Na Mapuli Kitina Misalaba
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha mtakatifu Joseph (St Joseph’s) tawi la
Shinyanga wamefanya zoezi la usafi wa
mazingira, uchagiaji damu salama pamoja na kutembelea wagonjwa katika kituo cha Afya Kambarage Manispaa ya Shinyanga.
Akizungumza Rais wa serikali ya
wanafunzi chuo cha mtakatifu Joseph tawi la Shinyanga Ridhiwani Ramadhani
amesema baadhi ya wanafunzi hao wameguswa na kuamua kuunga mkono kampeni ya
uchagiaji damu salama ili kusaidia wenye uhitaji.
Ametumia nafasi hiyo kuziomba taasisi mbalimbali
na jamii kwa ujumla kuwa na utaratibu wa
kuchagia damu salama kwani itasaidia kuokoa watu wenye uhitaji wa
damu salama.
Rais huyo wa serikali ya wanafunzi
katika chuo cha mtakatifu Joseph tawi la
Shinyanga Ridhiwani Ramadhani pia ameikumbusha jamii kuendelea kuzingatia usafi
wa mazingira ili kuepuka magonjwa ya mlipuko ikiwemo Kipindupindu.
Baadhi ya wanafunzi na viongozi wengine
wa serikali ya wanafunzi katika chuo hicho ambao wameshiriki zoezi la
uchangiaji damu salama pamoja na usafi wa mazingira kwenye kituo cha Afya
Kambarage wamesema watandelea kuwa na majitolea kwa watu wenye uhitaji.
Mwanafunzi wa chuo cha mtakatifu Joseph
tawi la Shinyanga akichangia kutoa damu salama katika kituo cha Afya Kambarage
mjini Shinyanga.
Mwanafunzi wa chuo cha mtakatifu Joseph
tawi la Shinyanga akichangia kutoa damu salama katika kituo cha Afya Kambarage
mjini Shinyanga.
Rais wa serikali ya wanafunzi chuo cha
mtakatifu Joseph tawi la Shinyanga Ridhiwani Ramadhani upande wa kushoto
akichangia damu salama katika kituo cha Afya Kambarage.
Mwanafunzi wa chuo cha mtakatifu Joseph tawi la Shinyanga akichangia kutoa damu salama katika kituo cha Afya Kambarage mjini Shinyanga.
Mwanafunzi wa chuo cha mtakatifu Joseph tawi la Shinyanga akichangia kutoa damu salama katika kituo cha Afya Kambarage mjini Shinyanga.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha mtakatifu Joseph (St Joseph’s) tawi la
Shinyanga wakifanya zoezi la usafi
katika maeneo yanayozunguka kituo cha Afya Kambarage kilichopo Manispaa ya
Shinyanga.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha mtakatifu Joseph (St Joseph’s) tawi la
Shinyanga wakifanya zoezi la usafi
katika maeneo yanayozunguka kituo cha Afya Kambarage kilichopo Manispaa ya
Shinyanga.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha mtakatifu Joseph (St Joseph’s) tawi la
Shinyanga wakifanya zoezi la usafi
katika maeneo yanayozunguka kituo cha Afya Kambarage kilichopo Manispaa ya
Shinyanga.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha mtakatifu Joseph (St Joseph’s) tawi la
Shinyanga wakiwa kwenye picha ya pamoja
baada ya kufanya usafi wa mazingira katika kituo cha Afya Kambarage mjini
Shinyanga.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha mtakatifu Joseph (St Joseph’s) tawi la
Shinyanga wakiwa kwenye picha ya pamoja
baada ya kufanya usafi wa mazingira katika kituo cha Afya Kambarage mjini
Shinyanga.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo cha mtakatifu Joseph (St Joseph’s) tawi la
Shinyanga wakiwa kwenye picha ya pamoja na
wataalam wa Maabala wa kituo cha Afya Kambarage mjini Shinyanga.
Post a Comment