" SHIRIKA LA COMPASS TANZANIA LAGAWA MICHE YA MITI 400 KATA YA ITWANGI NA NSALALA MKOANI SHINYANGA

SHIRIKA LA COMPASS TANZANIA LAGAWA MICHE YA MITI 400 KATA YA ITWANGI NA NSALALA MKOANI SHINYANGA

Na Mapuli Kitina Misalaba

Shirika lisilo la kiserikali la Compass Tanzania limegawa miche ya miti mia mbili (400) katika kata ya Itwangi pamoja na kata ya Nsalala Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali katika hatua za utunzaji wa mazingira.

Akigawa miche hiyo Afisa maendeleo wa kata ya Tinde Bi. Eva Mlowe amesema serikali inatambua mchango unaofanywa na mashirika yasiyoyakiserikali kwa lengo la kutatua changamoto zinazoikabili jamii.

Afisa maendeleo  amepongeza juhudi za shirika la Compass Tanzania kwa kuendelea kuunga mkono maono ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika utunzaji wa mazingira.

“Shirika la Compass Tanzania nimekuja wakati muafaka tunajivunia uwepo wa shirika hili katika kata ya Tinde kwa sababu ninaenda sambamba na sera ya Nchi kwa kweli wanamuunga mkono Mama Samia kwa kuifanya Tanzania kuwa ya kijani kwa kutunza mazingira”.amesema Afisa maendeleo Bi. Eva Mlowa

Mtendaji wa kata ya Nsalala Paul Kulwa amelishukuru shirika la Compass kwa kutoa miche ya miti mia mbili (200) ambayo waliomba ili wapande katika mazingira ya kata hiyo huku akiahidi kuilinda ili iweze kustawi vizuri.

Kata ya Nsalala miti hiyo itapandwa katika shule ya msingi Nshishinulu, Zahanati mpya ya Nshishinulu pamoja na ofisi ya kata ya Nsalala.

Aidha kata ya Itwangi miche hiyo itapandwa shule ya sekondari Imenya  pamoja na Zahanati ya Butini iliyopo kata ya Itwangi Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

 Kwa upande wake meneja miradi wa shirika la Compass Tanzania Bwana Boniface Mhana amesisitiza juu ya utunzaji wa miti hiyo huku akiahidi kutembelea kwenye vituo ambavyo vimepanda miti ili kufuatilia hatua za ukuaji wa miti hiyo.

Meneja huyo amesema shirika la Compass Tanzania kuanzia Mwezi Disemba Mwaka 2023 hadi  Januari Mwaka huu 2024 limegawa miche ya miti 5000 kama sehemu ya kutunza na kuhifadhi mazingira.

Mhana amesema shirika hilo litaendelea kugawa miti kwenye taasisi za serikali na binafsi, wadau mbalimbali na jamii kwa ujumla ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za serikali katika utunzaji wa mazingira na kwamba shirika hilo linatarajia kugawa miche ya miti kata ya Puni, Didia na taasisi za Dini katika Mkoa wa Shinyanga.Akigawa miche hiyo Afisa maendeleo wa kata ya Tinde Bi. Eva Mlowe akimkabidhi miche ya miti mtendaji wa kata ya Itwangi. Zoezi la kuchukua miche ya miti iliyotolewa na shirika la Compass Tanzania likiendelea.

Post a Comment

Previous Post Next Post