

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe.Joseph
Modest Mkude ameongoza wananchi kufanya Usafi wa Mazingira kwaajili ya
Kujikinga na mlipuko wa Ugonjwa wa Kipindupindu katika maeneo mbalimbali ya Mji
wa Mhunze.
Shughuli hizo zilianzia eneo la soko la wajasiliamali kata ya Kishapu
ambapo wananchi nawatumishi wa taasisi
mbalimbali zilizopo ndani ya Halmashauri walifanya usafi katika mitaro ya
barabara, maeneo ya taasisi na Maeneo ya
mnadani nakumalizia kwa kufanya usafi katika eneo la Dampo.
Mhe. Mkude amewataka Wananchi wajijengee
tabia ya kufanya usafi Mara kwa Mara iwe tabia ya kudumu kwa wananchi kuwa
wasafi pamoja na mazingira yanayowazunguka
"Niwashuru
sana Wananchi pamoja na Wanafunzi mliojolitokeza leo kwenye usafi Kuna muda
tunachukulia jambo hili la usafi kama la haraka jambo la usafi inatakiwa liwe
jambo endelevu Wananchi wote inatakiwa waje ngewe uwezo wa kuwa wasafi kama
Vile ambavyo anafanya Mkurugenzi anachukua wanafunzi anawajengea tabia ya kuwa
wasafi hii itasaidia Wananchi kutunza Mazingira na Kuwa wasafi katika maeneo
yao." Alisema Mkude
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya wilaya ya Kishapu Ndugu. Emmanuel Johnson amesema kwamba swala
la Usafi liwe utamaduni na isiwe msimu wa Kipindupindu tu. na kwa upande wa
Halmashauri wamejipanga kuleta mtambo kwaajili ya kujinba shimo la taka ili iwe
rahisi kuthibiti taka, pia Halmashauri imetenga eneo kubwa la Dampo ambalo
litakuwa ni Dampo kubwa la Kishapu litahudumia wananchi wote kwa kukusanya taka
na kupelekwa katika Dampo hilo, Wananchi watashiriki kulipa Gharama za
kujusanyia Uchafu.
Naye Afisa Afya wilaya ya Kishapu Ndugu. Godfrey Kisusi amesema kwamba
Wamejipanga kikamilifu kudhibiti Mlipuko wa Ugonjwa wa Kipindupindu kwa
kuhakikisha Wanafanya ukaguzi wa Mara kwa mara kwa wananchi pamoja na kutoa
elimu ya kujikinga na Kipindupindu.
Post a Comment