Ticker

6/recent/ticker-posts

BUGWETO FC YATINGA NUSU FAINALI SALOME MAKAMBA CUP

Timu ya Bugweto FC kutoka kata ya Ibadakuli imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali baada ya ushindi walioupata kupitia mikwaju ya penati katika michuano ya Salome Makamba Cup inayoendelea  kutimua vumbi hatua ya robo fainali .

Bugweto FC waliwakaribisha jirani zao timu ya Mwagala FC kutoka kata ya Kolandoto katika mchezo wa hatua ya pili (robo fainali) na kuibuka na ushindi kwa mikwaju ya Penati  6 – 5 baada ya kufungana goli 2- 2 ndani ya dakika 90.

Mwagala FC walitangulia kupata goli kipindi cha kwanza kupitia kwa Zabrone Ngassa  baadae Nkwano Deusi wa Bugweto FC alisawazisha goli hilo dakika za mapema kipindi cha pili kisha Renald wa timu ya Mwagala FC alipachika goli la pili ambapo baadae Frank Samweli aliisawazishia Bugweto FC na kumalizika kwa dakika 90 kwa sare ya goli 2 – 2.

Ushindi huo umewafanya Bugweto FC kutinga hatua ya nusu fainali katika michuano ya Salome Makamba Cup ambayo inafikia tamati siku ya jumamosi tarehe 1. 5.2024 kwa mchezo wa fainali utakaochezwa uwanja wa Sabasaba uliopo Kambarage na bingwa atakabidhiwa zawadi yake baada ya mchezo huo, kumbuka kuwa michuano hiyo inadhaminiwa na Mbunge wa viti maalumu Mkoa wa Shinyanga Mh. Salome Makamba.Wachezaji wa timu ya Mwagala FC wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo kuanza

Post a Comment

0 Comments