MWILI WA ALIYEKUWA DEREVA WA KATIBU TAWALA MKOA WA KILIMANJARO WAAGWA LEO


WANANCHI mkoa wa Kilimanjaro  wamejitokeza katika kuuaga mwili  aliyekuwa Dereva  wa Katibu Tawala mkoa Kilimanjaro Dk.Tixson Nzunda, Alphonce Edson (54)nyumbani kwake  katika kijiji cha majengo mampya,  kata ya Kahe wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro.




Watu hao walipa ajali  June 18 mwaka huu katika eneo la njiapanda ya uwanja wa Mataifa (KIA) wakieleka  kumpokea makamu  wa rais Dk Philip Mpango  aliyekuwa akienda jijini Arusha kwa majukumu ya kikazi.



Akitoa salama za Rambirambi, mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu  alisema  wao kama mkoa wamepata pigo kubwa na itawachukua muda kukaa sawa kutokana na  uhitaji wa watu hao katika ofsi hiyo.



Alisema  marehemu Alphonce alikuwa  mtulivu, mchapakazi  na hajawai kuwa na ugomvi wala hana manunguniko wakati wote hata anapongwa kazi za ziada bila malipo.



"Hapana duniani tunapita, hakuna haja ya kuwa wababe. Watumishi wa ofsi yangu igeni mfano wa  Alphonce,  marehemu aliwai kuniendesha, ameendesha  familia yangu,  sijawai kusikia analalamika, huwezi kujua ni wakati gani amekasirika au amefurahi kupitiliza, hakika alikuwa ni mtu wa ajabu sana hapa tunajambo la kujifunza, "alisema RC Babu 


Alisema kuwa, kifo chake ni pigo kubwa kwa ofisi ya mkuu wa mkoa  alikuwa ni Dereva mwenye busara na hekima katika kazi


Aidha Mkuu huyo wa mkoa alitumia pia msiba huo kuwasihi wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro kuendeleza mshikamano uliopo na kuacha kuiga mambo ya watu wengine kwani hayaweza kuwasaidia.



Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro, Patrick Boisafi alisema kuwa yapo mambo ambayo tunapaswa kujifunza kupitia kifo cha Alphonce kuwa wema na waaminifu katika majukumu ya kila siku. 


Alisema kuwa, kazi ya Mungu haina makosa na kuwataka kila mmoja kujiandaa maana hakuna ajuaye siku yake ya mwisho itakuwaje. 


"Yapo mambo mema yaliyofanywa na Rais Dk Samia Suluhu Hassan kupitia misiba hii ambapo chama kinamshuku kwa jinsi alivyojitoa kupia misaba hii,"


Aidha amewataka viongozi kuhakikisha wanapambana kuhakikisha barabara ya kuelekea Mabogini Kahe Chekereni inakarabatiwa ili kupitika wakati wote ambapo jambo hilo litakuwa ni la kumuenzi marehemu Alphonce Edson. 


Adha , Mkuu wa wilaya ya Moshi, Zephania Sumaye alitoa pole kwa familia kwa kuondokewa na mmoja wa familia ambaye alikuwa nguzo muhimu. 


Alisema kuwa, hapa dunia hakuna kinachotokea ambacho hakijaruhusiwa na Mwenyezi Mungu na kuwataka familia kuendelea kufarijika kwa kutumia maneno ya biblia.


Alisema serikali itaendelea kushirikiana na familia pale pote watakapohitaji msaada kutoka kwa Serikali ya wilaya. 



Akitoa salama kwa niaba ya Chama cha madereva wa Serikali Tanzania, Venus Ngalu alisema wamepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha Alphonce Edson akiwa katika majukumu yake na aliyekuwa Katibu Tawala mkoa wa Kilimanjaro. 



Naye Mwakilishi wa Madereva wa Makatibu Tawala mikoa, Dereva wa Katibu Tawala mkoa wa Tabora,Kennedy Nangawe  alisema kuwa Marehemu alikuwa akionyesha ushirikiano mkubwa katika Chama chao ambapo ni pigo kubwa kwa chama.


Akitoa mahubiri  mchungaji   wa kanisq la kiinjili kilteri (KKKT) Usharika  wa  Lowiri Mchungaji Thibias Msweka  aliwataka waamini  kujitadhimini   mambo wanayofanya  hasa katika maeneo wanayoishi hasa kwa wahitaji ili yawe alama  pale wanapoondoka.




"Leo tujitafakari mimi na wewe tukiondoka utakumbukwa kwa lipi? Watumishi, angalieni msije mkakumbukwa kwa kuwa mzigo kwenye ofsi za watu.Leo watu wengi wanaishi  kwa kiburi,majigambo na kunyanyua mabega.


Dunia ya sasa hakuna huruma na badala yake ni ukatili katika jamii, hatuwaonei huruma hadi kuamini kuwa wanapopata viungo vya binadamu wanapata utajiri.. huo ni uongo na naomba niwahakikishie    utajiri hauji bila kufanya kazi."alisema  Mchungaji


Aidha alimuomba mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro  kuhakikisha kusimamia   watu wenye ulemavu(Albino) huku akisisitiza kuwa  watu hao wanawindwa sana.


Marehemu  ameacha mjane na   watoto sita na wajukuu wawili.







Mkuu  wa mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu  akitoa salama za mwisho


Previous Post Next Post