Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha akiipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa kupata hati safi.
Na Mapuli Kitina
Misalaba
Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga Anamringi Macha ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa
kupata hati safi kutokana na kujibu hoja za mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za
serikali (CAG) kwa Mwaka wa fedha 2022\2023.
Ameyasema hayo leo Jumanne
Juni 25,2024 wakati akifunga kikao cha baraza maalum la madiwani wa Halmashauri
ya Manispaa ya Shinyanga lililojadili taarifa za utekelezaji wa majibu ya hoja
za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG.
RC Macha pamoja na
mambo mengine ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kupata hati safi kuhu akihimiza
kuendeleza ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.
“Kwanza
niwapongeza mstahiki meya pamoja na mkurugenzi kwa sababu mna tuzo tatu za siku
za hivi karibuni, kwanza kwa kupata tuzo ya kuwa Manispaa safi kwa Mwaka 2023 kuliko
Manispaa zote 19 za hapa nchini, lakini pia Manispaa hii ni kati ya Manispaa
zinazojitahidi kutoa taarifa kwa waandishi wa habari katika Halmashauri 184 hii
niya 18 Manispaa hii ni kati Manispaa bora kutoa taarifa kwa waandishi wa
habari katika shughuli zinazofanywa kwenye Manispaa hii lakini jambo la tatu ni
hili la kuwa miongoni mwa Halmashauri zilizopata hati safi kwahiyo haya mambo
matatu hahaji tu hivi hivi kuna watu wanashughulika kwahiyo mstahiki meya na
madiwani wake pamoja na mkurugenzi na watendaji wake wote niwapongezeni sana”.amesema
RC Macha
Pia Mhe. Macha ametumia
nafasi hiyo kuwataka watendaji wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kuendelea
kufanya kazi kwa bidii, juhudi na maarifa ili kuongeza tija na ufanisi.
Akiwasilisha taarifa ya
mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali kwa hesabu zilizokaguliwa katika
Mwaka unaoishia terehe 30 Juni, 2023 mkuu wa kitengo cha fedha na uhasibu
Manispaa ya Shinyanga Bwana Mulokozi Kishenyi ameitaja Halmashauri hiyo kupata hati safi 2023.
“Katika
hesabu zilizofungwa kwa kipindi cha kuishia tarehe 30, Juni 2023 Halmashauri ya
Manispaa ya Shinyanga ilipata hati safi ya ukaguzi aidha kutokana na ukaguzi
huo Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga ilikuwa na jumla ya hoja 43 ambazo
kati ya hoja hizo, hoja 13 zilikuwa za Miaka ya nyuma na hoja 30 zilikuwa za
Mwaka 2022\2023 Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga imeendelea kutekeleza hoja
zilizoibuliwa na hati safi ambapo hadi sasa jumla ya hoja 7 zimetekelezwa
kikamilifu na kufungwa na hoja 36 utekelezaji wake unaendelea”.amesema
Kishenyi
Kwa upande wake
mstahiki meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko amesisitiza kuongeza umakini na ushirikiano
katika utatuzi wa hoja zinazoibuliwa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za
serikali CAG ili kuepusha mkanganyiko.
Mwenyekiti wa Chama cha
Mapinduzi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Bwana Anord Makombe pamoja na mambo
mengine ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha madiwani kwenda kuhamasisha wananchi
kufanya maandalizi sahihi ya kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa
Mwaka huu 2024 pamoja na uchaguzi mkuu 2025.
Baraza
la madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga leo Jumanne Juni 25,2024 limefanya kikao maalum kujadili taarifa za utekelezaji
wa majibu ya hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Anamringi Macha akiipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa kupata hati safi.
Mkuu wa kitengo cha
fedha na uhasibu Manispaa ya Shinyanga Bwana Mulokozi Kishenyi akiwasilisha
taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali kwa hesabu
zilizokaguliwa katika Mwaka unaoishia terehe 30 Juni, 2023.
Mkuu wa kitengo cha
fedha na uhasibu Manispaa ya Shinyanga Bwana Mulokozi Kishenyi akiwasilisha
taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali kwa hesabu
zilizokaguliwa katika Mwaka unaoishia terehe 30 Juni, 2023.
Diwani wa kata ya
Kizumbi Mhe. Ruben Kitinya akitoa maoni yake kwenye kikao cha baraza maalum la
madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga lililojadili taarifa za utekelezaji
wa majibu ya hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG leo
Juni 25,2024.
Diwani wa kata ya Chibe Mhe. Kisandu John akitoa maoni yake kwenye kikao cha baraza maalum la madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga lililojadili taarifa za utekelezaji wa majibu ya hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG leo Juni 25,2024.
Diwani wa kata ya
Kitangili Mhe. Mariam Nyangaka akitoa maoni yake kwenye kikao cha baraza maalum la
madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga lililojadili taarifa za utekelezaji
wa majibu ya hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG leo
Juni 25,2024.
Mganga mkuu wa Manispaa
ya Shinyanga Dkt. Elisha Robert akishiriki kwenye kikao cha baraza maalum la
madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga lililojadili taarifa za utekelezaji
wa majibu ya hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali CAG leo
Juni 25,2024.
Mstahiki meya wa
Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko akizungumza kwenye kikao
cha baraza maalum la madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga lililojadili
taarifa za utekelezaji wa majibu ya hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu
za serikali CAG leo Juni 25,2024.
Mstahiki meya wa
Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias Ramadhan Masumbuko akizungumza kwenye kikao
cha baraza maalum la madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga lililojadili
taarifa za utekelezaji wa majibu ya hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu
za serikali CAG leo Juni 25,2024.