Na Mapuli Kitina Misalaba
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini Mzee Fue Mrindiko, amewahimiza wazazi
na walezi kushiriki kikamilifu katika zoezi la uchangiaji wa chakula shuleni
kwa ajili ya watoto wao ili kuimarisha afya zao na kuongeza ufaulu.
Mrindiko ametoa wito huo wakati wa ziara ya jumuiya
hiyo inayoendelea katika kata zote 17 za Jimbo la Shinyanga Mjini, ambapo leo
Februari 19, 2025, wamefanya ziara katika Kata ya Kizumbi na Kitangili.
Mrindoko amesisitiza umuhimu wa wazazi kuhakikisha
wanachangia chakula shuleni ili wanafunzi waweze kusoma kwa utulivu bila
changamoto za njaa.
Aidha, ametumia nafasi hiyo kulaani vikali vitendo
vya ukatili dhidi ya watoto, hasa ulawiti na ubakaji, akisisitiza kuwa serikali
itaendelea kuwachukulia hatua kali wahusika wa matukio hayo.
Katika ziara hiyo, Diwani wa Kata ya Kizumbi, Reuben
Kitinya, ameishukuru Serikali kwa kutoa shilingi milioni 603 kwa ajili ya
ujenzi wa shule mpya ya sekondari, akisema itasaidia kupunguza umbali wa kilomita
12 ambao wanafunzi walikuwa wakitembea hadi Shule ya Sekondari Kizumbi.
Ameeleza kuwa shule hiyo mpya, Sekondari ya
Igalukilo, inatarajiwa kuanza kupokea wanafunzi Machi 2025 kutoka shule za
msingi Mwamashele, Lyandu, na Bugayambele.
Kwa mujibu wa Msimamizi wa Ujenzi wa Shule ya
Sekondari Igalukilo, Maliki Yazidi Nofel, ujenzi wa shule hiyo ulianza Septemba
1, 2024, na ulipaswa kukamilika Desemba 30, 2024, lakini umekumbwa na
changamoto za mkandarasi.
Amebainisha kuwa madarasa mapya yako tayari kutumika,
huku maabara tatu, maktaba, na jengo la kompyuta vikiwa katika hatua za mwisho
za ujenzi.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya
Shinyanga Mjini, Fue Mrindiko, amepongeza jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita
chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha sekta ya elimu na
maendeleo kwa ujumla.
"Ninawapongeza
sana kwa ushirikiano wenu mzuri. Mmesimamia vyema ujenzi huu. Hii inaonesha
namna gani Serikali ya Awamu ya Sita imedhamiria kuboresha sekta ya
elimu," amesema Mrindiko.
Hata hivyo, amesisitiza kuwa ujenzi wa vyoo unapaswa
kukamilika haraka ili wanafunzi 102 waliopangiwa kuanza masomo wasikumbwe na
changamoto za miundombinu duni.
Aidha, amewataka wanachama wa CCM na wananchi kwa
ujumla kumuunga mkono Rais Samia na mgombea mwenza wake Dkt. Emmanuel Nchimbi
katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, akisisitiza kuwa chama hicho kiko imara na
tayari kwa ushindani wa uchaguzi huo.
Kwa upande wao, wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji
Wilaya ya Shinyanga Mjini, Bwana Daniel Kapaya na Giti Boniphace, wametoa wito
kwa wazazi kuwalea watoto wao kwa njia bora, kuwapeleka shule, kanisani, na
msikitini, pamoja na kuwafundisha kazi za mikono huku wakisisitiza kuwaepusha
na vitendo vya ukatili.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi,
Mhandisi James Jumbe, amesema wakati huu unahitaji zaidi uongozi wa Rais Dkt.
Samia Suluhu Hassan na mgombea mwenza wake, Dkt. Emmanuel Nchimbi, kutokana na
uwezo wao wa kuwaletea Watanzania maendeleo.
Jumbe amempongeza Rais
Dkt. Samia kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi
mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo sekta ya elimu, afya, na miundombinu, akisema
hatua hiyo inaendelea kuleta mabadiliko makubwa kwa wananchi wa Shinyanga na
Tanzania kwa ujumla.
Aidha,
amesema uteuzi wa Dkt. Nchimbi kuwa mgombea mwenza wa Dkt. Samia ni ishara ya
imani kubwa aliyonayo ndani ya chama na Taifa, akiwataka wanachama wa CCM na
wananchi kwa ujumla kuwaunga mkono katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Ziara ya Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini inaendelea, lengo likiwa ni kufanya tathmini ya utekelezaji wa Ilani ya CCM, kuangalia hali ya uhai wa chama, na kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa katika kata zote za Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini Mzee Fue Mrindiko, akizungumza katika kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi, Mhandisi James Jumbe, akizungumza katika kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Februari 19, 2025.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Mary Makamba, akizungumza leo Februari 19, 2025.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Bwana Daniel Kapaya, akizungumza leo Februari 19, 2025.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Mzee Giti Boniphace, akizungumza leo Februari 19, 2025.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi, Mhandisi James Jumbe, akizungumza na wanachama na viongozi mbalimbali katika kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Februari 19, 2025.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi, Mhandisi James Jumbe, akizungumza na wanachama na viongozi mbalimbali katika kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Februari 19, 2025.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini Mzee Fue Mrindiko, akizungumza na
wanachana na viongozi katika kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini Mzee Fue Mrindiko, akizungumza na wanachana na viongozi katika kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Bwana Daniel Kapaya, akizungumza leo Februari 19, 2025.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi,
Mhandisi James Jumbe, akizungumza na wanachama na viongozi mbalimbali katika
kata ya Kitangili Manispaa ya Shinyanga Februari 19, 2025.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi,
Mhandisi James Jumbe, akizungumza na wanachama na viongozi mbalimbali katika
kata ya Kitangili Manispaa ya Shinyanga Februari 19, 2025.
Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga
Mjini, ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya Wazazi,
Mhandisi James Jumbe, akizungumza na wanachama na viongozi mbalimbali katika
kata ya Kitangili Manispaa ya Shinyanga Februari 19, 2025.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini Mzee Fue Mrindiko, akisisitiza wazazi kuchangia chakula shuleni kwa ajili ya watoto wao.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Mjini Mzee Fue Mrindiko, akizungumza na
wanachana na viongozi katika kata ya Kitangili Manispaa ya Shinyanga.
Post a Comment