" MWANAFUNZI ALIYEOLEWA BAADA YA KUFAULU KUINGIA KIDATO CHA KWANZA AREJESHWA SHULENI MKOANI SHINYANGA

MWANAFUNZI ALIYEOLEWA BAADA YA KUFAULU KUINGIA KIDATO CHA KWANZA AREJESHWA SHULENI MKOANI SHINYANGA

Na Mapuli Misalaba

Serikali Mkoani Shinyanga imefanikiwa kumrejesha shule binti mkazi wa kijiji cha Iyugi kata ya Lyamidati Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ambaye aliolewa baada ya kufaulu kuingia kidato cha kwanza Mwaka huu 2024.

Hayo yamebainishwa na mkuuwa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema, mwanafunzi huyo alipata ufaulu wa wastani wa A katika mtihani wake wa kumaliza darasa la saba.

Mwanafunzi huyo aliozeshwa baada ya kumaliza darasa la saba ambapo familia ile inasemekana kuchukua mahari ya jumla ya Ng’ombe 15 na kumruhusu binti huyo kwenda kuanzisha maisha ya ndoa ambapo serikali imefanikiwa kumrejesha shule mpaka sasa anaendelea na masomo.

“Katika hali ya kusikitisha baadhi ya wazazi badala ya kuwapeleka shule watoto wanawaozesha tukio hili limetokea Mkoani Shinyanga katika kata ya Lyamidati kijiji cha Iyugi mzazi mmoja mtoto wake amefaulu vizuri sana kwa wastani wa A Mzazi huyo aliamua kumuozesha mtoto wake  kwa kupokea mahari ya Ng’ombe 15”.

 “Nawashukuru sana wananchi waliotupatia taarifa hiyo takini pia nawashukuru viongozi  pamoja na jeshi la polisi kwa kuhakikisha kwanza mtoto huyu anaondolewa kwenye Ndoa na kuja kuendelea na masomo yake shuleni”.

“Na huyu mzazi aliyeozesha mtoto amekimbia tunaendelea kumsaka popote alipo tumfikishe katika vyombo vya sheria na niwaombe wanaume acheni kuoa wanafunzi waacheni wapate haki yao”. amesema RC Mndeme

“Niwaombe sana wazazi tusimtumie mtoto wa kike kama chombo cha kujipatia mali na utajili na kumkosesha haki yake ya elimu, wazazi wote wanaoendelea kuwakatisha ndoto watoto wao hususan watoto wa kike kuwaozesha suala hilo halikubaliki tutaendelea kuwachukulia hatua za kisheria na wale watoto watarudishwa shuleni  na nitoe wito kama kuna mzazi mwingine ameshapokea mahari naomba arudishe wampoleke mtoto shule ukigundulika tutakuchukua hatua”.amesema RC Mndeme

Post a Comment

Previous Post Next Post