Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu, amewashukuru wazazi na walezi ambao wamekubali watoto wao wayatolee maisha yao kwa ajili ya kumtumikia Mungu na Kanisa, kupitia shirika jipya la kijimbo la Mtakatifu Bikra Maria Mama mwenye Huruma.
Askofu Sangu ametoa shukrani hizo katika Misa ya kufunga nadhiri za kwanza za kitawa kwa Wanovisi sita na kurudia nadhiri kwa Masister wawili wa Shirika hilo la Jimbo la Shinyanga, iliyofanyika Januari 1, 2023, katika Kanisa kuu la Mama mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga.
Amesema hayo yamewezekana kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na wazazi pamoja na walezi ya kuwalea katika misingi ya imani, uadilifu na maadili mema, hatua ambayo imewasaidia watawa hao wapya kutambua karama na wito wao wa kumtumikia Mwenyezi Mungu.
Amewataka wazazi na walezi kuendelea kupalilia misingi ya miito, ili Kanisa la Mungu liweze kuendelea kupitia miito na karama mbalimbali pamoja na kutambua kuwa, maisha ya hapa duniani ni ya kupita, bali maisha ya mbinguni ni ya milele, hivyo yanapaswa kupaliliwa.
Askofu Sangu amewapongeza watawa waliofunga nadhiri zao za kwanza pamoja na wale waliorudia nadhiri na kubainisha kuwa, wamefikia hatua hiyo huku wakiwa wamepitia changamoto mbalimbali ambazo waliweza kuzivumilia na kushinda.
Amewataka Watawa hao kuishi maisha ya sala na ibada, huku wakitambua kuwa, maisha ya kitawa hapa duniani yanatoa sura ya maisha ya mbinguni ambako hawaoi wala kuolewa.
Tunapokea watoto kwa ajili ya Nursery na Primary kwa mwaka wa masomo 2024/2025.
Ada kwa Muhula:
- Nursery: 150,000/=
- Primary: 210,000/=
Usafiri na hosteli zinapatikana.
Shule ipo Basihaya-Dawasco.
Mawasiliano:
0714 927 246
0766 927 247
Nafasi ni chache sana!
ADSTERRA
OFA KUBWA YA MAFUNZO YA UOKAJI BIASHARA MWANZA NA KANDA YA ZIWA
WASILIANA NASI 0788 774 594 au 0715 224 264
OFISI YA MARIASUZY BAKERY EXPERT (SME)
Inakuletea OFA KUBWA ya mafunzo ya uokaji na uendeshaji wa biashara kwa mkoa wa Mwanza na kanda ya ziwa.
Mafunzo haya yanalenga kukupa ujuzi na mbinu bora za uokaji pamoja na usimamizi wa biashara zako ili kuhakikisha unafanikiwa katika sekta ya ujasiriamali.
Tarehe: Kuanzia 28 Oktoba 2024 hadi 1 Novemba 2024
Muda: Saa 3:00 Asubuhi hadi Saa 10:00 Jioni
Mahali: Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza
Ada:Shilingi 125,000 kwa siku 5
Malipo: Yafanyike kupitia akaunti ya Azania Bank, A/C: 001810427389 – Mary Malemi.
NB: Nafasi 10 za bure zinatolewa kwa walemavu.
Kwa mawasiliano zaidi:
Simu: 0788 774 594 au 0715 224 264
Usikose nafasi hii ya kipekee ya kuongeza ujuzi wako na kuimarisha biashara yako!
0 Comments