Na Mapuli Kitina Misalaba
Diwani wa
Kata ya Ndala ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Zamda
Shaban, ametangaza kuwa mnada mpya wa vitu mbalimbali, ikiwemo nguo, mboga
mboga na biashara ndogondogo, utafanyika rasmi kuanzia Jumatano ijayo.
Ameyasema hayo kwenye mkutano wake wa hadhara
Februari 26, 2025 ameeleza kuwa mnada huo utakuwa unafanyika kila Jumatano
kuanzia asubuhi, ambapo amewakaribisha wafanyabiashara na wajasiriamali
kupeleka bidhaa zao na kuwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi.
Akizungumza na wananchi wa kata hiyo, Mhe. Zamda
amesema kuwa uamuzi wa kuanzisha mnada huo umetokana na juhudi zake kwa
kushirikiana na viongozi wengine wa kata katika kutafuta njia za kukuza uchumi
wa eneo hilo, hasa baada ya kuona kwamba soko la Ndala limekuwepo kwa zaidi ya
miaka 21 bila kuwa na maendeleo makubwa.
"Tumekaa
kama viongozi tukafikiria, soko letu la Ndala limekuwepo kwa muda mrefu lakini
halijapata ufumbuzi wa kudumu. Kwa sasa tumejipanga kuhakikisha linakuwa sehemu
ya kukuza uchumi wa wakazi wa Ndala," amesema Mhe.
Zamda.
Ameeleza kuwa baada ya kufuatilia suala hilo,
alilipendekeza kwa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga na kupata kibali kutoka
kwa Mstahiki Meya na Mkurugenzi wa Manispaa kuendelea na taratibu za kuanzisha
mnada.
"Katika
eneo letu la Soko la Ndala kumekuwa na changamoto nyingi. Wafanyabiashara
walikuwa wanashindwa kukaa kwa muda mrefu, lakini sasa tumepata suluhisho. Eneo
letu la chama cha mapinduzi pia tumeliomba na sasa linaenda kuwa sehemu ya
mnada huu mpya. Mnada huu utafanyika Jumatano kwa kuwa hakuna mnada mwingine
siku hiyo," amesema Zamda
Amefafanua kuwa mnada huo utakuwa fursa muhimu kwa
wafanyabiashara wa bidhaa mbalimbali kama mitumba, matunda, na huduma za
chakula.
"Mitumba
ya grid one itakuwa sehemu ya mnada huu, naomba wanandala tuwape nafasi
wafanyabiashara wa mnada waje ili kuinua uchumi wa kata yetu. Wananchi kutoka
kata nyingine jirani pia wanakaribishwa kushiriki,"
amesema Zamda.
Baadhi ya wananchi wa Kata ya Ndala wameeleza
kufurahishwa na hatua hiyo, wakisema kuwa mnada huo utachochea ukuaji wa uchumi
wa mtu mmoja mmoja, kata na Manispaa ya Shinyanga kwa ujumla.
Pia wamesema kuwa mnada huo utafungua fursa za ajira
kwa vijana na wanawake wajasiriamali.
Mkutano huo wa hadhara umewakutanisha wananchi na
viongozi wa taasisi mbalimbali kama SHUWASA, TANESCO, Idara ya Ardhi na TARURA
ambapo wananchi wamepata nafasi ya kuuliza maswali kuhusu changamoto
zinazowakabili, ambapo wataalamu wa taasisi husika wamejibu na kutoa ufafanuzi.
Diwani huyo ametolea ufafanuzi kuhusu maoni ya
wananchi juu ya changamoto za miundombinu ya barabara na huduma za afya
akieleza kuwa serikali inaendelea kushughulikia masuala hayo, huku akiwataka
wananchi kuwa wavumilivu wakati suluhisho la kudumu likitafutwa.
Mkazi wa kata ya Ndala akitoa maoni yake kwenye
mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Mhe. Zamda Shaban.
Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye
mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Mhe. Zamda Shaban.
Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Mhe. Zamda Shaban.
Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Mhe. Zamda Shaban.
Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Mhe. Zamda Shaban.
Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Mhe. Zamda Shaban.
Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Mhe. Zamda Shaban.
Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Mhe. Zamda Shaban.
Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Mhe. Zamda Shaban.
Mkazi wa kata ya Ndala akiuliza maswali kwenye mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo Mhe. Zamda Shaban.
Post a Comment