
Na Suzy Butondo, Misalaba Media
Mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini ambaye pia ni
naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu
Patrobas Katambi amewaomba viongozi wa
CCM na serikali kushirikiane nae katika kufanya shughuli mbalimbali za kimaendeleo
na kutatua kero mbalimbali za wananchi
ili waweze kufanya maendeleo makubwa katika jimbo la Shinyanga.
Hayo ameyasema wakati akizungumza na wananchi wa jimbo la Shinyanga katika kata
ya Kitangili, ambapo amesema ili kuweza kuijenga Shinyanga ni vizuri kuwa
wamoja na kushirikiana katika kufanya kazi za maendeleo, kuwahudumia wananchi na kuwaondolea
manung"uniko .
Katambi amesema wananchi wanatarajia kuona
maendeleo makubwa katika maeneo yao,
ambayo mengi tayari yamefanyiwa kazi,barabara zilikuwa hazipitiki madaraja
yalikuwa hayapo, lakini kwa sasa barabara zinapitika, zahanati, mashule bado
kero ndogo ndogo ambazo zinatakiwa kutatuliwa, ambapo ameahidi kuzifanyia kazi
wakati wowote.
"Niwaombe
wananchi muwaamini viongozi wenu kuanzia ngazi za mitaa,kata madiwani mbunge na
Rais kwa kuwaletea miundombinu ya barabara zahanati, mashule na ninaamini
tutaendelea kuboresha huduma mbalimbali za kijamii,"amesema
Katambi.
"Leo
naomba niwatajie michango mbalimbali nilioitoa katika jimbo langu kwa kipindi
cha January hadi Murch 2024,kwa taasisi za dini na jamii, ikiwemo kwenye Chama cha mapinduzi CCM na jumuiya
zake .kwa ajili ya makongamano mabaraza na ugeni mbalimbali wa jumuiya zetu jumla milioni 41.7"amesema
Katambi.
Aidha amesema january hadi Decemba 2023 aliwawezesha
wajasiliamali 910 kupata semina na kuwawezesha gharama za nauli na chakula
jumla shilingi milioni 75, ikiwa ni pamoja na kuwezesha wajasiliamali na
viongozi kupata semina ya matumizi ya majiko ya gesi na kugawa majiko ya gesi 1,680
pamoja na nauli jumla ya Shilingi milioni 92.4
“Jimbo
langu linakata 17, ambapo kata zote tayari nimegawa fedha kutoka mfuko wa jimbo
kwa ajili ya kuchochea utekelezaji wa
miradi ya maendeleo 2024, kuboresha huduma zote za kijamii zikiwemo huduma mbalimbali
za kijamii katika kata zote jumla Shilingi milioni 62.6”.
"Machungu
yangu ni kuhakikisha kila mmoja tunaungana pamoja na kuhakikisha masikini
anatendewa haki, tajili anatendewa haki, usaliti na roho mbaya sio mzuri
tuungane kwa pamoja ili tuweze kuijenga Shinyanga yetu., mimi kazi yangu ni
kufanya maendeleo, hivyo niwaombe viongozi wenzangu tuwatumikie wananchi wetu
na tuhakikishe katika uchaguzi tunapata ushindi kwa kishindo"ameongeza
Katambi.
Katambi
alimuomba Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi CCM wilaya ya Shinyanga asimame imara na kamati yake siasa ili kuhakikisha wananchi
wanapata huduma zinazohitajika kwenye jamii na kwuwataka madiwani kusimamia miradi mbalimbali ya serikali
inayoendelea kutekelezwa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Samia
Suluhu.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Kitangili Mariam
Nyangaka amesema yuko pamoja na mbunge katika kuhakikisha maendeleo
yanapatikana katika kata ya Kitangili kwani mpaka sasa kuna mabadiliko makubwa
katika barabara na madaraja kulikuwa na shida kubwa lakini kwa sasa wananchi
wana amani.

Post a Comment