Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga mjini Fue Mrindoko, akizungumza kwenye hitimisho la maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM ambapo jumuiya hiyo imehitimisha leo Januari 31, 2025 katika shule ya sekondari Mwangulumbi kata ya Chibe.
Na Mapuli Kitina Misalaba
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga mjini Fue Mrindoko, amewataka wanafunzi
kuzingatia elimu na kuepuka kurubuniwa katika vitendo vinavyoweza kuharibu
maisha yao huku akisisitiza jukumu la wazazi kuwalea na kuwatunza watoto wao
ili kuwakinga dhidi ya vitendo vya uhalifu na maadili mabovu.
"Ninawaombeni
sana wanafunzi mzingatie elimu, msirudi nyuma. Sisi wazazi ni jukumu letu kuwalea
na kuwahudumia watoto hawa. Tusipowalea, watakuwa vibaka na kushiriki michezo
michafu. Tukiwalea vizuri, tutawaepusha na ukatili. Wanafunzi, msimame imara na
msikubali kuchezewa, maana maisha yenu yataharibika,"
amesema Mrindoko.
Mwenyekiti huyo amesisitiza umuhimu wa utunzaji wa
mazingira, hasa katika shule, akiwataka wanafunzi na wazazi kuendelea kushiriki
katika upandaji wa miti kwa ajili ya maendeleo endelevu.
Mwenyekiti huyo amewahimiza wanajumuiya ya wazazi
kuendelea kushirikiana ili kuimarisha jumuiya hiyo, hasa katika nyanja za afya,
elimu na mazingira.
Kwa upande wake, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga Mjini, Bi. Doris Yotham Kibabi, ameeleza shughuli
mbalimbali zilizotekelezwa katika maadhimisho ya miaka 48 ya CCM.
"Tumeadhimisha
sherehe hizi katika kata zote 17 kwa kufanya shughuli mbalimbali kama vile
upandaji miti shuleni na vituo vya afya, utoaji wa vifaa vya elimu kwa
wanafunzi, na kuchangia chakula mashuleni. Pia, tumefanikisha upimaji wa damu
salama," amesema Bi. Doris.
Katika maadhimisho hayo, jumuiya hiyo imefanikiwa
kupanda miche 891 ya miti, kugawa daftari zaidi ya 60, kalamu zaidi ya 50, kilo
225 za unga wa mahindi, mfuko wa sukari wa kilo 25, na debe sita za mahindi
ambapo Shule zilizopokea msaada huo ni pamoja na Shule ya Msingi Msufini,
Kitangili, Town, na Sekondari ya Mwasele.
Katika sherehe hizo, wanafunzi wa Shule ya Sekondari
Mwangulumbi, iliyopo Kata ya Chibe Manispaa ya Shinyanga, wamebainisha
changamoto wanazokabiliana nazo, ikiwemo uhaba wa matundu ya vyoo, ukosefu wa
umeme, na ukosefu wa mabweni kwa wanafunzi wa kike.
Kaka mkuu na dada mkuu wa shule hiyo wamesema
ukosefu wa umeme unatatiza masomo ya vitendo katika maabara, huku upungufu wa
matundu ya vyoo ukisababisha msongamano mkubwa na kuhatarisha afya za
wanafunzi.
Akijibu changamoto hizo, Diwani wa Kata ya Chibe,
Kisandu John, ameeleza kuwa tayari shilingi milioni 44 zimetengwa kwa ajili ya
ujenzi wa matundu ya vyoo, huku akiahidi kuwa suala la umeme litapewa
kipaumbele ndani ya mwezi mmoja.
Shule ya Sekondari Mwangulumbi ina jumla ya
wanafunzi 523 na inakabiliwa na upungufu wa matundu 15 ya vyoo.
Katika sherehe hizo, jumuiya hiyo imempongeza Rais
Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake za kuleta maendeleo, ikiwemo ujenzi wa
shule na hospitali na kwamba jumuiya hiyo imetangaza kuunga mkono maamuzi ya
Mkutano Mkuu wa CCM ya kumpitisha Rais Samia kama mgombea wa urais kwa uchaguzi
mkuu ujao.
"Tunaendelea
kumuunga mkono Rais Samia na tunawahimiza wananchi wa Shinyanga kuhakikisha wanachagua
madiwani, mbunge, na Rais kutoka CCM ili maendeleo yaendelee,"
amesema Bi. Doris.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga mjini Fue Mrindoko, akiongoza zoezi la
upandaji miti katika shule ya sekondari Mwangulumbi kata ya Chibe.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga mjini Fue Mrindoko, akiongoza zoezi la
upandaji miti katika shule ya sekondari Mwangulumbi kata ya Chibe.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Bi. Doris Yotham Kibabi, akipanda mti katika shule ya sekondari
Mwangulumbi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Bi. Doris Yotham Kibabi, akipanda mti katika shule ya sekondari
Mwangulumbi ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga mjini Fue Mrindoko na Katibu wa Jumuiya ya
Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Bi. Doris Yotham Kibabi, wakiwasili
ukumbini.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga mjini Fue Mrindoko na Katibu wa Jumuiya ya
Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Bi. Doris Yotham Kibabi.
Katibu wa Jumuiya ya
Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Bi. Doris Yotham Kibabi akizungumza kwenye sherehe ya maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM na kwamba jumuiya hiyo imehitimisha leo katika shule ya sekondari Mwangulumbi kata ya Chibe.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Bi. Doris Yotham Kibabi akizungumza kwenye sherehe ya maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM na kwamba jumuiya hiyo imehitimisha leo katika shule ya sekondari Mwangulumbi kata ya Chibe.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Bi. Doris Yotham Kibabi akizungumza kwenye sherehe ya maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM na kwamba jumuiya hiyo imehitimisha leo katika shule ya sekondari Mwangulumbi kata ya Chibe.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga mjini Fue Mrindoko, akizungumza kwenye
hitimisho la maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM ambapo jumuiya hiyo imehitimisha
leo Januari 31, 2025 katika shule ya sekondari Mwangulumbi kata ya Chibe.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga mjini Fue Mrindoko, akizungumza kwenye
hitimisho la maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM ambapo jumuiya hiyo imehitimisha
leo Januari 31, 2025 katika shule ya sekondari Mwangulumbi kata ya Chibe.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga mjini Fue Mrindoko, akizungumza kwenye
hitimisho la maadhimisho ya Miaka 48 ya CCM ambapo jumuiya hiyo imehitimisha
leo Januari 31, 2025 katika shule ya sekondari Mwangulumbi kata ya Chibe.