" MWANAFUNZI WA SEKONDARI MANISPAA YA SHINYANGA AFARIKI DUNIA CHANZO CHADAIWA KUNYWA SUMU, MWENYEKITI AELEZA

MWANAFUNZI WA SEKONDARI MANISPAA YA SHINYANGA AFARIKI DUNIA CHANZO CHADAIWA KUNYWA SUMU, MWENYEKITI AELEZA

Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Magadula Humphrey Mtafungwa akizungumza na Misalaba Media

Msichana Joyce Hezron anayekadiriwa kuwa na Miaka 17  Mkazi wa Mtaa wa Magadula kata ya Ngokolo Manispaa ya Shinyanga, ambaye pia ni Mwanafunzi wa kidato cha tatu Shule ya sekondari Mazinge katika Manispaa ya Shinyanga amefariki Dunia kwa kile kinachosadikiwa kuwa kifo chake kimetokana na kunywa sumu

Kwa Mujibu wa Watu walioshuhudia tukio hilo wameeleza kuwa chanzo cha kifo chake kimetokana na kunywa sumu,baada ya kugombezwa na Babu yake, akituhumiwa kutumia fedha  iliyotumwa kwenye simu yake kwa bahati mbaya.

Wameeleza kuwa kabla ya kifo chake Msichana huyo alipokea mwamala wa fedha kiasi cha shilingi elfu sitini,ambayo ilitakiwa kutumwa kwa Bibi yake lakini kwa bahati mbaya ikaingia kwake na kwamba aliitumia  kwa matumizi binafsi bila idhini ya wakubwa

Misalaba Media,imezungumza na Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa Magadula Humphrey Mtafungwa ambaye amekiri kuwa na taarifa za kifo cha msichana  huyo mkazi wa  mtaa wake,ambapo ametumia nafasi hiyo kuwaomba wazazi na walezi kuwa karibu na watoto wao ili kuwaelekeza zaidi kuhusu mambo yanayofaa na yasiyofaa.

“Asubuhi kwenye saa mbili na nusu nilipigiwa simu na balozi akinitaarifu kuwa katika mtaa wangu kuna msiba umetokea usiku wa jana saa nne, nilipofika kwenye eneo la tukio niliongea na familia wakanieleza kweli msiba umetokea na alikuwa ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya Mazinge sekondari mpaka sasa hivi taratibu za maziko zinaendelea tunatarajia kuhifadhi mwili siku ya Jumanne”.amesema Mwenyekiti Mtafungwa


Post a Comment

Previous Post Next Post