" JK WALL PUTTY AFRICA LTD YAENDESHA MAFUNZO KWA MAFUNDI UJENZI NA WAUZAJI WA VIFAA VYA UJENZI MWANZA

JK WALL PUTTY AFRICA LTD YAENDESHA MAFUNZO KWA MAFUNDI UJENZI NA WAUZAJI WA VIFAA VYA UJENZI MWANZA

Kampuni ya JK Wall Puty Africa Limited imeendesha mafunzo kwa mafundi ujenzi na wauzaji wa vifaa vya ujenzi wa mkoa wa Mwanza ili kuwajengea uwezo na kuongeza ufanisi katika kazi zao za kila siku wanazozifanya


Akizungumza katika ukumbi wa mikutano wa jengo la Rock City Mall jijini Mwanza mgeni rasmi ambae pia ni mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe Hasan Elias Masala akimuwakilisha Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe CPA Amos Makala mbali na kuipongeza kampuni hiyo kwa kazi nzuri inazozifanya pamoja na kutaka kuharakishwa kwa utekelezaji wa mpango wa kampuni hiyo wa kujenga kiwanda cha kuchakata malighafi na kutengeneza bidhaa za Saruji nyeupe nchini badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi

'.. Niwasisitize katika kile mlichokisema juu ya kuanzisha kiwanda nchini kwaajili ya uchakataji wa malighafi na kutengeneza bidhaa hapa hapa nchini tofauti na awali ambapo mlikuwa mnaingiza bidhaa moja kwa moja nchini kutoka nje ..' Alisema


Aidha Mhe Masala amezisifu bidhaa za JK Wall Putty kwa namna zilivyo bora, kupatikana kwa urahisi sokoni, gharama nafuu na kupendwa na watumiaji walio wengi huku akizitaka kampuni nyengine kuiga mfano wa kampuni hiyo kwa kuwajali wateja wake na kurejesha sehemu ya faida kwao 


Nae meneja wa mauzo na masoko wa kampuni ya JK Wall Putty African LTD Kwa Kanda ya Ziwa Ndugu Michael Malili mbali na kuelezea ubora wa bidhaa zao kwa watumiaji ameongeza kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo watumiaji wa bidhaa zao pamoja na kutatua changamoto zinazowakabili ili kuongeza tija katika kazi zao 


Kwa upande wake meneja wa mauzo na masoko kutoka Kanda ya Kati Ndugu Albert Kingu amewaasa mafundi ujenzi kuendelea kutumia bidhaa za kampuni yake ya kwamba ni  nzuri, bora, zina gharama nafuu na kupatikana kwa urahisi


Paul Mtatiro ni fundi kutoka kata ya Igoma na Zaituni Nasibu ni fundi mwanamke kutoka kata ya Igogo kwa pamoja wameshukuru kutolewa Kwa mafunzo hayo na kwamba yamewajengea uwezo katika kazi zao watakazokuwa wakizifanya Kila siku na kuomba utaratibu huo uwe endelevu Ili kutatua kero na changamoto wanazokutana nazo sanjari na kuwashauri mafundi wenzao kuzingatia kilichofundishwa

Kampuni ya JK Wall Putty Africa Limited pia imetoa zawadi mbalimbali kwa wateja wake mara baada ya kuisha Kwa mafunzo hayo.

Post a Comment

Previous Post Next Post