kutambua kuwa, maisha ya hapa duniani ni ya kupita, bali maisha ya mbinguni ni ya milele, hivyo yanapaswa kupaliliwa.
Askofu Sangu amewapongeza watawa waliofunga nadhiri zao za kwanza pamoja na wale waliorudia nadhiri na kubainisha kuwa, wamefikia hatua hiyo huku wakiwa wamepitia changamoto mbalimbali ambazo waliweza kuzivumilia na kushinda.
Amewataka Watawa hao kuishi maisha ya sala na ibada, huku wakitambua kuwa, maisha ya kitawa hapa duniani yanatoa sura ya maisha ya mbinguni ambako hawaoi wala kuolewa.
Walelewa wa Shirika la Kitawa la Kijimbo la Mtakatifu Bikra Maria Mama mwenye Huruma wakiwa katika maandamano ya kuingia Kanisani kwa ajili ya adhimisho la Misa takatifuMhashamu Baba Askofu, Mapadre Watawa waliorudia nadhiri na wale walioweka nadhiri za kwanza wakiwa katika maandamano ya kuingia Kanisani kwa ajili ya adhimisho la Misa takatifuMafratel na Watawa kutoka mashirika mbalimbali wakiwa katika maandamano ya kuingia Kanisani kwa ajili ya adhimisho la Misa takatifu wanaofanya kazi katika Jimbo la ShinyangaWanovisi wakiwa Kanisani kabla ya kufunga nadhiri zao za kwanzaMhashamu Baba Askofu Liberatus Sangu akiendelea na adhmisho la MisaWaamini wakiwa katika adhimisho la MisaMafratel na baadhi ya Watawa wakiwa katika adhimisho la MisaMisa inaendeleaWatoto wa utoto mtakatifu pamoja na wanakwaya wakiendelea na MisaWatumikiaji wakiwa katika adhimisho la Misa takatifuMlezi wa Kiroho wa jimbo wa Shirika la Mtakatifu Bikra Maria Mama mwenye Huruma Padre Emmanuel Kahabi akisoma somo la InjiliKatibu wa Askofu Padre Deusdedith Kisumo akimkaribisha mlezi mkuu wa Wanovisi Sister Regina Muzi kwa ajili ya kuwatambulisha wanaofunga nadhirimbele ya AskofuWanovisi baada ya kuitwa mbele kwa ajili ya kuendelea na hatua za kufunga nadhiri za kwanza mbele ya Askofu wa Jimbo, wa kwanza (kushoto) ni Mnovisi Restituta Cosmas Zengo kutoka Parokia ya Maganzo Jimbo la Shinyanga, wa pili ni Felister Dotto Charles kutoka Parokia ya Nindo Jimbo la Shinyanga, wa tatu ni Gloria Asenga kutoka Jimbo la Moshi, wa nne ni Felister Deus Masumbuko kutoka Parokia ya Ngokolo Jimbo la Shinyanga, wa tano ni Magreth Michael kutoka Jimbo la Singida na wa sita ni Victoria Martine Msagawale kutoka Jimbo la Sumbawanga.Askofu Sangu akiwahoji wanovisi kuhusu nia yao ya kuishi maisha ya kitawa, aliyeshika Mic ni Paroko wa Parokia ya Mwadui Padre Michael Msabila na aliyeshika kitabu ni Katibu wa Askofu Padre Deusdedith KisumoAskofu Sangu akisali sala maalum ya kuwaombeaAskofu Sangu akibariki mavazi ya kitawa watakayovishwa baada ya kufunga nadhiri zo za kwanzaAskofu Sangu akiwakabidhi Wanovisi mavazi ya kitawa wanatakayovishwa baada ya kufunga nadhiriWanaovisi wakirudi Kanisani baada ya kuvaa magauni ya kitawa waliyokabidhiwa (isipokuwa shela) ambazo watavalishwa baada ya kufunga nadhiriSister Pascholina akirudia nadhiri zake za utawambele ya Askofu wa JimboSister Happy akirudia nadhiri zake za kitawa mbele ya Askofu wa JimboAskofu Sangu akitia saini viapo vya Watawa waliorudia nadhiriWanovisi wakifunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya kitawa mbele ya Askofu wa Jimbo na kutia sainiviapo vyaoAskofu Sangu akitia saini viapo vya wanovisi baada ya kufunga nadhiri zao za kwanzaWatawa wapya wakiimba wimbo maalum wa majitoleo kwa MunguHapo tayari ni watawa wakiwa wamevalishwa taji ishara ya ushindi, lakini wataendelea kurudia nadhiri zao mpaka watakapofunga za milele kulingana na utaratibu wa shirikaAskofu Sangu akiwapongeza mara baada ya kufunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawa katika Shirika la Mtakatifu Bikra Maria Mama mwenye HurumaMapadre wakiwapongezaMasister kutoka Mashirika mbalimbali wakiwapongeza watawa wapyaWakiwa katika nafasi zao baada ya PongeziAskofu Sangu akiwakomunishaMapadre waliohudhuria Misa hiyo wakiwa katika adhimisho la MisaAskofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawaAskofu Sangu akiwa katika picha ya pamoja na watawa wapya, mbele yao kushoto ni mlezi mkuu wa Novisiati Sister Regina Muzi na msaidizi wake Sister Eusebia SenkaAskofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawapamoja na wazazi waoAskofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawa, mbele yao ni wale waliorudia nadhiri Sister Pascholina wa kwanza kushoto na wa pili ni mwenzake Sister HappyAskofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawapamoja na walelewaAskofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawapamoja na walelewahatua ya kwanza (wasio na sare)Askofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawapamoja na wazazi waoAskofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawapamoja WAWATA jimbo ambao wamepewa jukukumu na Askofu la kulitegemeza shirika hilo kwa majitoleo mbalimbali
Post a Comment