Ticker

6/recent/ticker-posts

MBOWE NA TUNDU LISSU WATIWA NGUVUNI ,JESHI LA POLISI LATHIBITISHA










Polisi nchini Tanzania imewakamata watu kumi na wanne (14) wakiwemo viongozi wa chama hicho Freeman Mbowe, Tundu Lissu na Godbless lema.


Kwa mujibu wa taarifa ya polisi viongozi hao wamekamatwa wakiwa wanahamasisha kufanyika kwa maandamano ambayo hayana kibali.


"Taarifa rasmi tunazozitoa nikuwa watu hawa tunawashikilia na sio kuwa wametekwa kama taarifa zinazozagaa, huko mtaani ulinzi umeendelea kuhamasishwa ili kuilinda amani tulionayo," ameeleza Mkuu wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar Es Salaam, Jumanne Muliro.


Polisi wanaendelea kusisitiza kuwa hakuna kibali cha kufanya maandamano hivyo wataendelea kuwakamata wote wanaohamasisha maandano hayo.


Aidha polisi hawajaweka wazi ni lini watuhumiwa hao watapelekwa mahakamani.


Soma zaidi:

Post a Comment

0 Comments