Ticker

6/recent/ticker-posts

JESHI LA POLISI MKOA WA SHINYANGA LAWAKAMATA WATATU WANAOTUHUMIWA NA MAUAJI KATIKA MANISPAA YA SHINYABNGA

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga limewakamata watuhumiwa watatu wanaohusishwa na mauji ya watu wawili waliouawa na kisha kuchomwa moto kwa tuhuma za wizi katika kata za Kitangili na Kizumbi Manispaa ya Shinyanga.

Taarifa hiyo imetolewa na kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa Shinyanga kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi (SACP) Janeth Magomi wakati akizungumza na Misalaba Media,  ambapo amesema kukamatwa kwa watuhumiwa hao ni mafanikio yanayotokana na msako na doria mbalimbali zinazofanywa na askari wa jeshi hilo.

Amesema jeshi hilo halitawafumbia macho wale wote wanaobainika kujichukulia sheria mkononi dhidi ya watuhumiwa wa matukio ya uhalifu kwani kwa kufanya hivyo ni kukiuka sheria za nchi.

Kamanda Magomi amewataka wananchi kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi kutoa taarifa za matukio ya wahalifu na uhalifu badala ya kujichukulia sheria mkononi.

“Hatutakubali matendo haya ya kikatili yaendelee ndani ya Mkoa wa Shinyanga kwahiyo jeshi la Polisi tumeingia katika oparesheni kali kabisa kuhakikisha kwamba tunawasaka wale wote ambao wamehusika katika matendo haya na kwa kuanzia sasahivi tunawatuhumiwa watatu mparoni kuhusiana na lile tukio la mwanzo ambalo lilitokea katika kijiji cha Iwelyangula na Bugayambelele kata za Kitangili na Kizumbi na hawa watuhumiwa ni wakazi wa Mkoa wa Shinyanga sisi tutawapeleleza mpaka pale ambalo tutahakikisha jarada lao tunalifikisha kwa wanasheria halafu tuweze kupisha makahama”.amesema SACP Magomi

“Sisi jeshi la Polisi bado tunaendelea kutoa elimu kwamba wananchi anayefanya kosa adhabu yake si kupigwa na kuuawa kisha kuchomwa moto na ndiyo maana tunaendelea kuwaelimisha kwamba vipo vyombo vya sheria mahakama zipo kwahiyo wananchi waendelee kushirikiana na jeshi la Polisi na sisi tunaendelea kutoa elimu katika kata zetu kuna wakaguzi wa kata kuna maaskari ambao wanashirikiana na viongozi wa vijiji, tarafa, mtaa, vitongoji na kata”. amesema SACP Magomi

Hata hivyo baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Shinyanga wameiomba serikali kuendelea kuchukulia hatua za kisheria dhidi ya watu wanaokutwa na tuhuma za uhalifu, badala ya kuwaachia huru hali inayochochea hasira kwa wananchi.

Wamesema kitendo cha wananchi kujichukulia sheria mkononi kimekuwa kikichochewa na hasira baada ya kuona watuhumiwa wa vitendo vya uhalifu ikiwemo wizi, unyang’anyi na ujambazi wakiwa mtaani baada ya kuachiwa huru.

Wameliomba jeshi la Polisi na mamlaka nyingine za kisheria kutoa adhabu kwa mujibu wa sheria zilizopo ili iwefundisho kwa watuhumiwa na watu wengine wenye tabia kama hizo na kukomesha uhalifu.

Wananchi hao wametaja sababu mbalimbali zinazochangia uhalifu kwa vijana kwamba ni hulka binafsi, hali ngumu ya maisha inayosababishwa na ukosefu wa ajira lakini pia kujihusisha kwenye makundi mabaya.

Misalaba Media pia imezungumza na kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga kamishna msaidizi mwandamizi wa Polisi Janeth Magomi ambaye ameendelea kuonya tabia ya wananchi kujichukulia sheria mkononi ambapo amesema kwa kufanya hivyo ni ukiukwaji wa sheria za nchi.

Post a Comment

0 Comments