Ticker

6/recent/ticker-posts

MKURUGENZI MKUU WA TCRA DKT. JABIRI BAKARI ATOA MAELEKEZO KWENYE VYOMBO VYA HABARI, WAANDISHI WA HABARI NCHINI

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt Jabiri Bakari akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt Jabiri Bakari amewasisitiza waandishi wa habari na watoa huduma za utangazaji kuzingatia maadili,kanuni na sheria za kutoa huduma hiyo kwani  sekta hiyo ina mchango mkubwa    katika kujenga jamii bora na kuleta maendeleo ya jamii na Taifa.

Dkt. Bakari amesema hayo  Jumatano Mei 29,2024 katika warsha kwa waandishi wa habari wa mkoa wa Mwanza iliyoandaliwa na TCRA ili kuwajengea uwezo na kuwakumbusha kanuni za utangazaji na maudhui mtandaoni.

Dkt. Bakari  amesema lengo la TCRA ni kukuza ubunifu na kuwapa nafasi ya kuanzia vijana wasio na ajira rasmi hivyo watumie fursa ya mtandao katika kujenga jamii bora.

Aidha Dkt. Bakari amesema TCRA imeshaanza mchakato wa kuwatambua  watoa huduma za utangazaji, blogs na maudhui mtandaoni wanaofanya vizuri katika kufuata kanuni na ubunifu 

Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. Jabiri Bakari akitoa maelekezo kwa waandishi wa habari.

“Sisi tunaozalisha na kusambaza taarifa zinazoenda kwa watu walio wengi, wapokeaji taarifa wanatengenezwa kutegemeana na taarifa ambayo wameipokea,” amesema Dkt Bakari.

Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda Salum amesema Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inahimiza ushindani katika utoaji wa huduma bora ili kuchangia ustawi wa wananchi na maendeleo.

"TCRA itaendelea kushirikisha wadau katika kutatua changamoto katika ukuaji wa sekta ya utangazaji lakini pia tutaendelea kushirikiana na wadau kuhakikisha sekta ya Utangazaji inatoa mchango katika maendeleo ya nchi",amesema Mhandisi Imelda.

Meneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda akizungumza.

"Endapo namba ya simu, email unayotumia kuwasiliana na TCRA haipo, tafadhali weka taarifa ili iwe rahisi kwa mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kuwasiliana na watoa huduma, sisi hatuhitaji kumuacha mtu nyuma, tunataka kila mmoja wetu atumie mfumo wetu wa Tanzanite Portal. Tunataka tufanye mawasiliano kupitia mfumo huu".

"Uhalisia ni kwamba Teknolojia imebadilisha mambo mengi, hivyo Vyombo vya habari vinatakiwa kuwa wabunifu ili vipate Matangazo. Vipindi vyenye viashiria vya kuhamasisha Ushoga haviruhusiwi, tusiiachie mamlaka, ukiona kuna kipindi chenye viashiria vya ushoga kwenye chombo cha habari, toa taarifa TCRA", ameongeza Mhandisi Imelda.

Meneja huyo pia amesisitiza waandishi wa habari kujikita zaidi katika kuchakata na kusambaza maudhui ya ndani ili kujenga jamii imara. 
Kwa upande wao waandishi wa Habari wameishukuru Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania kwa warsha za mara kwa mara za kukumbushana kanuni za utangazajiMeneja wa TCRA Kanda ya Ziwa Mhandisi Imelda akizungumza katika warsha na waandishi wa habari jijini Mwanza.

Kikao cha Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na waandishi wa habari kikiendelea jijini Mwanza ambapo kimelenga  kuwakumbusha watoa huduma ya maudhui  mtandaoni kuzingatia kanuni na kujadili namna bora ya kuboresha urushaji wa maudhui mtandaoni pamoja na Kanuni za Utangazaji wa Uchaguzi kwa vya Siasa.


Post a Comment

0 Comments