" IBADA YA LEO JUMAPILI KATIKA KANISA LA AICT KAMBARAGE MJINI SHINYANGA, ASKOFU BUGOTA AWAKUMBUSHA WAKRISTO KUMTUMAINI MUNGU 2024

IBADA YA LEO JUMAPILI KATIKA KANISA LA AICT KAMBARAGE MJINI SHINYANGA, ASKOFU BUGOTA AWAKUMBUSHA WAKRISTO KUMTUMAINI MUNGU 2024

Na Mapuli Misalaba

Askofu wa Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT Dayosisi ya Shinyanga Zakayo Bugota amewakumbusha wakristo kuendelea kumtumainia Mungu katika maisha ya kila siku

Ameyasema hayo leo wakati akihubiri kwenye ibada ya Jumapili katika Kanisa la AICT Kambarage mjini Shinyanga ambapo amesema ni muhimu kila mtu kuwa na matumaini mapya kwa  Mungu Mwaka huu 2024.

Amewahimiza wakristo kuwa sehemu ya kugusa maisha ya watu wengine kwa majitoleo yao huku akiwaomba watanzania kuwa wabunifu katika maisha ya kila siku wawapo katika Familia, Biashara pamoja na kazi mbalimbali kama sehemu ya kuimarika kiuchumi.

Askofu Bugota amewaasa wakristo kuendelea kuliombea Taifa la Tanzania kuepukana na athari zitokanazo na majanga ya mvua huku akiwakumbusha kujijengea utaratibu wa kumshukuru Mungu hasa wawapo katika Nyumba za ibada.

Kanisa la AICT Kambarage ni moja ya makanisa yanayohubiri na kufundisha injili ya Yesu Kristo kwa usahihi na kumhudumia Mwanadamu katika ukamilifu wake kwa msingi wa neno la Mungu.Askofu wa Kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT Dayosisi ya Shinyanga Zakayo Bugota akihubiri kwenye ibada hiyo.Kwaya ya AICT Kambarage ikiimba kwenye ibada ya Jumapili leo.

Post a Comment

Previous Post Next Post