Ticker

6/recent/ticker-posts

ASP KAIGWA AWATAKA WAENDESHA DALADALA ZA BASKELI MJINI SHINYANGA KUWEKA KENGERE NA TAA KWENYE BASKELI ZAO

Jeshi  la polisi kitengo cha usalama barabarani   Wilaya ya Shinyanga limesema limeendelea kuelimisha jamii kuhusu  umuhimu wa kuzingatia sheria, kanuni,na matumizi sahii ya alama za usalama barabarani ili kuzuia ajali.

 Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa polisi  kitengo cha usalama Barabarani wilaya ya shinyanaga  ASP Dezidery Kaigwa wakati akizungumza na Misalaba Media  ofisini kwake,  ilipotaka kujua hatua zinazochukuliwa  kwa waendesha baiskeli wanaokiuka sheria za usalama barabarani ikiwemo vyombo vyao kutokuwa na kengere na taa.

Kaigwa amesema kuwa jeshi hilo limekuwa likitoa elimu ya usalama barabarani  mara kwa mara kwa watumiaji wa vyombo vya moto,baiskeli pamoja na watembea kwa miguu na  kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wale wote wanaokiuka sheria ya usalama barabarani.

“Sisi tumejipanga na tunaendelea kutoa elimu kwa hawa watumiaji wa Baskeli kwahiyi tunawaelekeza kwamba lazima wazingatie sheria za usalama barabarani pindi wawapo barabarani hususan wakati wa usiku sambamba na hilo tunawataka kuhakikisha Baskeli zao zimefungwa taa kwa ajili ya kuonyesha mwanga wanapokuwa wanaendesha Baskeli zao usiku pamoja na kuwa na kengere na breki za Baskeli ili wasije wakasababisha ajali wanapokuwa barabarani”.

“Sheria iko wazi kwa wale ambao wanakiuka sheria basi sheria huchukua mkondo wake kwa kuwakamata na hili zoezi huwa linaendelea hasa nyakati za usiku kukamata Baskeli ambazo hazina breki, taa pamoja na refrekta kwahiyo niwatake wale watumiaji wa Baskeli waendelee kuzingatie sheria za usalama barabarani pia na watumiaji wengine wa vyombo vya moto na wao wachukulie kwamba hawa watumiaji wa Baskeli ni sehemu ya barabara kwahiyo wawapo barabarani wasiwe vyanzo vya kusababisha ajali, ili kuepuka ajali zisizotarajiwa basi watumiaji wote wa barabara wachukue tahadhari”.

“Nitoa wito kwa wale wanaotumia aina hii ya usafiri kwa wale ambao ni abiria ukikuta Baskeli haina refrekta haina breki au haina taa basi uchukue tahadhari ya kukataa kupanda hiyo Baskeli kwani kupanda Baskeli kunaweza kupelekea kwenda kupata ajali “.amesema ASP Kaigwa

Kauli ya ASP Kaigwa inafuatia  malalamiko ya  baadhi ya wanainchi  dhidi ya waendesha baiskeli zinazosafirisha abiria  maarufu daladala kutokuwa na kengere wala taa hali ambayo waliitaja inatishia usalama wa abiria wao na watembea kwa miguu.

Kwa upande wake  mwenyeketi wa  wilaya wa waendesha baiskeli za kubeba abiria  Bwana Mashaka Malugu  ameendelea kutumia nafasi yake kuwakumbusha umuhimu  wa kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuzuilika .

Uzingatiaji wa sheria za barabarani ni muhimu kwa watumiaji wote wa barabara wakiwemo madereva wa Magari, waendesha Pikipiki, Bajaji , Baiskeli pamoja na watembea kwa miguu ili kuzuia ajali zinazoweza kuzuilika .

TAZAMA VIDEO 

Post a Comment

0 Comments