Ticker

6/recent/ticker-posts

MAMIA YA WANANACHI WAJITOKEZA KATIKA TAMASHA LA UTAMADUNI WA MSUKUMA NHELEGANI MANISPAA YA SHINYANGA

Na Mapuli Kitina Misalaba

Tamasha la utamaduni wa Msukuma (SHINYANGA SUKUMA FESTIVAL SEASON 3, ambalo limeandaliwa na taasisi ya  BSL INVESTMENT COMPANY LIMITED AND THE TRUE LIVE FOUNDATION” limeanza leo na litahitimishwa kesho Jumapili Juni 30, 2024 katika viwanja vya shule ya msingi Nhelegani kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga.

Akizungumzia tamasha hilo Mkurugenzi wa  BSL INVESTMENT COMPANY LIMITED AND THE TRUE LIVE FOUNDATION Bwana Peter Frank (MR. BLACK) ameendelea kuwakaribisha wakazi wa Mkoa wa Shinyanga na Mikoa jirani ikiwemo Mkoa wa Mwanza, Simiyu, Tabora pamoja na Geita kujitokeza katika tamasha hilo.

MR. BLACK amesema kuwa malengo ya tamasha la utamaduni wa Kisukuma ni kutunza na kuenzi utamaduni wa Msukuma pamoja na kuendeleza umoja wa kabila hilo katika kushirikiana mambo mbalimbali yakiwemo ya kijamii kwa lengo la kukuza uchumi.

Katika tamasha hilo yamefanyika maonyesho ya Biashara, sanaa, ngoma za asili, burudani pamoja na Nyama choma” ambapo kauli mbiu ya tamasha la utamaduni wa Msukuma kwa Mwaka huu 2024 inasema “UTAMADUNI WETU URITHI WETU, SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA MAENDELEO YA TAIFA”

Viongozi na wananchi kutoka maeneo mbalimbali wamejitokeza kushiriki katika tamasha hilo kama sehemu ya kuunga mkono mwendelezo wa utamaduni wa kabila la Kisukuma “SHINYANGA SUKUMA FESTIVAL SEASON 3, LEJIGUKULU LYA NZENGO”.

Misalaba Media imezungumza na baadhi ya wananchi ambapo wamempongeza  Mkurugenzi wa  BSL INVESTMENT COMPANY LIMITED AND THE TRUE LIVE FOUNDATION Bwana Peter Frank (MR. BLACK) kwa kuandaa tamasha hili ambapo wameomba kuwa endelevu.

Wameeleza kuwa katika tamasha hili wamejifunza mambo mbalimbali ikiwemo kuendelea kuenzi mila na desturi za kabila la Kisukuma ikiwemo chakula mavazi, mavazi ya heshima pamoja na kilimo.

Naibu katibu mkuu wizara ya utamaduni, sanaa na michezo Dkt. Suleiman Serera anatarajiwa kuwa mgeni rasmi siku ya kufunga tamasha la utamaduni wa Msukuma kesho Jumapili Juni 30,2024.

 TAZAMA PICHA  HAPA CHINI

 


 

Post a Comment

0 Comments