Ticker

6/recent/ticker-posts

UGONJWA WA PUMU NA DAWA YAKE

Pumu ni ugonjwa unaoathiri sehemu ya kupitisha hewa kwenda kwenye mapafu ya binadamu yanazojulikana kitaalamu kama bronchioles.

Mtu mwenye pumu husababisha kuvimba kwa kuta za mirija, kujaa kwa ute mzito na kupungua kwa njia ya kupitishia hewa.

Hali hiyo humsababishia mwathirika kushindwa kuvuta na kutoa hewa nje, hivyo kupumua kwa shida.

 

Pia, hali hiyo inaweza kudumu kwa muda mfupi au mrefu kiasi cha kuhitaji tiba ili kumuwezesha mgonjwa kupata nafuu.

Mtu aliye na pumu, huwa nayo kipindi chote cha maisha yake.

Pumu husababisha na nini?

Kuna mambo kadhaa yanayoweza kusababisha kutokea kwa pumu, ikiwamo matatizo ya kinasaba.

Uvutaji wa sigara au tumbaku kipindi cha ujauzito pia unahusishwa na kusababisha pumu kwa mtoto atakayezaliwa.

Magonjwa ya mapafu kama bronchitis Vyanzo vya mzio (allergens) kama vumbi, kinyesi cha wanyama na baadhi ya vyakula.

Uchafuzi wa mazingira kama moshi na baadhi ya harufu kali.

Baadhi ya kemikali kwenye maeneo ya kazi hasa kwenye viwanda vya rangi, chuma, saruji na vigae.

Magonjwa kwenye mfumo wa kupumua yasabishwayo na baadhi ya virusi na bakteria kama pneumonia.

Tiba

Tiba mbadala inaweza kuondoa tatizo la pumu kwa mgonjwa.

Chukua magome ya mizizi ya mlimao kiasi (kama mkono mmoja), chemsha kwenye maji lita moja kisha maji yake tia tangawizi ilosagwa nusu kikombe na asali nusu lita, chemsha kunywa kikombe kimoja mara tatu.

Au:-

Chukua majani ya ngogwe na majani ya tura chemsha pamoja na kidonge kimoja cha halititi, kisha kunywa glasi moja kutwa mara tatu ikiwa vuguvugu, unaweza iunga na sukari ili ilete ladha nzuri

Mwandishi wa makala hii ni mtaalamu wa tiba mbadala

 

Post a Comment

0 Comments