Ticker

6/recent/ticker-posts

CHANGAMOTO YA UKOSEFU WA MAJI KUENDELEA KATIKA BAADHI YA MAENEO MANISPAA YA SHINYANGA

TAARIFA
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) anawataarifu wateja na Wadau wote kuwa mawasiliano na wenzetu wa KASHWASA  yamefanyika na tayari matengenezo yamekamilika na hatua ya kwanza ni kujaza tanki kuu la Maji lililopo Mabale  katika wilaya ya Misungwi,
hivyo kwa Manispaa yetu    tutarajie huduma ya maji kuanza kuingia kwenye Tanki letu kuu la Old Shinyanga kesho asubuhi.

Mamlaka inaendelea kuzalisha huduma  ya majisafi  kupitia chanzo cha Maji toka bwawa la Ninghwa.
Maeneo yanayopata huduma kwa sasa ni Mwalugoye, Bushushu, kambarage,Mwasele ,
Lubaga pamoja na maeneo ya Butengwa.

Tunaomba radhi  kwa usumbufu uliojitokeza.
Taarifa imetolewa na kitengocha Mawasiliano na Mahusiano kwa Umma - SHUWASA


Post a Comment

0 Comments