Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga
linaendelea kuwatafuta watu watatu wanaotuhumiwa kwa kosa la kumshambulia
Seleman James Mabula, kwa kitu kizito kichwani hali iliyopelekea kifo chake.
Selemani James Mabula ni mwenye umri wa
Miaka 50 mkazi wa kata ya Busoka Manispaa ya Kahama Mkoani Shinyanga ameuwawa
na watu wasiojulikana kwa kupigwa na kitu kizito kichwani.
Jeshi la polisi Mkoa wa Shinyanga tayari
linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kuwabaini na kuwafikisha mahakani watuhumiwa
waliohusika.
Misalaba Media imezungumza na kamanda wa
jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi (SACP)
Janeth Magomi ambaye amesema tukio hilo limetokea majira ya saa saba kasorobo
usiku wa kuamkia Machi 12 Mwaka huu 2024.
Kamanda Magomi amefafanua kuwa, watu hao
walifika nyumbani kwa marehemu na kumtaka awapatie kile walichokuwa wakidai kuwa
ni fedha zao, na baadae walianza kumshambulia kwa kitu kizito kichwani hali
iliyosababisha kifo chake.
“Jeshi
la Polisi tunaendelea kuwafuatilia waliohusika katika tukio la mtu
anayejulikana kwa jina la Seleman James Mabula Mwenye Miaka 50 aliuawa kwa kupigwa
na kitu kizito kichwani karibu na Sikio la kulia na watu wasiojulikana”.
“Kilichotokea
ni kwamba majira ya saa sita na dakika 45 usiku marehemu huyo akiwa amelala
chumbani na mke wake walisikia Mbwa wanabweka nje Nyumba yao haina fensi lakini
wanazizi la Ng’ombe kwahiyo mwanaume huyu baada ya kusikia Mbwa wanakweka
akahisi kuna wezi wamekuja kuiba akatoka alipofungua tu mlango akakutana na
watu na maelezo haya ni kwa mujibu wa
mke wake, watu hao walikuwa wamevaa zile kofia za kuficha uso”. “Alichokisikia
mke wa marehemu alisikia sauti ya mmoja wa wale watu akimwambia tupe hela zetu
wakati huo walikuwa wameshaingia naye ndani chumbani wakiwa wanamwambia tupe
hela zetu mwanamke huyo alichokisikia marehemu aliuliza hela zipi mwamamke Yule
alichosikia walimpiga na kitu kizito kichwani akadondoka na wale watu
wakatokomea kusikojulikana’
“Marehemu
huyo pia alikuwa katika Baraza la kata la Ardhi kwahiyo sisi tunaendelea na
upelelezi ili tuweze kufahamu chanzo zaidi pengine tutaweza kufamamu
kilichokuwa kikiendelea na tuweze kuwakamata hao watuhumiwa”.amesema
SACP Magomi
SACP Magomi ametumia nafasi hiyo
kuendelea kuwataka wananchi kuacha tabia za kujichukulia sharia mkononi huku
akiwasisitiza watu wenye changamoto hizo kuziona mamlaka husika ikiwemo
Mahakama ili kupata haki zao.
“Wito
wangu ni kwamba kujichukulia sheria mkononi ni kosa na kwamba endapo
tutawabaini kwa kweli sheria itachukua mkondo wake lakini niwaombe wananchi wa
Mkoa wa Shinyanga ndani ya Halmashauri zote Kishapu, Msalala, Shinyanga
vijijini na Kahama, Shinyanga mjini na Ushetu tuache kujichukulia sharia mkononi
kwa sababu hata katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema kila mtu
anahaki ya kuishi lakini pia hakuna mtu ambaye yuko juu ya sheria kwamba wewe
utoe uhai wa mtu mwingine, hivi sasa wale wote ambao watajichukulia sharia mkononi
tutapambana nao kuhakikisha sheria inachukua mkondo wake”.
“Kwahiyo
niwaambie wananchi kama unachangamoto kama hii chombo cha Mahakama kipo na
bahati nzuri zimeboreshwa kweli kweli na haki tunaziona zinatendeka wewe kama
kweli unamdai mtu nenda Mahakamani fungua madai ili uweze kupata haki yako na
siyo kuchukua sheria mkononi kwenda kwa mtu kumuua”.amesema
SACP Magomi
Post a Comment