" SMAUJATA MKOA WA SHINYANGA YAFANYA ZIARA WILAYA YA KAHAMA, VIONGOZI WAKUMBUSHWA KUWA WAZALENDO

SMAUJATA MKOA WA SHINYANGA YAFANYA ZIARA WILAYA YA KAHAMA, VIONGOZI WAKUMBUSHWA KUWA WAZALENDO

Imeandaliwa na idara ya habari SMAUJATA Wilaya ya Kahama.

Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa jamii Tanzania (SMAUJATA) mkoani Shinyanga wametakiwa kuendelea kujikita zaidi katika kufanya kazi kwa vitendo na sio maneno pamoja na kuwa wazalendo kwa kuibua vitendo vya ukatili wa kijinsi vinavyofanyika kwa wanawake, watoto na wazee mkoani humo.

Kauli hiyo ametolewa  na kaimu mkuu wa wilaya ya Kahama JOSEPH MKUDE wakati wa viongozi wa SMAUJATA walipokuwa wakitambulisha baadhi ya viongozi wapya wa wilaya Kahama kwa mwaka 2024, huku wakiombwa kufanyakazi kwa kujitoa ili kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye jamii inatuzunguka.

Aidha, MKUDE amesema kuna kila sababu serikali kuwa na ushirikiano na SMAUJATA kupinga na kufufua vitendo vya ukatili vinavyoendelea katika mkoa wa shinyanga pamoja kutoa elimu kwa wananchi ili kupunguza ama kutokomeza ukatili huo ambao una athari kubwa kwa jamii ambapo waathrika wakubwa ni wanawake, watoto na wazee.

“Sisi ni watu wa kijitolewa na tufanyekazi kwa vitendo kwa ajili ya nchin yetu, tukubali kufanya kazi kwa kuwa tatizo ni kubwa sana kuliko tunavyofikiria kwa hiyo tunapaswa kufanya kazi kweli kweli, alisema Mkude.

Naye, mwenyekiti wa SMAUJATA mkoa wa Shinyanga NABILI KISENDI, amesema kuwa kumekuwepo na changamoto ambazo wakati mwingine wanashindwa kufika maeneo ya mbali hasa vijiji hali inayosababisha kushindwa kuibua vitendo vya ukatili na kuomba serikali kuendelea kutoa ushirikiano namna ya kufika maeneo hayo.

Amesema kuwa wameendelea kutoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia katika wilaya tatu za mkoa wa shinyanga kwa kufanya mikutano ya hadhara kwa wananchi, mashuleni pamoja kwenye vikao vya wakina mama vikoba, pamoja na kuwataka SMAUJATA kupaza sauti kwa kupinga ukati na kutomeza.

Kwa upande wake kaimu afisa tawala wa wilaya ya kahama VICENTI NDESEKIO katika kikao hicho alisema kuwa jukumu la kupinga ukatili wa kijinsi ni la pamoja na kupambana kulitokomeza na pia kuwataka waendelee kufanya kazi hizo ya kizalendo ili kuokoa kizazi kijacho katika kutoa elimu ya mmonyonyoko wa maadili.

Menyekiti wa maadili SMAUJATA mkoa wa Shinyanga SOLOMONI NAJULWA almaafu CHEUPE, ameomba viongozi wa SMAUJATA mkoani humo wawaze kutambuliwa kwenye sherehe, makongamano na mikutano ya kiserikali ili waweze kutoa elimu pamoja na kutoa vizuizi kwa baadhi ya taasisi za kiserikali kama vile hospitali na mashuleni na ili kuweza kutekeleza majukumu yao ya kupinga na kutokomeza ukatili kijinsia.

“Ofisi za mkurugenzi pamoja na maafisa ustawi na maendeleo ya jamii mkoa wa shinyanga zinapaswa kuwatambua SMAUJATA na kupewa heshima zote kana kwamba wao ni sehemu ya chombo ambacho kinaweza kumasidia Dkt Rais SAMIA HASANI pamoja na wandaamizi wote kwa kumaanisha sisi ni jukumu letu la kupambana kwa kuporomoka kwa maadili alisema Najulwa.

Hata hivyo katibu wa SMAUJATA mkoa wa shinyanga DANIEL KAPAYA alisema mpaka sasa wana kampeni ya miaka mitatu toka mwaka 2022, yenye lengo la kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia nchi nzima ambapo wanashirikiana na maafisa maendeleo ya jamii na ustawi wa jamii pamoja na viongozi wote wa serikali ikiwa chini ya wazira ya maendeleo ya jamii jinsia na wanawake na makundi maalum Dr DOROTHY GWAJIMA.

Kikao cha pamoja cha viongozi wa SMAUJATA Mko wa Shinyanga na kaimu mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Joseph Mkude kikiendele.Picha ya pamoja

 

 

 Viongozi mbalimbali wa SMAUJATA Mkoa na viongozi kutoka katika Halmashauri za Wilaya ya Kahama wakiwa katika kikao baada ya kutembelea sehemu mbalimbali.




Post a Comment

Previous Post Next Post