Ticker

6/recent/ticker-posts

MTU MMOJA AKUTWA AMEFARIKI CHUMBANI KWAKE MJINI SHINYANGA

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Mwanaume mmoja anayekadiliwa kuwa na umri wa miaka 32, Daud John amekutwa akiwa amefariki chumbani kwake katika mtaa wa Kambarage mjini Shinyanga.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo Januari 2,2023 ambapo marehemu Daud John alikuwa ni mmoja wa wapangaji wa Nyumba ya Mzee Hangwa katika mtaa wa Kambarage kata ya Kambarage Manispaa ya Shinyanga.

Misalaba Blog imefika katika eneo la tukio na kuzungumza na Mwenyekiti wa mtaa wa Kambarage Bwana Malick Juma Mbasha ambaye ameeleza kuwa amepogea taarifa hizo leo asubuhi na kwamba baada ya kufikia kwenye familia hiyo alipiga simu kituo cha polisi kutoa taarifa.

Nilikuwa ofisini kwangu asubuhi alikuja balozi wa nyumba kumi akasema kwenye nyumba ya mzee Hangwa kuna kijana amekutwa amefariki basi tumefika kwenye tukio tukaambiwa huyu kijana mara ya mwisho alionekana siku ya jana na alikuwa ndani analiza mziki lakini asubuhi ya leo tumemkuta amefariki na mziki ukiendelea”.amesema Mwenyekiti Malick Mbasha

Aidha Mwenyekiti huyo amewataka wananchi wa mtaa huo ambao hawafahamiki kwenye ofisi ya serikali ya mtaa kupeleka taarifa zao sahihi ili kuepusha changamoto pale zinapotokea.

Baadhi ya wananchi walioshuhudia tukio hilo wakiwemo wapangaji katika nyumba hiyo wamesema marehemu huyo hakuwa na tatizo lolote la kiafya na kwamba baada ya kugundua kifo chake walikuta amefariki akiwa amelala kitandani huku mziki ukiendelea kulia chumbani kwake.

Misalaba Blog pia imezungumza na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kamishna msaidizi wa Polisi Janeth Magomi ambaye amedhibitisha kifo cha Daud John.

Kamanda Magomi amesema jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linaendelea na upelelezi ili kubaini chanzo cha kifo.

Marehemu Daud John alikuwa ni Mwenyekiti wa mafundi wanaofanyakazi katika eneo la mnara wa Voda karibu na ofisi za CCM Wilaya ya Shinyanga mjini.

Wananchi wakawa katika eneo la tukio.

Post a Comment

0 Comments