Ticker

6/recent/ticker-posts

UTOVU WA NIDHAMU WATAJWA JONATHAN MADETE KUMUONDOA KWENYE NAFASI YA UENYEKITI WA UVCCM WILAYA YA SHINYANGA MJINI

Katibu wa Siasa, itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Mkoa wa Shinyanga Bwana Richard Masele akitoa taarifa kwa waandishi wa habari.

Na Mapuli Kitina Misalaba

Halmashauri kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga imemuachisha nafasi ya uongozi Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM) wilaya ya Shinyanga Mjini Bwana Jonathan Agustino Madete kwa madai ya utovu wa nidhamu.

Taarifa hiyo imetolewa kwa waandishi wa habari na katibu wa Siasa, itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Mkoa wa Shinyanga Bwana Richard Masele, ambaye amesema maamuzi hayo yametolewa katika kikao cha Halmashauri kuu ya CCM Mkoa wa Shinyanga.

“Kikao cha Halmashauri kuu ya CCM Mkoa wa Shinyanga chini ya Mwenyekiti wake Ndugu Mabala Mlolwa, kilichoketi mnamo tarehe 13,06.2024, pamoja na mambo mengine kimemuachisha nafasi ya uongozi ndugu Jonathani Agustino Madete Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Shinyanga Mjini kwa sababu ya utovu wa nidhamu,”amesema Masele.

“Vilevile Halmashauri kuu ya CCM Mkoa wa Shinyanga imeazimia kuwa, kwamwe haitamfumbia Macho wala kumvumilia Mtu yeyote awe kiongozi au Mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM, atakayevunja kanuni,taratibu na Katiba ya Chama chetu,  hatua za kinidhamu zitachukuliwa mara moja”.

“Hiini pamoja na kulinda heshima ya Chama chetu na Jumuiya zake na kuhakikisha misingi ya Chama hiki na miongozo inaendelea kuheshimiwa chini ya Mwenyekiti wetu mahiri, mchapa kazi na mzalendo wa kweli Mhe. Samia Suluhu Hassan na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”.amesema Masele

Katibu wa Siasa, itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Mkoa wa Shinyanga Bwana Richard Masele akitoa taarifa ya kuvuliwa uongozi Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Shinyanga mjini Bwana Jonathan Madete.



 

TAZAMA VIDEO HII.

Post a Comment

0 Comments