Ticker

6/recent/ticker-posts

CHADEMA MKOA WA SHINYANGA KUFANYA MKUTANO WA HADHARA LEO

Na Mapuli Kitina Misalaba

Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mkoa wa Shinyanga kinatarajia kufanya Mkutano wa hadhara unaolenga kutoa elimu ya uraia  kwa wananchi ikiwa ni sehemu ya Maandalizi ya Uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika baadaye Mwaka huu Nchini kote

Mkutano huo unatarajiwa kufanyika leo Ijumaa Juni 14,2024 kuanzia saa tisa Alasili katika uwanja wa shule ya msingi Town karibu na viwanja vya Zimamoto Kambarage mjini Shinyanga.

Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Shinyanga Mhe. Emanuel Ntobi ametoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga na viunga vyake kuhudhuria katika Mkutano huo ambao ameutaja kuwa ni muhimu kwa kuwa wananchi watapata elimu ya uraia kuelekea mchakato wa kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura na maandalizi ya Uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mkutano huo wa hadhara umeandaliwa na CHADEMA Jimbo la Shinyanga mjini.

MKUTANO WA HADHARA HAUTAFANYIKA TENA KATIKA VIWANYA VYA ZIMAMOTO

MKUTANO WA HADHARA HAUTAFANYIKA TENA KATIKA VIWANYA VYA ZIMAMOTO

Post a Comment

0 Comments