Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Makusanya amewataka
waumini wa dini ya kiislamu
Mkoani Shinyanga na watanzania wote
kushiriki katika zoezi la uchaguzi
wa serikari za mitaa linalotalajiwa kufanyika baadaye Mwaka huu nchini
kote .
Akiongoza swala ya Iddi El Adha
katika uwanja wa sabasaba mjini Shinyanga Sheikh
Makusanya amewaomba waumini wa dini ya kiislamu na jamii nzima kushiriki
kikamilifu katika uchaguzi wa serikari
za mitaa utakaofanyika mwaka huu ili
kutimia haki yao ya msingi ya kuchagua
na kuchaguliwa.
Pia ametoa wito
kwa waumini wa dini ya kiislamu kuwa chachu
ya kulinda na kudumisha amani
iliyopo.
“Mwaka
huu serikali yate pendwa, serikali yetu tukufu inafanya uchaguzi wa serikali za
mitaa kwahiyo ndugu zangu waislamu nakuombeni ushiriki sana katika chaguzi hizi
tena tushiriki kwa ukamilifu wale ambao watakuwa wanatarajia kuomba nyazifa
mbalimbali za uongozi katika mitaa yetu wakiona
fursa na vigezo wanavyo waombe lakini pia kwa wale ambao hawaombi nafasi yoyote
usiache kushiriki katika jambo hili la uchaguzi katika mitaa yetu”.
“Mungu
akijalia katika Mwaka ujao 2025 tutakuwa na uchaguzi mkuu kwahiyo nakuombeni waislamu
tushiriki, tushiriki kwa amani na utulivu na sisi waislamu kila mtu anahiali ya
kuwa katika chama chochote kilichoandikishwa kwa mujibu wa sheria kila mtu
anahaki ya kuchagua chama ambacho yeye kinamridhia kwahiyo vyama vyetu
visitufanye sisi tukavunja amani na utulivu kila mmoja anahaki ya kufanya
uchaguzi kwa amani na utulivu kwahiyo nakuombeni mshiriki katika zoezi”.amesema
Sheikh Makusanya
Katika mawaidha
yake wakati wa swala ya Iddi El Adha Sheikh
wa Wilaya ya Shinyanaga Soud Kategile amewaasa waislamu
kuendelea kuwa wazalendo na kudumisha amani iliyopo sanjari na kulinda
maadili ya Taifa la Tanzania
“Shukurani
si kusema asante shukurani haiishii kusema Alhamdulillah peke yake lakini
tumshukuru mwenyezi Mungu kwa kutujalia amani katika nchi yetu na tuilinde
amani hii kwa sababu ni tunu kwetu ambayo wengi wanaitamani katika nchi za
wenzetu bila ya amani sisi tusingekuwepo hapa amani haina dini, amani haina
kiongozi amani haina mtawaliwa kwahiyo tumshukuru mwenyezi Mungu kwa kutujalia
amani, ndugu zangu waislamu kila mmoja aondoke na jambo hili la kutunza amani
katika nchi yetu”.amesema Sheikh Kategile
Wakiongea na Misalaba
Media baadhi ya waumini wa dini ya
kiislamu wemesema watazingatia
mafundisho waliyopatiwa na viongozi wa dini
kupitia mawaidha kwenye ibada ya Eid El Adha ikiwemo kushiriki
kikamilifu uchaguzi wa serikali za mitaa baadaye mwaka huu.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Makusanya akiongoza
swala ya Iddi El Adha katika uwanja wa sabasaba Kambarage mjini
Shinyanga leo Jumatatu Juni 17,2024.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Makusanya akiongoza swala ya Iddi El Adha katika uwanja wa sabasaba Kambarage mjini Shinyanga leo Jumatatu Juni 17,2024.
Sheikh wa Mkoa wa Shinyanga Ismail Makusanya akiongoza
swala ya Iddi El Adha katika uwanja wa sabasaba Kambarage mjini
Shinyanga leo Jumatatu Juni 17,2024.
Sheikh wa Wilaya ya Shinyanaga Soud Kategile akisoma mawaidha yake wakati wa swala ya Iddi El Adha katika uwanja wa Sabasaba Kambarage mjini Shinyanga leo Jumatatu Juni 17,2024.
Waumini wa dini ya kiislamu
Waumini wakiwa katika swala la Idd El Adha leo mjini Shinyanga.
Waumini.
Post a Comment