Ticker

6/recent/ticker-posts

MHE. KATAMBI AKABIDHI MAGARI MATATU HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na watu wenye ulemavu Paschal Patrobas Katambi, amekabidhi Magari matatu kwa ajili ya kutolea huduma mbalimbali katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga- Mwawaza.

Magari hayo ni Gari la kubebea Wagonjwa (Ambulace) Gari la usimamizi shirikishi (Utawala) na Basi kwa ajili ya kuwachukua na kuwarudisha nyumbani watumishi.

Akikabidhi Magari hayo, Katambi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga mjini, ameahidi kushirikiana na Serikali kuendelea kuboresha miundombinu ya Afya katika mkoa wa Shinyanga, ikiwemo kuongeza gari la wagonjwa katika Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga pamoja na kukijenga kwa kiwango cha lami kipande cha barabara chenye kilomita 7, kinachoanzia eneo la Ndala kuelekea katika Hospitali hiyo, ili kuondoa adha kwa wananchi.

Ametumia nafasi hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa moyo wake wa kuwezesha miradi mingi katika mkoa wa Shinyanga, na hasa inayogusa maisha ya watu.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Wakili Julius Mtatiro, ameutaka uongozi wa Hospitali hiyo kuhakikisha unatunza vifaa tiba na magari yanayotolewa na Serikali kwa kushirikiana na wadau, huku Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko akisisitiza Magari yaliyokabidhiwa yatumike kwa malengo yaliyokusudiwa.

Awali, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt.Luzila John, aliishukuru Serikali na wadau kwa kuendelea kuiwezesha hospitali hiyo kupata vitendea kazi na amemuomba Mheshimiwa Katambi kuendelea kusaidia upatikanaji wa mahitaji mengine ikiwemo kuboresha miumbombinu ya barabara inayotokea Ndala kuelekea Hospitalini hapo.    

Muonekano wa Magari ambayo yamekabidhiwa na Mheshimiwa Katambi

Mheshimiwa Katambi akiwasili katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga

Mheshimiwa Katambi baada ya kupokelewa na Mganga mfawidhi wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. Luzila John (mwenye suti ya kijivu kushoto)

Mheshimiwa Katambi akisalimiana na wananchi waliohudhuria hafla ya kukabidhi Magari, mbele yake mwenye kofia ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko

Baadhi ya Madiwani kutoka Kata mbalimbali za Manispaa ya Shinyanga waliohudhuria Hafla hiyo wakimpokea Mheshimiwa Katambi

Madiwani wakiwa wamekaa

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga Dkt. Luzila John akitambulisha wageni

Utambulisho ukiendelea

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Anold Makombe akizungumza kwa niaba ya Chama cha Mapinduzi

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga Dkt. Luzila John akisoma Risala kwa Mgeni rasmi

Baadhi ya wananchi waliohudhuria hafla hiyo

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko akizungumza kwa niaba ya Manispaa

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Wakili Julius Mtatiro akizungumza kwa niaba ya Serikali

Hafla inaendelea

Mheshimiwa Katambi akizungumza muda mfupi kabla ya kukabidhi Magari

Mheshimiwa Katambi akimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Wakili Julius Mtatiro kwa kazi nzuri anazozifanya katika Wilaya ya Shinyanga

Katambi akiendelea kuzungumza

Mheshimiwa Katambi na msafara wake wakielekea kwenye eneo yalipo Magari kwa ajili ya zoezi la kukabidhi

Mheshimiwa Katambi akikata utepe ishara ya kukabidhi rasmi Magari hayo kwa uongozi wa Hospitali rufaa ya mkoa wa Shinyanga

Shangwe zikiendelea baada ya Mheshimiwa Katambi kukata utepe

Mheshimiwa Katambi akiteta jambo na baadhi ya viongozi

Mheshimiwa Katambi akiwasha Gari ishara ya kulizindua rasmi tayari kwa shughuli za Hospitali

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Wakili Julius Matatiro kwa kushirikiana na Mheshimiwa Katambi wakikata utepe kuzindua Gari la Wagonjwa

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko kwa kushirikiana na Mheshimiwa Katambi wakikata utepe kuzindua Gari la Utawala

Picha ya pamoja na uongozi wa Hospitali

Post a Comment

0 Comments