" CHUO CHA USHIRIKA MOSHI TAWI LA SHINYANGA WANUFAIKA NA ELIMU YA UKATILI TOKA SMAUJATA.

CHUO CHA USHIRIKA MOSHI TAWI LA SHINYANGA WANUFAIKA NA ELIMU YA UKATILI TOKA SMAUJATA.

Na. Elias Gamaya, Shinyanga

Katika kuhakikisha jamii inaondokana na vitendo na viashiria vya ukatili wa kijinsia taasisi ya Shujaa wa Maendeleo na Usitawi wa Jamii Tanzania SMAUJATA Mkoa wa shinyanga imefika chuo kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) tawi la Shinyanga lililopo halimashauri ya manispaa ya Shinyanga mkoani humo kutoa elimu ili kuwawezesha wanachuo wajue athari za ukatili.

Akizungumza wakati wa Semina Katibu Wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Masunga Dotto Mazoya amewasihi wanachuo kuepukana na mapenzi ya jinsia moja(Ushoga na Usaganaji) yanayoharibu taifa letu ambapo kawaasa wanachuo kuachana na mila na desturi za kigeni na kusema kua Tanzania Bila ukatili inawezekana.

 " tuache mambo ya kukopikopi mila na desturi za wazungu, simu zetu tuzitumie kwa ajili ya mambo ya msingi wala si kwa ajili ya kuangalia picha zisizo faa" Amesema Katibu SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Mazoya.

Mwenyekiti idara ya michezo SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Alkwin Wille amebainisha aina za Ukatili ikiwemo Ukatili wa kingongo, Ukatili wa Kiuchumi, Ukatili wa kimwili na Ukatili wa kisaikolojia ambapo kasema ili kuwa baba au mama wa kesho lazima tuwe mabalozi kwa jamii juu ya vitendo na viashiria vya Ukatili.

 Kwa upande wake Katibu wa idara ya michezo SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Meshack Kwanja amesema maranyingi ukatili unasababishwa na watu waliokalibu, ndugu au jamaa wa karibu 

"Maranyingi ukatili unafanywa na watu waliokatibu yetu hivyo ni jukumu ka kilammoja wetu kuibua na kupinga vitendo vya ushoga kwa kupiga namba ya bure 116 nchi nzima" amesema Meshack Kwanja Katibu wa idara ya michezo SMAUJATA mkoa wa Shinyanga.

 Nao baadhi ya washiriki wa semina hiyo wameeleza namna ambavyo elimu hiyo itawasaidia kutokomeza ukatili wa kijinsia huku wengine wakiiomba serikali kuchukua hatua kali dhidi ya wale wote wanaofanya ukatili wa kijinsia , kuweka jitihada za uelimishaji dhidi ya ukatili kwenye mashirika yanayopinga vitendo hivi. 

" mimi kama mama mtarajiwa nimefurahi na elimu iliyotolewa ambayo itanisaidia katika malezi ya watoto wangu pia naweza kua mjumbe katika kuelimisha kwenye jamii kupinga ukatili wa jamii" amesema Salome Jackson mwanachuo. (MoCU) tawi la shinyanga. 

"Watoto wengi wameharibika kiseikolojia sababu ya ukatili wa kijinsia unaofanya na wazazi wao hivyo serikali hivyo serikali iziwezeshe shirika zote zinazopambana na ukatili wa kijinsia" amesema frola Shujaa Joseph mwanachuo chuo cha ushirika (MoCu) tawi la Shinyanga.

Katibu Wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Masunga Dotto Mazoya akizungumza kwenye semina hiyo.

Katibu Wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Masunga Dotto Mazoya akizungumza kwenye semina hiyo.




Post a Comment

Previous Post Next Post