" UMISETA YATIMUA VUMBI UWANJA WA CCM KAMBARAGE NGAZI YA WILAYA.

UMISETA YATIMUA VUMBI UWANJA WA CCM KAMBARAGE NGAZI YA WILAYA.

Na Elisha Petro

Michuano ya Umiseta manispaa ya Shinyanga  imetimua vumbi katika uwanja wa CCM Kambarage mkoa wa Shinyanga kwa michezo tofauti kucheza ikiwemo mpira wa miguu (Football),mpira wa wavu (Volleyball) pamoja na mpira wa pete (Netball).

Mchezo wa mpira wa miguu Shule ya sekondari Mwasele imefanikiwa kutwaa kombe baada ya ushindi wa goli 3-0  walioupata kufuatia kichapo walichokitoa kwa wapinzani wao kutoka Shule ya sekondari  Old Shinyanga.

 Edward Mashenene kocha na  mwalimu wa michezo katika shule ya sekondari Mwasele amewapongeza vijana wake kwa kazi nzuri walioifanya kwa kuibuka na ushindi licha ya mchezo huo kuwa wa ushindani zaidi na ameahidi kuwa mashindano ya msimu ujao watafanya vizuri zaidi ya walichokifanya msimu huu.

"Mimi huwa nakaa na vijana na binafsi niwapongeze wachezaji wangu kwa walichokifanya leo huu ulikuwa mchezo mgumu sana kwetu kwani tulilazimika kufanya mabadiliko mapema leo kwa sababu tuliyemfanyia mabadiliko mlinda mlango wetu number moja aliumia mapema wakati wa wrm up lakini kilichofanyika leo msimu ujao itakuwa zaidi ya hiki naahidi kuwafunga sana"

Kwa upande wake Simba Selemeni kocha wa timu wa timu ya Mwasele sekondari amewapongeza wapinzani wake kwa kupata matokeo mazuri katika mchezo huo na kuahidi kujipanga zaidi msimu ujao kwa lengo la kufanya vizuri zaidi ya kile walichokionyesha katika mchezo huo.

"Naipongeza timu ya Mwasele wamepata matokeo na wamecheza mpira mzuri wenzetu ni timu ya muda mrefu wanamuunganiko mzuri na wanavyocheza inaonyesha kabisa kuwa walichokipata leo ni matunda ya maandalizi yao mazuri sisi tulianza na wachezaji kidato cha kwanza lakini wamejitahidi binafsi niwaombe wazazi na hata walimu kuwaunga mkono wanafunzi katika michezo yote sisi tutarudi imara zaidi"

Kwa upande wa mpira wa wavu wasichana wa shule ya sekondari Ngokolo wameibuka kifua mbele baada ya  ushindi wa seti 3-0 dhidi ya shule ya sekondari Chamaguha lakini pia timu ya mpira wa wavu kwa wavulana kutoka shule ya Ngokolo wamefanikiwa kupata ushindi wa set 3-0 dhidi ya shule ya sekondari Chamaguha.

Kwingineko katika mpira wa pete  vijana kutoka shule ya Sekondari Mwasele wamepeperusha vyema bendera ya timu yao kwa ushindi wa jumla ya goli 48 – 23 dhidi ya timu kutoka shule ya sekondari Masekelo.

Mganga hajigangi hatimaye waalimu wakubali kufundishwa soka baada ya kupokea kichapo cha goli 3-1 katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa CCM Kambarage.

Afisa michezo Manispaa ya Shinyanga Arnold Ruzika ametoa baadhi ya changamoto mbalimbali  kwa mgeni rasmi ambaye ni Afisa Elimu sekondari Manispaa ya shinyanga ikiwa ni pamoja na kuboresha  ulinzi la usalama  katika maeneo yote yatakayokuwa yanatumika kwa michezo ya Umiseta.

"Kwanza changamoto ya kwanza ni suala la ulinzi na usalama kuna vijana wengi ambao sio wanafunzi wanaoshiriki nasi lakini wamekuwa wakihatarisha usalama wa wanafunzi msimu huu kuna baadhi ya wanafunzi wamejeruhiwa na tayari waliohusika katika hilo wapo mikononi mwa sheria, pia kuna wanafunzi wanapoteza vipaji vyao kutokana na baadhi ya walimu kuwazuia kushiriki katika haya mashindano lakini haya mashindano hayawezi kumuathiri mwanafunzi kitaaluma kwa sababu walimu wanapaswa kuwaandaa wanafunzi vizuri katika masomo na sio kuwazuia kushiriki mashindano na mwisho kuna baadhi ya shule hazina vifaa vya michezo kitu ambacho kinarudisha nyuma maendeleo ya michezo kwa vijana wetu"

Aidha Afisa Elimu sekondari manispaa ya Shinyanga Cleophace Mzungu ametoa maagizo kwa wakuu wa shule zote kuhakikisha wananunua vifaa vyote vya michezo na kuahidi kuwa atapita shule moja baada ya nyingine ili kukagua utekelezaji wa zoezi hilo.

 "Tuendeleze utaratibu wa kuendesha mashindando mashindano haya ngazi ya shule,kata,wilaya na ngazi ya taifa ili tupate vipaji bora zaidi mimi binafsi na ofsi ya mkurugenzi tunaahidi kuwapa ushirikiano pale ambapo mtakuwa mmekwama kunatatizo la baadhi ya shule kutokuwa na vifaa vya michezo natoa agizo na sio ombi kila  mkuu wa shule ahakikishe ananunu vifaa vya michezo kwa mwaka huu itakapofika mashindano ya msimu ujao kila shule iwe na vifaa vya michezo na nitafanya ukaguzi kwa kushirikiana na uongozi wa Halmashauri"

Mwisho wa michuano ya Umiseta ngazi ya wilaya iliyochezwa katika uwanja wa CCM Kambarage ni mwanzo wa maandalizi ya mashindano hayo ngazi ya Mkoa yanayotarajiwa kutimua vumbi katika uwanja wa chuo cha ualimu ShyCom uliopo Shinyanga mjini.

 

 Picha za wanafunzi kutoka shule mbalimbali za sekondari Manispaa ya Shinyanga  ikiwemo Mwasele,Masekelo,Ngokolo,Old Shinyanga pamoja na Chamaguha.

Post a Comment

Previous Post Next Post