Na Moshi Ndugulile
Serikali imepongeza utekelezaji wa Mradi wa USAID kizazi hodari kanda ya kaskazini Mashariki unaotekelezwa na kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania K.K.K.T Makao makuu, kuendelea kufanya kwa weledi,tija na ufanisi katika juhudi za kukabiliana na maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi
Akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali Mjini Shinyanga kando ya Mkutano wa wadau wanaotekeleza mradi huo Mkuu wa idara ya afya ,lishe,na ustawi wa jamii,ofisi ya Rais TAMISEMI,Bwana Rashid Kitambulilo,ambaye pia ni Mchumi amesema mradi huo kwa kushirikiana na serikali umesaidia kuyabaini makundi au jamii ya pembezoni hivyo kuwezesha kuingizwa kwenye vipaumbele vya mipango ya afya katika halmashauri husika (complesive hearth plan na concern social worker planning)
Amesema hali hiyo imewawezesha walengwa hao ambao ni watoto wanaoishi na virusi vya ukimwi wenye umri wa Miaka 0-17 kupata huduma na matunzo na tiba.
“Tunashirikiana na Kanisa la K.K.K.T kuhakikisha kwamba shughuli ambazo zimepangwa kufanyika zinafanikiwa na ushiriki wetu mkubwa upo katika eneo la usimamizi ambapo tunahakikisha kwambwa wale walengwa wanapata zile huduma zilizokusudiwa lakini eneo lingine tunashirikiana katika kuzipitia taarifa za utekelezaji wa mradi huu, tukiangalia moja ya mafanikio ni kwamba hizi jamii ambazo zilikuwa zimesahaulika kwa sasa hivi tumeweza kuzibaini kupitia mradi wa USAID Kizazi Hodari unaofadhiliwa na shirika la maendeleo ya kimataifa la marekani USAID kupitia mfuko wa Rais PEPFA, na tunashukuru walengwa wanaendelea kunufaika”.amesema Kitambulio
Mratibu wa kudhibiti Ukimwi TACAIDS Mkoa wa Geita Dkt Yohane Fulgence Kyaga amesema Mradi huo wa USAID kizazi hodari kanda ya kaskazini Mashariki umeendelea kusaidia kufikia malengo ya serikali ambayo ni ifikapo Mwaka wa 2030 tunatarajia kutokuwa na maambukizi mapya yatokanayo na virusi vya UKIMWI
“Mradi huu hasa unasaidia kuwafikia watoto ambao kimsingi ni changamoto kubwa kwa hapa Tazania ambapo takwimu zinaonyesha kuwa Mwaka 2022 Watoto Milioni 13,laki Saba walipoteza mzazi moja au wote wawili kutokana na maambukizi ya virusi vya ukimwi,lakini pia watoto 1030, walibainika kuwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi wenye umri wa Miaka 0-14 ambapo ni asilimia 57% tu wapo kwenye dawa za kufubaza virusi vya ukimwi,wakati malengo ya Dunia na Tanzania ni kuhakikisha zaidi ya Asilimia 95% wanapaswa kuwa kwenye huduma ya dawa za kufubaza ukimwi, lakini pia watoto 84 walipoteza maisha kutokana na janga la virusi vya ukimwi.
Mradi huu kwa ujuma unatusaidia sisi serikali kufikia malengo ya kufikia zile 95 tatu (95% ya watoto wanajua maambukizi yao,95% wanaanishiwa dawa za kufubaza virusi vya ukimwi,na 95% nyingine watoto waweze kufubaza virusi vya ukimwi.
Kwa hiyo mradi huu unaisaidia serikali kuwatambua watoto wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi,mradi huu umeweza kuwakatia bima za afya watoto na familia zao,kuwapatia vifaa mbalimbali vya elimu ambavyo vinasaidia kuondoa chngamoto za mtoto hivyo kumwezesha kuwa mfuasi mzuri wa dawa za kufubaza virusi vya ukimwi lakini pia kuhudhuria masomo kawaida.
Leo tumekutana na kujadili kuhusu takwimu mbalimbali za mradi,tumeweza kushirikishana uzoefu na mbinu mbadala ambazo zitasaidia katika utekelezaji wa huu mradi,lakini pia tupo kwenye majadiliano kuangalia namna bora ya kuwa na mikakati endelevu ya kuhakikisha miradi inaendelea baada ya mfadhili kuondoka” ameeleza Dkt Kyaga
Akizungumzia kuhusu Mradi huo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Zabron Masatu ambaye ameshiriki katika Mkutano huo unaojumuisha wadau wa Mikoa inayotekeleza mradi huo,amesema wameendelea kushirikiana na USAID kizazi hodari kanda ya kaskazini Mashariki kuhakikisha wanakuwa na mipango ya pamoja katika utoaji wa huduma za tiba na matunzo kwa watoto hao wanaoishi na virusi vya ukimwi,ambapo serikali imekuwa ikiainisha vipaumbele huku watekelezaji wa mradi wakitoa fedha
“Tumekuwa tukifanya ziara za usimamizi za pamoja kutembelea familia zilizopo kwenye mazingira magumu,lakini tumekuwa tukitoa vifaa mbalimbali kwa ajili ya kusaidia watoto waliopo kwenye mazingira magumu,lakini pia watoto waliopo kwenye mazingira magumu wameweza kutambuliwa ambapo baadhi ya familia zimepatiwa ufadhili wa kadi za bima ya afya yaani ICHF,abazozimekuwa zikiwasaidia kupata matibabu,kuanzia watoto hadi familia nzima kwa ujumla
Lakini vilevile katika kufanya mipango shirikishi sisi serikali kwa sababu tunatambua vipaumbele vinavyohitajika kwa wananchi wetu tumehakikisha kwamba watoto ambao waliokuwa hawajatambuliwa au walikuwa hawapati matibabu toshelevu kwa sasa wamerudishwa kwenye vituo vya kutolea huduma za dawa kwa ajili ya matunzo kwenye eneo la VVU na UKIMWI
Hii imesaidia kuboresha afya za watoto na familia zao,hali inayowawezesha kuendelea na shughuli za kijamii ikiwemo kuhudhuria masomo ambayo ni haki msingi kwao,wamepatiwa tiba na matunzo vizuri hali iliyosaidia CD4 zao kuongezeka, na kuziwezesha familia zao kuendelea na shughuli za uzalishaji ikilinganishwa na awali ambapo walikuwa wakitumia muda wao kushughulikia afya za watoto wao, kupitia mradi huu pia vimeundwa vikundi vya kujikwamua kiuchumi,ambavyo vimesaidia kuongeza kipato cha familia.
Hayo ni mafanikio makubwa kwa serikali kupitia mradi huo,kwani kwa kuwatumia maafisa wetu kwenye halmashauri mbalimbali tumeendelea kushirikiana na mradi huu kuhakikisha tunawapata walengwa,ameeleza” Dkt Masatu
Naye mratibu wa Mikoa na Halmashauri kutoka tume ya kuthibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Bi Amina Masoud amepongeza kwa mradi huo kuendelea kuwatambua na kuwawezesha kupata huduma zinazistahili waathirika wa virusi vya UKIMWI ambapo ameshauri mradi huo wa ‘USAID Kizazi Hodari’ kuwa endelevu ili kuzuia maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi.
Mratibu huyo amesema serikali kupitia tume ya kudhibiti ukimwi Tanzania TACAIDS inatambua na kuthamini mchango wa wadau wa maendeleo katika juhudi za mapambano dhidi ya maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi.
Mkurugenzi mshiriki matokeo ya Asasi zinazotekeleza mradi wa USAID kizazi hodari kanda ya kaskazini Mashariki Bwana Aminiel Allen Mongi,ametaja mafanikio yaliyofikiwa katika utoaji wa huduma kipindi cha nusu ya Mwaka kwamba mradi umefanikiwa kufikia malengo katika utoaji wa huduma za Afya ambapo walengwa 157,974 wamefikiwa ambayo ni asilimia 105% wakati idadi iliyokuwa imetarajiwa katika nusu ya Mwaka ni kuwafikia walengwa 157,110
ikiwa ni pamoja na kuwafikia walengwa 62,162 kwenye shughuli za kiuchumi zaidi ya lengo lililokuwa limekusudiwa la kuwafikia walengwa 59,162
Bwana Mongi ameeleza kuwa mafanikio hayo ni matokeo mazuri ya utekelezaji wa mradi huo katika kipindi cha nusu Mwaka 2023/2024 Machi ambapo umefanyika kwa kiwango kizuri zaidi
“matokeo ya ushirikiano mzuri baina ya serikali na watekelezaji hao kwenye ngazi mbalimbali kuanzia ngazi ya Wizara zinazoshirikiana moja kwa moja na mradi huo, ikiwemo ofisi ya Rais TAMISEMI,wizara ya maendeleo ya jamii,jinsia,wanawake na makundi maalumu,TACAIDS,Wizara ya Elimu,lakini kwenye ngazi ya Mikoa na Wilaya tumekuwa na ushirikiano mzuri zaidi na wenzetu wa kamati za afya lakini pia kwenye ngazi za kata tunao wasimamizi wa mashauri ya watoto kama FHI na wadau wengine” ameeleza Mkurugenzi huyo
Ameyataja malengo ya mradi huo kuwa ni kuboresha Afya,ustawi na ulinzi wa watoto walio katika mazingira hatarishi na vijana kuanzia umri wa Miaka 0 hadi 17 ili kufikia malengo ya kidunia ya kupambana na virusi vya ukimwi
“kwa maana ya 95, 95, 95 (wenye maambukizi waweze kujua hali zao,waliofahamu kuwa wana maambukizi waweze kuunganishwa na vituo vya tiba na matunzo kwa ajili ya kuanzishiwa dawa,na walioanzishiwa dawa waweze kuhudhuria kwenye vituo vya tiba na matunzo ili kufubaza maambukizi)”
Ameyataja makundi yanayofikiwa na katika mradi huo kuwa ni pamoja watoto wanaoishi na maambuki ya virusi vya ukimwi,kaya zinazosimamiwa na watoto,lakini kuna watoto wa wanawake wanaoishi katika mazingira hatarishi,watoto waliookolewa kwenye matukio ya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia
“Tunatoa huduma mbalimbali baada ya kuwatambua na kuwaunganisha na vituo vya kutoa huduma wanaweza tunaongeza afua mbalimbali ambazo zinazuia na maeneo makuu tunayoyalenga katika utoaji wa huduma ni pamoja na kutoa bima za afya kwa walengwa ili waweze kupata matibabu wanapopata changamoto za kiafya,haki ya elimu na afya ya uzazi, huduma ya Elimu ambapo tunahakikisha wamesaidiwa ili wahudhurie masomo,ambapo tunawasaidia vifaa vya elimu ili wahudhurie masomo kwa uhakika,elimu ya biashara na fedha kuweka na kukopa,kuwapa vifaa anzilishi vya biashara ili waweze kuanzisha biashara ndogondogo, lakini pia kuna Nyanja ya ulinzi na usalama kuhakikisha tunawalinda dhidi ya matukio ya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia”amesema Mongi
Wadau wanaotekeleza Mradi wa mradi wa USAID kizazi hodari kanda ya kaskazini Mashariki kutoka Mikoa minne ya Singida,Mwanza,Geita na Mara wamekutana Mjini Shinyanga kutathimini mafanikio,changamoto na matarajio katika nusu ya Mwaka wa fedha 2023/2024
Kanisa la kiinjili la kilutheri Tanzania K.K.K.T Makao Makuu linatekeleza mradi wa USAID kizazi hodari kanda ya kaskazini Mashariki katika Mikoa tisa ya Tanzania Bara ambayo ni Mwanza,Mara,Geita,Singida,
MWISHO
Mratibu wa kudhibiti UKIMWI Mkoa wa Shinyanga akizungumza leo Juni 27,2024.
Mratibu wa Mikoa na Halmashauri kutoka tume ya kuthibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Amina Masood akizungumza leo Juni 27,2024.
Mkutano wa wadau wanaoshiriki katika utekelezaji wa mradi huo wakiwemo wawakilishi kutoka ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia wanawake na makundu maalum, TACAIDS, kamati ya usimamizi wa Afya ngazi ya Mikoa na Halmashauri, wadau wanaosimamia afua za tiba na mafunzo katika Mikoa husika ukiendelea leo Alhamis Juni 27,2024.
Mkutano wa wadau wanaoshiriki katika utekelezaji wa mradi huo wakiwemo wawakilishi kutoka ofisi ya Rais TAMISEMI, Wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia wanawake na makundu maalum, TACAIDS, kamati ya usimamizi wa Afya ngazi ya Mikoa na Halmashauri, wadau wanaosimamia afua za tiba na mafunzo katika Mikoa husika ukiendelea leo Alhamis Juni 27,2024.
Post a Comment