Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Kmati ya utekelezaji Jumuiya ya wazazi CCM Wilaya ya
Shinyanga mjini imewaomba wanachi kata ya Ngokolo kutoa taarifa za watu
wanaoharibu miundombinu katika miradi mbalimbali maendeleo inayotekelezwa na
serikali.
Ombi hilo limetolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya
wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Bwana Fue Mrindoko wakati wa ziara ya
kamati ya utekelezaji jumuiya hiyo baada ya kutembelea na kukagua uhai wa
jumuiya ya wazazi kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti Bwana Fue amezungumzia miradi mbalimbali
inayotekelezwa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu
Hassan na kwamba amepongeza usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo unaofanywa
na viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.
Ametumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi kuilinda miradi
yote inayotekelezwa na serikali huku akisisitiza kutoa taarifa za watu
wanaoharibu miundombinu ya miradi ili hatua stahiki zichukuliwe na mamlaka
husika.
“Upo
usimamizi mzuri ambao unasimamiwa na Manispaa chini ya uongozi wa Mkurugenzi
wetu wa Manispaa ya Shinyanga ninachokiomba ni kwamba hii miradi inayojengwa na
serikali ni miradi ya wananchi sisi wananchi tunatakiwa kuisimamia kwa sababu
ni mali yetu kwahiyo tuungane kuilinda miradi yote”
“Suala
hili la baadhi ya watu kuharibu miundombinu kwa sababu ni mali ya wananchi wote
tuwe makini kuilinda miradi yetu, miundombinu yetu na kwa yeyote yule
atakayeonekana ni chanzo cha kuharibu miundombinu yetu mara moja taarifa
zitolewe kwa vyombo vya umma serikali na jeshi la polisi waweze kukamatwa ili
wachukuliwe hatua zinazostahiki”.amesema Mwenyekiti Bwana
Mrindoko
Kwa upande wake katibu wa Jumuiya ya wazazi CCM Wilaya
ya Shinyanga mjini Bi. Doris Kikabi ameipongeza serikali ya awamu ya sita kwa
kujenga madarasa na kuboresha mazingira ya wanafunzi shuleni ambapo amewasihi
wazazi kusimamia na kufuatilia mienendo ya watoto wao ili waweze kufikia
malengo yaliyokusudiwa na serikali.
Baadhi ya viongozi na wanachama wa jumuiya ya wazazi kata ya Ngokolo wameipongeza kamati hiyo huku wakiomba ziara hizo zifanyike mara kwa mara na kwamba hali hiyo itasaidia kuimarisha jumuiya za wazazi.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi CCM Wilaya ya
Shinyanga mjini Bwana Fue Mrindoko akizungumza leo Mei 15,2023.
Katibu wa Jumuiya ya wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Bi. Doris Kikabi akizungumza na jumuiya ya wazazi kata ya Ngokolo leo Jumatatu Mei 15,2023.
Post a Comment