Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)
Wilaya ya Shinyanga Mjini imeanza ziara rasmi ya kutembelea kata zote 17 za
jimbo la Shinyanga Mjini ambapo leo imetembelea kata ya Mwamalili na kata ya
Old Shinyanga ndani ya Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Mzee Fue Mrindoko,
amesisitiza umuhimu wa malezi bora kwa watoto na kuonya dhidi ya mmomonyoko wa
maadili katika jamii.
Ametoa wito kwa wazazi kuhakikisha wanalea watoto
wao kwa maadili mema ili kuwaepusha na vitendo visivyofaa kama vile wizi,
ukahaba, na utumiaji wa madawa ya kulevya.
Aidha, Mrindoko amekemea vikali ukatili dhidi ya
wanawake na watoto, akiwataka wanaume wanaojihusisha na vitendo vya ubakaji na
ulawiti kwa imani za kishirikina kuacha mara moja tabia hizo huku akisisitiza
kuwa serikali itaendelea kuchukua hatua kali kwa wote watakaobainika
kujihusisha na vitendo hivyo.
Mwenyekiti huyo pia amekemea ushoga kwa wanaume na
kuwataka wanawake wanaouza miili yao kwa tamaa ya pesa kuachana na tabia hiyo
ambapo ameeleza kuwa vitendo hivyo ni dhambi kwa Mwenyezi Mungu na vinakiuka
maadili ya taifa la Tanzania.
Katika ziara hiyo, Mrindoko ametumia nafasi hiyo
kuwahakikishia wananchi kuwa changamoto zinazowakabili, hususan tatizo la
upatikanaji wa umeme na maji katika kata ya Mwamalili, zitashughulikiwa kwa
usimamizi wa CCM na serikali ya awamu ya sita.
Kwa upande wake, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM
Wilaya ya Shinyanga Mjini, Doris Yotham Kibabi, amewahimiza wanachama wa
jumuiya hiyo kuongeza wanachama wapya.
Amesisitiza pia umuhimu wa kulipa ada za uanachama
kwa wakati ili wanachama waendelee kuwa hai ndani ya CCM.
Jumuiya hiyo imeendelea kumshukuru Rais Samia Suluhu
Hassan kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika Wilaya ya
Shinyanga Mjini.
Viongozi wa jumuiya hiyo wameendelea kuahidi kumuunga
mkono katika hatua zote za maendeleo na kuhakikisha anashinda kwa kishindo
katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mhandisi James Jumbe, ameeleza imani yake kuwa
CCM itashinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 huku akitoa wito
kwa wanachama na viongozi wa chama kuendelea kudumisha mshikamano ili
kuhakikisha ushindi wa CCM.
Akizungumza katika ziara hiyo, Mhandisi Jumbe
amesema kuwa Rais Samia ameonyesha uongozi thabiti na mafanikio makubwa katika
sekta muhimu kama vile miundombinu, elimu, afya, na utoaji wa mikopo kwa
makundi maalum.
"Rais
Samia ni mtu wa maendeleo, ameboresha miundombinu ya barabara ambayo inasaidia
kwa kiasi kikubwa uchumi wa nchi yetu," amesema
Mhandisi Jumbe.
Amesema Rais Samia amefanya juhudi kubwa katika
sekta ya afya kwa kuhakikisha upatikanaji wa vifaa tiba, ujenzi wa hospitali,
vituo vya afya, na zahanati. Vilevile, ameboresha sekta ya elimu kwa kuongeza
mikopo ya wanafunzi wa vyuo vikuu na kuajiri walimu kwa wingi.
Mhandisi Jumbe amewahimiza wanachama wa CCM
kushirikiana kwa nguvu, kujenga chama, na kumuunga mkono Rais Samia pamoja na
viongozi wa chama ili kuhakikisha ushindi katika uchaguzi wa mwaka 2025.
"Tushirikiane
kwa nguvu, tuendelee kujenga chama, tuunge mkono Rais wetu na viongozi wa
chama, na tupate ushindi mkubwa," amesema Jumbe.
Mjumbe huyo wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya
Shinyanga Mjini pia ameeleza kuwa utendaji wa Rais Samia katika utekelezaji wa
Ilani ya CCM umekuwa wa kiwango cha juu huku akitaja kuwa ndiyo sababu wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM
walimpendekeza kwa kauli moja kuwa mgombea pekee wa urais kupitia chama hicho
katika uchaguzi mkuu wa 2025.
"Mheshimiwa
Rais Samia anatekeleza majukumu yake kwa weledi mkubwa, ndiyo maana wajumbe wa
mkutano mkuu wa CCM walipitisha azimio la kumpitisha kuwa mgombea pekee wa
Urais kupitia CCM," amesema Jumbe.
Pia amempongeza Dkt. Emmanuel Nchimbi kwa kuteuliwa
kuwa mgombea mwenza, akisema kuwa ni mtu mwenye heshima, mchapakazi, na
mstahimilivu.
"Kwa
hiyo ukiangalia muunganiko wa Dkt. Samia na Dkt. Nchimbi, hakuna mashaka kwamba
uchaguzi mkuu wa mwaka huu, tunaenda kushinda kwa kishindo,"
ameongeza Jumbe.
Baadhi ya wanachama wa Jumuiya hiyo wamepongeza
ziara hiyo na kuahidi kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali na CCM ambapo
wamesema kuwa ziara kama hizo zinawapa fursa ya kuelewa mipango ya maendeleo na
kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wake.
Wajumbe wengine wa kamati ya utekelezaji Jumuiya ya
Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga ambao wameshiriki kwenye ziara ya leo ni pamoja
na Daniel Kapaya, Marry Makamba na Zulfa Hassan.
Ziara ya Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini inaendelea kesho kwa kutembelea kata nyingine ndani ya jimbo hilo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko akizungumza kwenye katika kata ya Mwamalili ikiwa ni sehemu ya ziara ya jumuiya hiyo leo Februari 18, 2025.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Doris Yotham Kibabi, akihimiza wanachama wa jumuiya hiyo kuongeza
wanachama wapya.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mhandisi James Jumbe, akizungumza kwenye ziara
hiyo leo Februari 18, 2025.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Doris Yotham Kibabi, akihimiza wanachama wa jumuiya hiyo kuongeza
wanachama wapya katika kata ya Mwamalili leo Februari 18, 2025.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Doris Yotham Kibabi, akihimiza wanachama wa jumuiya hiyo kuongeza wanachama wapya katika kata ya Mwamalili leo Februari 18, 2025.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, Doris Yotham Kibabi, akihimiza wanachama wa jumuiya hiyo kuongeza wanachama wapya katika kata ya Mwamalili leo Februari 18, 2025.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko akizungumza kwenye
katika kata ya Mwamalili ikiwa ni sehemu ya ziara ya jumuiya hiyo leo Februari
18, 2025.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko akizungumza kwenye
katika kata ya Mwamalili ikiwa ni sehemu ya ziara ya jumuiya hiyo leo Februari
18, 2025.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko akizungumza kwenye
katika kata ya Mwamalili ikiwa ni sehemu ya ziara ya jumuiya hiyo leo Februari
18, 2025.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Doris Yotham Kibabi, akihimiza wanachama wa jumuiya hiyo kuongeza
wanachama wapya katika kata ya Old Shinyanga.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Doris Yotham Kibabi, akihimiza wanachama wa jumuiya hiyo kuongeza
wanachama wapya.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mhandisi James Jumbe, akizungumza kwenye ziara
hiyo leo Februari 18, 2025 katika kata ya Old Shinyanga.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Mhandisi James Jumbe, akizungumza kwenye ziara
hiyo leo Februari 18, 2025.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko akizungumza kwenye
katika kata ya Old Shinyanga ikiwa ni sehemu ya ziara ya jumuiya hiyo leo Februari
18, 2025.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko akizungumza kwenye katika kata ya Old Shinyanga ikiwa ni sehemu ya ziara ya jumuiya hiyo leo Februari 18, 2025.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Fue Mrindoko akizungumza kwenye katika kata ya Old Shinyanga ikiwa ni sehemu ya ziara ya jumuiya hiyo leo Februari 18, 2025.
Post a Comment