" WADAU WAUNGANA NA CHUO CHA SAYANSI ZA AFYA KOLANDOTO KATIKA MDAHALO WA MMOMONYOKO WA MAADILI NCHINI.

WADAU WAUNGANA NA CHUO CHA SAYANSI ZA AFYA KOLANDOTO KATIKA MDAHALO WA MMOMONYOKO WA MAADILI NCHINI.

Na Elisha Petro.

Imeelezwa kuwa hali ya mmomonyoko wa maadili imechangiwa na sababu mbalimbali ikiwemo wazazi kutowajibikia jukumu la malezi na makuzi kwa watoto, na badala  yake kujikita zaidi kwenye shughuli za kutafuta kipato

Hayo yamesemwa na washiriki wa mdahalo uliohusisha wadau mbalimbali katika kujadili mada inayohusu kuporomoka kwa maadili katika jamii.

 Kaimu Mkuu wa Chuo Sayansi za Afya kolandoto,Michael Henerco anasema kuwa changamoto ya mmomonyoko wa maadili inawahusu watu wote katika jamii kufuatia  agizo la serikali ya Tanzania katika kujadili hali ya mmomonyoko wa maadili nchi na unatekelezwa katika vyuo vyote na leo chuo cha kolandoto kimechukua hatua.

" Hii changamoto ya kuporomoka kwa maadili inatuhusu sisi sote kwa sababu imetuathiri na wengine wanapoteza maisha yao na  utu tulifurahishwa na agizo la serikali kwa ajili ya kujadili hali ya mmonyoko wa maadili kwa kuwa kila mmoja hapa anaguswa na athari hizi na tumealika wataalam wabobezi wa masuala haya  ili  ya kuweza kujadiana na kupata  maoni kwa washiriki kutoka makundi mbalimbali"anasema Henerco

"Tunaomba washiriki wote kuweza kutoa maoni ili tuweze kujifunza na tuondoke hapa tukiwa mabalozi kwa kusimamia jamii  yetu kuhusu hali ya maadili na si wakati  kunyamaza kwa hali maadili ilivyo kwa sasa  kwa kuwa kila moja wetu hili lina mhusu"Anasema Henerco.


 

Kaimu mkuu wa Chuo cha Sayansi za Afya Kolandoto Michael Hernerico akifungua mdahalo wa mmomonyoko wa maadili nchi.

Akichangia katika  mdahalo huo juu ya  chimbuko la mmomonyoko wa maadili kwa mujibu wa neno la Mungu Mchungaji wa Chuo cha sayansi za Afya Kolandoto Joel Luginya  amebainisha kuwa matendo yasiyompendeza Mungu yanachangia kuporomoka kwa maadili katika jamii.

‘Mmomonyoko maana yake ni ukiukwaji wa maelekezo yaliyowekwa na Mungu au kiongozi kutoka katika jamii flani kwa ajiri ya maendeleo ya ustawi wa jamii,chimbuko la mmomonyoko wa maadili lilianzia katika bustani ya Edeni baada ya Adam na Hawa kushindwa kutekeleza magizo ya Mungu na kusikia Sauti ya muovu ibilisi kitabu cha Mwanzo 3: 1- 8 kwahiyo mmomonyoko wa maadili mzizi wake ni matokeo ya dhambi kusingekuwa na dhambi kusingekuwa na mmomonyoko wa maadili lakini Mungu ametuletea dawa ya mmomonyoko wa maadili kupitia kumwamini Mungu, kuwa na hofu ya Mungu bila kusahau kumuomba Mungu kwa kuungama na kutubu’

Mchungaji  Joel Mginya wa kanisa la AICT chuo cha sayansi za Afya Kolandoto akiwasilisha na kuchangia mada ya kwanza kuhusu chimbuko la mmomonyoko wa maadili kwa mujibu wa neno neno la Mungu.

Afisa ustawi wa jamii kutoka wizara ya maendeleo ya jamii,jinsia,wanawake na makundi maalumu  Mkoa wa Shinyanga Sophia Kang’ombe amewasilisha na kuchangia mdahalo katika mada ya pili inayohusu namna saikolojia inavyoathiri tabia na kubainisha kuwa

‘Tabia ya mtu anakuwa nayo kupitia malezi au kurithi,Mazingira anayokulia kama vile shuleni,katika maeneo yake ya kazi,nyumbani na hata katika jamii zetu yanaweza kuathiri tabia ya mtu hata hivyo tunaowajibu wa kuhakikisha makuzi na malezi bora kwa watoto ili kuepukana na mporomoko wa maadili katika jamii zetu’

Afisa ustawi wa jamii kutoka wizara ya maendeleo ya jamii,jinsia,wanawake na makundi maalumu  Mkoa wa Shinyanga Sophia Kang’ombe akiwasilisha mada inayohusu namna gani saikolojia inavyoathiri tabia Naye Afisa ustawi Mkoa wa Shinyanga,Lydia Kwesgabo akiwasilisha mada ya malezi na makuzi yanayovyochangia kuporomoka wa maadili,anasema uwajibikaji hafifu,jamii kutowajibika kama zamani kusaida watoto,umaskini wa kipato,ukosefu wa hofu ya Mungu na migogoro ya ndoa ni chanzo cha mmomonyoko wa maadili katika jamii.

"Wana ndoa waepuke migogoro na watenge muda wa ziada wa kulea watoto na wakubaliane idadi ya watoto wanaoweza kuwalea kadri ya kipato chao na hata kuepuka kuiga maisha ya mitandao ya jamii ili tusiharibu watoto"Anasema Lydia.

Afisa ustawi mkoa wa Shinyanga Bi. Lidya Kwesigabo akiwasilisha ma kuchangia mada ya malezi na makuzi yanavyoathiri mmomonyoko wa maadili nchini.

Kwa upande wake Mrakibu mwandamizi wa polisi Monica Sehere amebeinisha sababu mbalimbali zinazoweza kusababisha kuporomoka kwa maadili wakati wa kuwasilisha na kuchangia mdahalo huo juu ya ukubwa wa mmomonyoko wa maadili na madhara yake.

‘kukosekana kwa hofu ya Mungu,kupungua kwa upendo na hata imani za kushirikina ni moja ya sababu zinazoweza kusababisha mmomonyoko wa maadili lakini kunamadhara makubwa yanayoweza kutokea maadili yakishuka kwanza tutaathiri mila na desturi za taifa letu,kukosekana kwa Amani lakini pia tutaathiri maendeleo yetu na taifa kwa ujumla’

Mkuu wa dawati la jinsia jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga SSP Monica Sarehe akiwasilisha mada                            inayohusu ukubwa wa mmomonyoko wa maadili na madhara yake.

Wakati huohuo Afisa maendeleo ya jamii mkoa wa Shinyanga Tedson Ngwale akiwasilisha na kuchangia mada inayohusu namna maendeleo yanavyo sababisha mmomonyoko wa maadili  amesema maendeleo ya kidemokrasia na uhuru wa kutumia mitandao ya kijamii ni chanzo mojawapo katika hilo.

‘Maendeleo ya kidemokrasia na uhuru wa mitandao ya kijamii imetuweka hapa tulipo kwa sasa na kutusahaulisha mambo ya msingi badala yake tunaegemea katika mambo yasiyokuwa ya msingi yanayotumia muda mwingi na gharama kubwa lakini pia maendeleo ya mtu na vitu yanaongeza ubinafsi na kutufanya tushindwe kujishugulisha na masuala ya kijamii’

Afisa maendeleo mkoa wa Shinyanga Tedson Ngwale akiwasilisha na kuchangia mada inayohusu maendeleo yanavyoathiri mmomonyoko wa maadili nchini.

Ngwale ameongeza kuwa ili jamii ijikwamue katika hali mbaya ya mmonyoko wa maadili serikali inapaswa kuegemea zaidi katika ngazi za elimu kuwaelimisha watoto na jamii kwa ujumla.

‘ Niwakati wa taifa kufanya mchopeko wa mataala wa maadili kuanzia ngazi ya msingi ili watoto wajifunze maadili toka wakiwa shuleni lakini pia Wizara ya sayansi na technolojia ione namna ya kuendesha hii mitandao ya kijamii ili kuepuka matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.

Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi wa chuo cha sayansi ya Afya Kolandoto  wamebainisha njia mbalimbali zinazoweza kutumika katika kulinda maadili nchini ikiwa ni pamoja na kuiomba  serikali, wazazi  na viongozi wa dini nchini kote kushirikiana.

‘Viongozi wa Dini zote washirikiane kuisema kweli ya Mungu,Serikali izuie machapisho potoshi katika mitandao ya kijamii yanayoharibu maadili lakini pia wazazi wanapaswa kutumia lugha rafiki kwa watoto pamoja na  kutenga muda wa kuzungumza na watoto wao ili kuwajengea watoto hali ya kujitambua, Pia madawati ya jinsia yaongeze kasi ya kupambana na mmomonyoko wa maadili kwa kutoa elimu kwa watoto,wazazi na walezi’



   Mdahalo huo umefanyika katika chuo cha Afya Kolandoto ukihusisha mada inayohusu Mmomonyoko wa maadili nchini  na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa chuo,serikali, wazazi pamoja na wanafunzi wa chuo hicho.




                      Wanafunzi wa chuo cha sayansi za Afya Kolandoto wakifuatuilia mdahalo.

Madam Josephine Charles kutoka kitengo cha masoko na udahili chuo cha sayansi nza Afya                                     Kolandotoakiongoza mdahalo wa mmomonyoko wa maadili nchini.


Watumishi wa chuo cha sayansi za Afya Kolandoto wakifuatilia mdahalo wa mmomonyoko wa                                                             maadili  nchini.






                                 Baadhi ya wazazi wakiendelea kufuatilia mdahalo.









Post a Comment

Previous Post Next Post