MHESHIMIWA SAMBALA AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUMWAGA FEDHA KWENYE KATA YA MONDO

Na Sheila Katikula, Dodoma

Diwani wa Kata ya Mondo na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chemba iliyopo mkoani  Dodoma Mheshimiwa ,Said Sambala amemshukuru  Rais  Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia Kata  hiyo fedha nyingi za  miradi ya maendeleo hususan katika   ujenzi wa miundombinu ya huduma za jamii katika kata hiyo. 

Hayo ameyasema juzi kwenye mahafali ya  mahafali ya 27 ya Shule ya Sekondari ya Mondo iliyoko Kata ya Mondo  Wilaya ya Chemba mkoa wa mkoni Dodoma.

Mheshimiwa Sambala amesema Rais Dk Samia Suluhu Hassan ametoa zaidi ya Sh Bilioni Moja na Milioni Miatatu kwenye Kata yetu ya Mondo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya huduma za jamii ikiwemo elimu na  vile vile  ametuongezea Sh Milioni Mia Moja kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Waida tunajukumu la kuunga mkono juhudi hizi za Rais.

Ameitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na sekta ya afya, elimu, maji  hivyo amewataka  wananchi wa Kata hiyo  kuunga mkono juhudi za Rais  kwa kutunza miradi hiyo ili waweze kutumia kwa muda mrefu. 

 Hata hivyo amewataka wazazi kuwapatia watoto wao  mahitaji  ya msingi ili waweze kwenda shule kwa wakati sanjali na kuwapatia  chakula.  
 

Hata hivyo katika kutatua changamoto zinazoikabili shule hiyo ikiwemo ya  utoro Mheshimiwa Sambala  amemshauri Mwenyekiti wa Bodi ya Shule hiyo, Thomas Chorray kuitisha kikao cha haraka ili waweze kujadili  changamoto hiyo na  kuipatia ufumbuzi ili wanafunzi hao waweze kutimiza ndoto zao za baadaye. 

 "Nadhani kuna haja ya Bodi ya Shule tukutane haraka kuzipatia  ufumbuzi changamoto za shule hii ikiwemo changamoto sugu ya  utoro.  

Sambala amesema utoro tafsiri yake ni moja tu kwamba mahala fulani jamii yetu  hatuko sawa kauli hii ameitoa kufuatia takwimu za wahitimu wa mwaka huu  kuonesha karibu nusu ya wanafunzi 103 kati yao wavulana 36 na wasichana 67 wameshindwa kuhitimu kwa sababu ya utoro ikilinganishwa na wanafunzi 112  kati yao wavulana 54 na wasichana 68 waliohitimu leo.

Katika hatua nyingine Mheshimiwa Sambala  amewataka wahitimu wa miaka ya nyuma waliomaliza kwenye shile hiyo kuungana katika kutatua changamoto za shule hiyo.

 "Mimi ni  mmoja wa wahitimu wa shule hii pamoja na wenzangu  Mkuu wa Shule Msaidizi  na Mjumbe mmoja wa Bodi ya Shule ninawaomba kutumia fursa hii watu wote tuliosoma hapa   kuunganisha nguvu zetu  na  kuanzisha utaratibu maalumu wa kurudisha fadhila kwa shule yetu  kufanya hivi 
 tutapunguza changamoto zinazoikabili shule yetu"

Vile vile Mheshimiwa Sambala  ametumia fursa hiyo kuwahimiza wananchi wa Kata hiyo kwa ujumla kujitokeza kwenye zoezi la kujiandikisha kwenye daftari la wakazi ili kupata sifa ya kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika   Novemba 27 mwaka huu.

 "Ninawaomba wananchi kwa ujumla tuhimizane kujiandikisha kwenye daftari  la wakazi ili tupate sifa ya kushiriki  uchaguzi unataraji kufanyika Novemba 27 mwaka huu",amesema Mheshimiwa Sambala.

Mahafali hayo yamekutanisha watu mbalimbali akiwemo   Profesa Fadhil Hamza Mgumia kutoka Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini aliyemwakilisha Mkuu wa Chuo Profesa Hozen Mayaya.

Previous Post Next Post