" MAZISHI YA MWANAFUNZI WA MAZINGE SEKONDARI MANISPAA YA SHINYANGA YAFANYIKA

MAZISHI YA MWANAFUNZI WA MAZINGE SEKONDARI MANISPAA YA SHINYANGA YAFANYIKA

TAZAMA VIDEO MWILI UKIAGWA

Na Mapuli Misalaba

Mazishi ya  Msichana Joyce Hezron John mwenye umri wa Miaka 14 Mkazi wa Mtaa wa Magadula kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga, ambaye pia alikuwa ni Mwanafunzi wa kidato cha tatu Shule ya sekondari Mazinge katika Manispaa ya Shinyanga yamefanyika katika makabuli ya Dodoma kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.

Marehemu Joyce alizaliwa Februari 5, 2009 Babati Mkoani Manyara ambapo elimu ya msingi alisoma na kuhitimu 2021 katika shule ya msingi Bugoyi B iliyopo Manispaa ya Shinyanga.

Mwaka 2022 alijiunga kidato cha kwanza shule ya sekondari Mazinge iliyopo Manispaa ya Shinyanga na kwamba amefariki Mwaka huu 2024 akiwa kidato cha tatu.

Marehemu Joyce Hezron alifariki Jumamosi majira ya saa tatu usiku Januari 13,2024.

Aidha Mchungaji wa Kanisa la AICT Kambarage Charles Lugembe wakati akihubiri kwenye ibada fupi ya kumwombea marehemu Joyce Hezron ambayo imefanyika nyumbani alipokuwa anaishi, ametumia nafasi hiyo kuitaka jamii kutafuta hekima inayosaidia kujua namna ya kuishi nyakati katika maisha ya kila siku.

Mchungaji Lugembe amewakumbusha watanzania kuendelea kuishi maisha ya kumpendeza mwenyezi Mungu huku akisisitiza  kuacha tabia za kupuuza mafundisho ya viongozi wa Dini.

Pia amesema katika kuishi maisha ya Duniani ni vyema kila mtu kuwa na utaratibu wa kufikiria maamuzi sahihi na siyo kufanya maamuzi mabaya ambayo hayampendezi Mungu ambapo amehimiza kujiepusha na mambo mabaya.

Askofu wa Kanisa la AICT Dayosisi ya Shinyanga Zakayo Bugota ameshiriki ibada ya kumwombea marehemu Joyce Hezron ambapo ibada hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali, jamii na wadau wakiwemo viongozi wa kampeni ya kupinga ukatili SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga.

  

Zoezi la kuaga mwili wa marehemu Joyce Hezren likiendelea.


 

Post a Comment

Previous Post Next Post