Ticker

6/recent/ticker-posts

SHINYANGA: MWANAMKE AFARIKI KWA KUMEZA VIDONGE VYA SUMU, INASADIKIWA KUWA VYA PANYA

Na Mapuli Kitina Misalaba

Mwanamke mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 75, mkazi wa kijiji cha Masengwa, Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, amefariki dunia ndani ya chumba chake baada ya kudaiwa kumeza vidonge vinavyosadikika kuwa vya sumu ya panya.

 Tukio hili limetokea mnamo Septemba 22, 2024, majira ya asubuhi.

Misalaba Media imezungumza na mwenyekiti wa kijiji cha Masengwa Bwana Zachalia Ntemi Sanane, ambaye alielezea jinsi alivyopokea taarifa ya tukio hilo.

Sanane alieleza kuwa baada ya kufika kwenye familia hiyo, alimjulisha mtendaji wa kijiji, ambaye naye alimuarifu mtendaji wa kata ili kuwaita polisi.

Polisi walifika eneo hilo saa kumi na moja jioni wakiwa na daktari wao. Baada ya kuchukua maelezo kutoka kwa familia na kukagua masalia ya vidonge, waliwaruhusu waendelee na taratibu za mazishi.

“Nilitoka kanisani muda wa mchana badae nikapigiwa simu kwamba sogea hapa kwenye familia ya Suzana Jinya Ganai kweli nilienda kufika pale nikamkuta mama yule tayaru mauni yamemkuta”.

“Baada ya kufika katika familia hiyo nilimpigia mtendaji wangu wa kijiji  nikamwambia na yeye akasema ampigie mtendaji wa kata ili awapigie polisi wakati wanakuja mimi nilianza kuchukua maelezo kwenye familia wakasema mama huyo hakuwa na ugomvi na mtu yoyote maana anaishi yeye, mama yake mzazi, watoto na wajukuu wake ambapo asubuhi siku ya Jumapili watoto wote aliwaambiwa waende kanisani baada ya watoto hao kwenda kanisani kumbe yeye alikuwa amepanga sasa kufanya maamuzi hayo inasemekana alikunywa dawa ya panya alimeza vidonge viwili kimoja alikitapika walikikuta chini”.

“Badae polisi walikuna muda wa saa kumi na moja walikuwa na daktari wao wakapinga na wao walichukua maelezo kwa familia walienda kuangalia alipotapika wakaona masalia ya vidonge badae wakaturuhusu kuendelea na taratibu za mazishi”.amesema Sanane

Mazishi ya Suzana Jinya yamefanyika leo saa nane mchana katika kijiji cha Masengwa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Misalaba Media inaendelea kumtafuta kaimu kamanda wa polisi Mkoa wa Shinyanga kwa taarifa zaidi kuhusu upelelezi wa tukio hilo.

Post a Comment

0 Comments