NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI,SANAA NA MICHEZO HAMIS MWINJUMA (MWANA FA), AMPONGEZA PATROBAS KATAMBI KWA KUIBUA VIPAJI VYA VIJANA KUPITIA MICHEZO

Na Mwandishi wetu, Misalaba Media

Naibu Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma (Mwana FA), amempongeza Mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini Mhe. Paschal Patrobas Katambi kwa kuibua vipaji vya vijana kupitia ligi aliyoiandaa kwa kuwa mpira ni ajira.

Mwijuma ametoa pongezi hizo wakati akizindua Rasmi Ligi ya Dr. Samia/ Katambi Cup ambayo imelenga kuibua vipaji vya vijana,na itashirikisha timu 32 za mpira wa miguu katika Mkoa wa Shinyanga.

Ligi hiyo imezinduliwa katika viwanja vya Jasco vilivyopo Ngokolo, na kucheza michezo mbalimbali ikiwamo ya kuvuta kamba,kukimbiza kuku,kuchoma nyama ambapo washindi waliibuka na zawadi, na timu hizo 32 za mpira wa miguu zitatimua vumbi katika viwanja mbalimbali.

Naibu Waziri huyo Mhe. Mwijuma  amewaomba wananchi wa Shinyanga kwamba wasije jaribu kumpoteza mbunge huyo bali wanapaswa kumlinda na kumpigania kwa nguvu zote ili aendelee kuwa mbunge wao na kuwaletea maendeleo.

“Rais wetu Mheshimiwa Dr. Samia Suluhu Hassan anapenda michezo hivyo Katambi kuanzisha ligi hii ni kumuunga Mkono Rais katika kukuza michezo hapa nchini na kutoa ajira kwa vijana,”amesema Mwinjuma.

“Katambi ni Mbunge ambaye anachapa kazi, ni mtu mwenye maarifa makubwa sana, hata Rais Samia ana mwamini katika kumsaidia kazi na kuwatumikia Watanzania wote,hivyo anapaswa kulindwa na kupiganiwa Wabunge kama hawa wapo wachache msije kumpoteza,”ameongeza.

Zawadi ambazo watapewa washindi kwenye ligi hiyo, mshindi wa kwanza wa mpira wa miguu, anapewa kiasi cha Shilingi milioni 6 pamoja na kombe, mpira na jezi, mshindi wa pili atapewa Shilingi milioni 3, kombe,mpira na jezi, huku mshindi wa tatu atapewa Sh.milioni moja,mpira na jezi.

Zawadi zingine  mfungaj bora atapewa Shilingi  Elfu 50, mchezaji mwenye nidhamu Shilingi laki moja, na washindi wa kucheza “Dansi”mshindi wa kwanza atapewa Shilingi milioni Moja, wapili Laki 5 na watatu Laki 3, na kueleza kwamba zawadi ambazo ametoa mbunge huyo ni fedha nyingi na anawapenda wananchi wake.

 

Previous Post Next Post