" WANAFUNZI WALIOFUTIWA MATOKEO KIDATO CHA PILI NA DARASA LA NNE 2023, TAZAMA HAPA

WANAFUNZI WALIOFUTIWA MATOKEO KIDATO CHA PILI NA DARASA LA NNE 2023, TAZAMA HAPA

Baraza la Mitihani Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya kitaifa ya upimaji wa darasa la nne na kidato cha pili uliofanyika mwaka 2023 ambapo ufaulu umeongezeka kwa asilimia 0.13 kwa kidato cha pili na asilimia 0.39 kwa darasa la nne.

Akitangaza matokeo hayo leo Jumapili, Januari 7, 2024 Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Said Mohamed amesema baraza hilo  limefuta matokeo kwa wanafunzi 178 wa darasa la nne na 28 wa kidato cha pili waliofanya udanganyifu.

Pia baraza limewafutia matokeo wanafunzi watatu wa darasa la nne na 14 wa kidato cha pili walioandika matusi.

Aidha amesema katika masomo ya darasa la nne, matokeo yanaonyesha ufaulu wa sayansi na teknolojia ukifikia asilimia 86.86 kutoka asilimia 83.19 ya mwaka 2022 na somo la hisabati likifiki asilimia 54.00 kutoka asilimia 49.7.

Kwa kidato cha pili, ufaulu wa somo la uraia umeimarika kutoka asilimia 31.12 mwaka 2022 hadi kufiki asilimia 48.27.

Katibu huyo amefafanua kuwa  matokeo ya darasa la nne, wanafunzi 1,287,934 sawa na asilimia 83.34 wamefaulu kuendelea na darasa la tano.

Lakini katika upande wa kidato cha pili, wanafunzi 592,741 ambao ni sawa na asilimia 85.31 wamefaulu kwa daraja la kwanza hadi la nne.

MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2023 NA KIDATO CHA PILI (FTNA) 2023 YAMETANGAZWA.

MATOKEO YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE (SFNA) 2023

Post a Comment

Previous Post Next Post