Ticker

6/recent/ticker-posts

BREAKING: MWANDISHI WA HABARI AFARIKI KWA AJALI YA GARI

 


Mwandishi wa habari Mkongwe nchini  Michael Sikapundwa   ambae amawahi kuandikia Magazeti mbali mbali makubwa nchini kutoka mkoa wa Morogoro amefariki Dunia kwa ajali ya gari.

Mwandishi huyo amefariki usiku wa kuamkia leo kwa ajali iliyotokea eneo  la  Tungi Morogoro  na gari Hilo alikuwa akiendesha mwenyewe na hakuna na mtu mwingine.

Mwili wake umehifadhiwa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Tunaomba mwenye mawasiliano yeyote na familia yake aujulishe Uongozi wa Morogoro Press Club, Polisi Moro, ama waweza Wasiliana na mwandishi  Idda  Mushi 0754296927.

Jitihada za kumtafuta kamanda wa polisi wa mkoa wa Morogoro zinaendelea ili kujua chanzo hasa Cha ajali hii na taarifa zaidi .

CHANZO - MATUKIO DAIMA MEDIA

Post a Comment

0 Comments