Ticker

6/recent/ticker-posts

DC CHIKOKA APITA MTAA KWA MTAA KUHAMASISHA WANANCHI KUJITOKEZA KUJIANDIKISHA DAFTARI LA MKAZI 2024.



Na Gabon Mariba, Mara.

Mkuu wa Wilaya ya musoma Mhe.Juma Chikoka leo oct 15 amefanya ziara fupi ya kutembea mtaa kwa mtaa kwaajili ya kuhamasisha wananchi wa musoma na wafanya Biashara kujitokeza kwa wingi kwaajili ya kujiandikisha katika Daftari la mkazi ili kuweza kupiga kura na kuchagua viongozi ndani ya mitaa yao.

Akizungumza na wafanya biashara mbali mbali wa musoma mjini  mhe chikoka amewataka Wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwenye daftari la mkazi ili waweze kupiga kura na kuwachagua viongozi wenye kuwaletea maendeleo katika maeneo yao.

Aidha ameweza kuwapa elimu baadhi ya wananchi kutokana na imani yao ya kua walikwisha jiandikisha na kupewa vitambulisho.
"Uandikishaji huu ni tofauti na ule uliopita wa vitambulisho, kwani vitambulisho vitatumika kupiga kura kumchagua Diwani,mbunge na Rais. Hivyo ni vema kujiandikisha kwenye daftari la mkazi ili kuchagua viongozi ngazi za chini hasa viongozi wa Serikali za mitaa nk." Amesema Chikoka.

Pia amewataka wananchi kujitokeza mapema kujiandikisha na kuendelea na majukumu mengine ya kibiashara kwani wafanyabiashara wengi wamekua wakizungumzia swala la kupungukiwa muda wa kwenda kujiandikisha, kwani wanachelewa kutoka  kwenye biashara zao.




























Hjhjjjjjjj


Post a Comment

0 Comments