" UMOJA WA MAKANISA YA KIPENTEKOSTE WILAYA YA SHINYANGA WAPATA VIONGOZI WAPYA.

UMOJA WA MAKANISA YA KIPENTEKOSTE WILAYA YA SHINYANGA WAPATA VIONGOZI WAPYA.

Na Mapuli Kitina Misalaba

Umoja wa Makanisa ya Kipentekoste Wilaya ya Shinyanga umefanya uchaguzi wa viongozi ngazi mbalimbali ambapo Mwenyekiti wa umoja wa makanisa ya Kipendekoste Wilaya hiyo ni  Pr. Thomas Batenga kutoka Kanisa la International Evangelical Assembilies of God (IEAGT).

 Uchaguzi huo umefanyika katika Kanisa la International Evangelical Assembilies of God (IEAGT)  ambao umesimamiwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Makanisa ya Kipentekoste Mkoa wa Shinyanga Mchungaji David Hamad pamoja na  Katibu wa umoja huo Mkoa Mch. Sondole.

 Wasimamizi wa uchaguzi huo wamewatangaza viongozi walioshinda ambapo  Mwenyekiti wa umoja wa makanisa ya Kipendekoste Wilaya ya Shinyanga ni  Pr. Thomas Batenga kutoka  kanisa la FPCT na kwamba  Makamu Mwenyekiti ni Winifrida Kashumba wa kanisa la IEAGT huku  Katibu wa umoja huo Wilaya ya Shinyanga ni Mch. Selemani wa kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG)

Wajumbe wengine waliochaguliwa ni Mch. Benjamin Mayunga wa kanisa la HOSANA pamoja na Mch. Boni wa kanisa la New Harvest Ministry.

Katika mahubiri yake Askofu Valelian Kway wa Deeper Life amewataka viongozi waliochaguliwa kuendelea kuwa waaminifu katika maneno na matendo yao ikiwa ni pamoja na kuwa wabunifu ili kufikia malengo ya umoja wa makanisa hayo.

Kwa upande wake Askofu Mkuu David Mabushi wa kanisa la  IEAGT amewaasa viongozi hao kuzingatia muda na malengo ya umoja wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania( CPCT) katika kuwatumikia waamini wa makanisa hayo.

Naye Mwenyekiti wa CPCT Mkoa wa Shinyanga Mch. David Hamad kutoka kanisa la Agape Life, amewasistiza viongozi waliochaguliwa kufuata Katiba na kuweka taratibu bora za kuwaunganisha Wachungaji wote wa Kipentekoste na Madhehebu mengine ili umoja huo uweze kuimarika zaidi.

Aidha amewakumbusha Viongozi waliochaguliwa kuendeleza uhusiano mwema kati ya CPCT na Serikali ya wilaya ya Shinyanga, Halmashauri na vyombo vya ulinzi.

Mwenyekiti Pr. Thomas Batenga amewashukuru wajumbe kwa kumwamini katika nafasi hiyo ambapo ameahidi kuitumikia vema nafasi hiyo huku akiwaomba ushirikiano ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Wajumbe waliohudhuria uchaguzi huo  wamepongeza kwa mwendelezo wa kuchaguza viongozi bora na kuwatakia viongozi wao baraka za Mungu.


Post a Comment

Previous Post Next Post