Ticker

6/recent/ticker-posts

ASKOFU SANGU AWASHUKURU WAZAZI NA WALEZI SHINYANGA

 

Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu, amewashukuru wazazi na walezi ambao wamekubali watoto wao wayatolee maisha yao kwa ajili ya kumtumikia Mungu na Kanisa, kupitia shirika jipya la kijimbo la Mtakatifu Bikra Maria Mama mwenye Huruma.

Askofu Sangu ametoa shukrani hizo katika Misa ya kufunga nadhiri za kwanza za kitawa kwa Wanovisi sita na kurudia nadhiri kwa Masister wawili wa Shirika hilo la Jimbo la Shinyanga, iliyofanyika Januari 1, 2023, katika Kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga.

Amesema hayo yamewezekana kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na wazazi pamoja na walezi ya kuwalea katika misingi ya imani, uadilifu na maadili mema, hatua ambayo imewasaidia watawa hao wapya kutambua karama na wito wao wa kumtumikia Mwenyezi Mungu.

Amewataka wazazi na walezi kuendelea kupalilia misingi ya miito, ili Kanisa la Mungu liweze kuendelea kupitia miito na karama mbalimbali pamoja na kutambua kuwa, maisha ya hapa duniani ni ya kupita, bali maisha ya mbinguni ni ya milele, hivyo yanapaswa kupaliliwa.

Askofu Sangu amewapongeza watawa waliofunga nadhiri zao za kwanza pamoja na wale waliorudia nadhiri na kubainisha kuwa, wamefikia hatua hiyo huku wakiwa wamepitia changamoto mbalimbali ambazo waliweza kuzivumilia na kushinda.

Amewataka Watawa hao kuishi maisha ya sala na ibada, huku wakitambua kuwa, maisha ya kitawa hapa duniani yanatoa sura ya maisha ya mbinguni ambako hawaoi wala kuolewa.

Walelewa wa Shirika la Kitawa la Kijimbo la Mtakatifu Bikra Maria Mama mwenye Huruma wakiwa katika maandamano ya kuingia Kanisani kwa ajili ya adhimisho la Misa takatifu
Mhashamu Baba Askofu, Mapadre Watawa waliorudia nadhiri na wale walioweka nadhiri za kwanza wakiwa katika maandamano ya kuingia Kanisani kwa ajili ya adhimisho la Misa takatifu
Mafratel na Watawa kutoka mashirika mbalimbali wakiwa katika maandamano ya kuingia Kanisani kwa ajili ya adhimisho la Misa takatifu wanaofanya kazi katika Jimbo la Shinyanga
Wanovisi wakiwa Kanisani kabla ya kufunga nadhiri zao za kwanza
Mhashamu Baba Askofu Liberatus Sangu akiendelea na adhmisho la Misa
Waamini wakiwa katika adhimisho la Misa
Mafratel na baadhi ya Watawa wakiwa katika adhimisho la Misa
Misa inaendelea
Watoto wa utoto mtakatifu pamoja na wanakwaya wakiendelea na Misa
Watumikiaji wakiwa katika adhimisho la Misa takatifu
Mlezi wa Kiroho wa jimbo wa Shirika la Mtakatifu Bikra Maria Mama mwenye Huruma Padre Emmanuel Kahabi akisoma somo la Injili
Katibu wa Askofu Padre Deusdedith Kisumo akimkaribisha mlezi mkuu wa Wanovisi Sister Regina Muzi kwa ajili ya kuwatambulisha wanaofunga nadhiri mbele ya Askofu
Wanovisi baada ya kuitwa mbele kwa ajili ya kuendelea na hatua za kufunga nadhiri za kwanza mbele ya Askofu wa Jimbo, wa kwanza (kushoto) ni Mnovisi Restituta Cosmas Zengo kutoka Parokia ya Maganzo Jimbo la Shinyanga, wa pili ni Felister Dotto Charles kutoka Parokia ya Nindo Jimbo la Shinyanga, wa tatu ni Gloria Asenga kutoka Jimbo la Moshi, wa nne ni Felister Deus Masumbuko kutoka Parokia ya Ngokolo Jimbo la Shinyanga, wa tano ni Magreth Michael kutoka Jimbo la Singida na wa sita ni Victoria Martine Msagawale kutoka Jimbo la Sumbawanga.
Askofu Sangu akiwahoji wanovisi kuhusu nia yao ya kuishi maisha ya kitawa, aliyeshika Mic ni Paroko wa Parokia ya Mwadui Padre Michael Msabila na aliyeshika kitabu ni Katibu wa Askofu Padre Deusdedith Kisumo
Askofu Sangu akisali sala maalum ya kuwaombea
Askofu Sangu akibariki mavazi ya kitawa watakayovishwa baada ya kufunga nadhiri zo za kwanza
Askofu Sangu akiwakabidhi Wanovisi mavazi ya kitawa wanatakayovishwa baada ya kufunga nadhiri
Wanaovisi wakirudi Kanisani baada ya kuvaa magauni ya kitawa waliyokabidhiwa (isipokuwa shela) ambazo watavalishwa baada ya kufunga nadhiri
Sister Pascholina akirudia nadhiri zake za utawa mbele ya Askofu wa Jimbo
Sister Happy akirudia nadhiri zake za kitawa mbele ya Askofu wa Jimbo
Askofu Sangu akitia saini viapo vya Watawa waliorudia nadhiri
Wanovisi wakifunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya kitawa mbele ya Askofu wa Jimbo na kutia saini viapo vyao
Askofu Sangu akitia saini viapo vya wanovisi baada ya kufunga nadhiri zao za kwanza
Watawa wapya wakiimba wimbo maalum wa majitoleo kwa Mungu
Hapo tayari ni watawa wakiwa wamevalishwa taji ishara ya ushindi, lakini wataendelea kurudia nadhiri zao mpaka watakapofunga za milele kulingana na utaratibu wa shirika
Askofu Sangu akiwapongeza mara baada ya kufunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawa katika Shirika la Mtakatifu Bikra Maria Mama mwenye Huruma
Mapadre wakiwapongeza
Masister kutoka Mashirika mbalimbali wakiwapongeza watawa wapya
Wakiwa katika nafasi zao baada ya Pongezi
Askofu Sangu akiwakomunisha
Mapadre waliohudhuria Misa hiyo wakiwa katika adhimisho la Misa
Askofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawa
Askofu Sangu akiwa katika picha ya pamoja na watawa wapya, mbele yao kushoto ni mlezi mkuu wa Novisiati Sister Regina Muzi na msaidizi wake Sister Eusebia Senka
Askofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawa pamoja na wazazi wao
Askofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawa, mbele yao ni wale waliorudia nadhiri Sister Pascholina wa kwanza kushoto na wa pili ni mwenzake Sister Happy
Askofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawa pamoja na walelewa
Askofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawa pamoja na walelewa hatua ya kwanza (wasio na sare)
Askofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawa pamoja na wazazi wao
Askofu Sangu akiwa katika Picha ya pamoja na Masister wapya waliofunga nadhiri zao za kwanza za maisha ya utawa pamoja WAWATA jimbo ambao wamepewa jukukumu na Askofu la kulitegemeza shirika hilo kwa majitoleo mbalimbali

Post a Comment

0 Comments