Ticker

6/recent/ticker-posts

BABA WA MAREHEMU AOMBA POLISI KUCHUNGUZA MAUAJI YA MWANAWE CHARLES KASHINJE, POLISI SHINYANGA WAKIRI UCHUNGUZI UNAENDELEA

Na Mapuli Kitina Misalaba

Kastory Kashinje Shija, Baba mzazi wa marehemu Charles Kashinje, ameliomba Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini waliohusika na mauaji ya mtoto wake.

Charles Kastory Kashinje, mwenye umri wa miaka 24 na mkazi wa kijiji cha Idodoma, kata ya Samuye, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, alikutwa akiwa ameuawa kwa kukatwa sehemu mbalimbali za mwili wake kando ya barabara usiku wa kuamkia Jumatatu, Septemba 9, 2024.

Misalaba Media imezungumza na Baba wa marehemu, Kastory Kashinje Shija, ambaye ameliomba Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini waliohusika na mauaji hayo na kwamba amesema marehemu alikuwa mtoto wake wa mwisho kati ya watoto kumi na ameacha watoto wawili wa kike.

“Mimi nalipongeza jeshi la polisi walikuja tukashirikiana nao, mimi nawategemea wafanye mbinu zote hao watu waliofanya hivo wajulikane, wapatikane hilo tu nataka wajulikane maana sina lakufanya kabisa mtoto wangu amechinjwa kama kuku tena likuwa namtegemea alikuwa mtu mzuri sana hao watu labda alikuwa anawadai inawezekana walikuwa wenyeji wake ndiyo maana wakafanya hivo wakaona tusimbakize tumchinje kabisa yaani familia yangu alikuwa anahudumia kila kitu nilikuwa namtegemea sana, mimi ninawatoto kumi (10) huyo Charles alikuwa ni mtoto wangu wa mwisho ameacha watoto wawili wote wa kike”.amesema Baba mzazi  

Kaimu Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Kennedy Mgani, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa uchunguzi bado unaendelea.

"Ni kweli tukio lilitokea, lakini mpaka sasa hakuna mtu aliyekamatwa maana ufuatiliaji bado unaendelea, uchunguzi unaendelea bado hatuna update zaidi watiliwa mashaka na wengine kwahiyo bado uchunguzi unaendelea" amesema ACP Mgani.

Misalaba Media itaendelea kufuatilia tukio hilo na kutoa taarifa zaidi.

Post a Comment

0 Comments