Na Mapuli Misalaba,
Moshi Ndugulile
Wakazi wa kata ya
Ndembezi Manispaa ya Shinyanga wamewaomba wakala wa Barabara mijini na vijijini
TARURA Mkoa wa Shinyanga kukarabati daraja linalounganisha mawasiliano ya kata
hiyo na maeneo mengine ambalo limekatika kutokana na Mvua zinazoendelea
kunyesha.
Wakizungumza na Misalaba
Media ilipotembelea katika daraja hilo wamesema kuharibika kwa daraja hilo imekuwa
ikikwamisha shughuli za kiuchumi kutokana na kukatika kwa mawasiliano kutoka
sehemu moja kwenda sehemu nyingine.
Wamesema changamoto
hiyo inahusisha pia wanafunzi wanaotumia daraja hilo ambao wamekuwa wakichelewa
masomo darasani kwa sababu ya kuzunguka.
Wananchi hao wameiomba
TARURA kutengeneza daraja hilo kwa kiwango chenye ubora ili liweze kudumu kwa
muda mrefu kwani limekuwa likitengenezwa na kuharibika mara kwa mara hivyo
kuitia hasara serikali.
Misalaba Media
imezungumza na meneja wa wakala wa barabara za mjini na vijijini TARURA Mkoa wa
Shinyanga mhandisi Oscar Gilbert kwenye eneo la tukio ambaye ameahidi
kushughulikia changamoto hiyo ili kuondoa usumbufu kwa wananchi wanaotumia
daraja hilo.
Hata hivyo injinia
Gilbert amesema mpango uliopo ni kuwasiliana na mamlaka ya reli kwa kuwa daraja
hilo limejengwa kwenye hifadhi ya reli.
Mwananchi akivuka katika daraja linalounganisha Ndembezi Mazinge na Ndembezi
Bushimangila kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Mwonekano wa daraja linalounganisha Ndembezi Mazinge na Ndembezi Bushimangila kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Mwonekano wa daraja linalounganisha Ndembezi Mazinge na Ndembezi
Bushimangila kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Mwonekano wa daraja linalounganisha Ndembezi Mazinge na Ndembezi Bushimangila kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Meneja wa wakala wa
barabara za mjini na vijijini TARURA Mkoa wa Shinyanga mhandisi Oscar Gilbert akiangalia
hali ya changamoto katika daraja linalounganisha
Ndembezi Mazinge na Ndembezi Bushimangila kata ya Ndembezi Manispaa ya
Shinyanga.
Meneja wa wakala wa
barabara za mjini na vijijini TARURA Mkoa wa Shinyanga mhandisi Oscar Gilbert akiangalia
hali ya changamoto katika daraja linalounganisha
Ndembezi Mazinge na Ndembezi Bushimangila kata ya Ndembezi Manispaa ya
Shinyanga.
Post a Comment