Na Mapuli Kitina Misalaba
Jumuiya ya wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini
imewaomba wanachama na wananchi kuendelea kuweka imani juu ya CCM katika
utatuzi wa kero na changamoto mbalimbali zinazowakabili.
Hayo yamezungumzwa na mwenyekiti wa jumuiya hiyo
Mzee Fue Mrindoko pamoja na wajumbe wa kamati ya utekelezaji wa jumuiya hiyo
wakati wa ziara yao ambapo leo Februari 20, 2025 jumuiya hiyo imefanya ziara
katika kata ya Ndembezi, Chibe pamoja na kata ya Ibinzamata.
Ambapo katika kata ya Chibe wametembelea daraja
jipya linalounganisha Chibe na kata ya Old Shinyanga ambapo kata ya Ibinzamata
wametembelea mradi wa daraja la makabulini ambayo yote utekelezaji wake
unaendelea vizuri huku wakimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt
Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha kwa ajili ya utatuzi wa changamoto katika
maeneo hayo.
Mrindoko pia ameipongeza serikali kwa kutoa fedha za
ujenzi wa miradi ya maendeleo, ikiwemo miradi ya barabara, elimu, maji, na
afya, na kuhimiza jamii kuendelea kushirikiana kwa pamoja katika utekelezaji wa
miradi hiyo.
Viongozi hao wamewahimiza wanachama wa CCM na
wananchi kwa ujumla kuendelea kukiamini Chama cha Mapinduzi na kwamba
changamoto zilizopo zitaendelea kuwekwa kwenye mpango ili kutatuliwa kwa mujibu
wa Ilani ya chama hicho.
Kwa upande wake, Mjumbe wa kamati ya Siasa ya CCM
Wilaya ya Shinyanga mjini ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya
ya Wazazi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhandisi James Jumbe, amesema ujenzi
wa daraja kubwa la Chibe ni sehemu ya kazi nzuri zinazofanywa na Mhe. Rais
Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha miundombinu ya barabara inakuwa mizuri
ili kuwezesha kukua kwa uchumi.
“Daraja
la Chibe ni kubwa na zuri. Haya ni mambo mazuri yanayofanywa na Mhe. Rais Samia
Suluhu Hassan. Mama Samia ametekeleza Ilani ya CCM kwa zaidi ya asilimia 100.
Ameonesha maendeleo ya kiuchumi kwa vitendo, nasi hatuna zawadi ya kumpa zaidi
ya kumpatia kura za kutosha kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2025 kwa sababu tayari
Chama kimempitisha kuwa mgombea Urais kupitia CCM pamoja na mgombea mwenza Dkt.
Emmanuel Nchimbi ili waweze kutuletea maendeleo zaidi,”
amesema Jumbe.
“Tunazo
sababu nyingi za kutamba na Mama Samia, tunazo sababu lukuki za kumuunga mkono
Rais Samia kwa mambo makubwa na mazito aliyoyafanya katika taifa hili. Amefanya
mabadiliko makubwa katika mahusiano ya kimataifa, ujenzi wa miundombinu ya
barabara, afya, elimu, maji, umeme na kuimarisha demokrasia katika nchi ambapo
hata vyama vya upinzani vinafanya mikutano yake kwa amani,”
ameongeza Jumbe.
Jumbe ametumia fursa hiyo kuwaomba Watanzania
kuendelea kukiunga mkono Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwakaribisha waliopo
katika vyama vya upinzani na wasio na chama kujiunga CCM kwani ni chama imara
chenye nia ya dhati ya kuwaletea maendeleo wananchi.
“Mwaka
2020 Shinyanga tulikuwa wa pili katika kukipigia kura kwa kishindo Chama Cha
Mapinduzi, mwaka huu 2025 tunataka tushike nafasi ya kwanza. Nafasi ya Urais
tayari tuna mgombea Mama yetu Mhe. Samia Suluhu Hassan, nafasi za Udiwani na
Ubunge wagombea watapatikana kwa mujibu wa taratibu za Chama,”
ameongeza Jumbe.
Diwani wa kata ya Chibe, Mhe. John Kisandu, amesema
ujenzi wa daraja la Chibe – Old Shinyanga lenye urefu wa mita 45 linalojumuisha
barabara, kalvati na daraja likigharimu jumla ya shilingi milioni 475,
umekamilika na lipo katika matazamio huku akiomba taa ziwekwe katika eneo hilo
ili kuimarisha usalama wapitaji kwani linatumiwa na watu kutoka maeneo mengi,
ikiwemo kutoka Mkoani Tabora.
“Daraja
hili limerahisisha mawasiliano kati ya kata ya Chibe na Old Shinyanga, kwa
sababu hapa palikuwa hapapitiki wakati wa masika kutokana na kuwepo kwa mto
mkubwa. Usalama sasa upo na mapato ya halmashauri yameongezeka kutokana na
kwamba sasa wafanyabiashara wengi wanaokwenda katika mnada wa Old Shinyanga na
Tinde wanapita katika daraja hili,” ameeleza Kisandu.
Naye Diwani wa kata ya Ibinzamata, Mhe. Ezekiel
Sabo, amesema ujenzi wa Daraja la Ibinzamata Makaburini linasaidia kurahisisha
kufika katika eneo la makaburini na maeneo ya jirani kwani eneo hilo lilikuwa
halipitiki wakati wa masika baada ya daraja la awali kuvunjika.
Wananchi wa maeneo husika wameishukuru serikali kwa
kujenga madaraja hayo ambayo yamerahisisha usafiri na kuondoa adha ya
kutopitika kwa baadhi ya barabara wakati wa mvua ambapo wamesema madaraja hayo
yamekuwa mkombozi kwao, hasa wafanyabiashara na wakazi wanaotumia njia hizo
kila siku kwa shughuli zao za kiuchumi.
Jumuiya ya Wazazi Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya
ya Shinyanga Mjini inaendelea na ziara ya kutembelea kata za Jimbo la Shinyanga
Mjini, lengo kuu ni kuzungumza na wanachama na viongozi wa CCM, kufanya
tathmini ya utekelezaji wa Ilani ya CCM, kuangalia hali ya uhai wa chama, na
kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa katika maeneo hayo.
Wakiwa katika ziara hiyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Wazazi CCM Shinyanga Mjini, Fue Mrindoko, amesisitiza umuhimu wa wanachama wa
CCM kudumisha mshikamano na umoja ili kuimarisha chama na kuendelea na
utekelezaji wa mipango yake ya maendeleo.
Naye, Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya
Wazazi Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mary Makamba, ametoa onyo kwa akina mama
kuhusu madhara ya ulevi kwa familia.
Makamba amesisitiza kwamba ulevi, hasa pombe,
unachangia migogoro ya familia na hata kudhoofisha afya ya akili ya akina baba
ambapo ameeleza kwamba baadhi ya ndoa zimevunjika au kuingia matatizoni kwa
sababu ya tabia ya wanawake kujiingiza katika ulevi.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi
Wilaya ya Shinyanga Mjini Bwana Daniel Kapaya ametoa wito kwa jamii kuwalinda
watoto dhidi ya vitendo vya ukatili, huku akionya kuhusu vitendo vya ulawiti na
ubakaji, na kuhamasisha jamii kuchukua hatua za haraka ili kukomesha vitendo
hivi vinavyohatarisha usalama wa watoto.
Wakati huo huo Kapaya amewasisitiza wazazi na walezi
kuwaepusha watoto na matumizi ya simu janja na kwamba hatua hiyo imekuwa
ikisababisha mmomonyoko wa maadili na vitendo vya ukatili.
Naye mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wilaya ya
Shinyanga Mjini, Mzee Giti Boniphace, amewahimiza wazazi na walezi kuhakikisha
watoto wanapata haki yao ya elimu huku akiwasisitiza kutimiza wajibu wao katika
huduma stahiki.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Mzee Fue Mrindoko, akizungumza na wanachama wa CCM, viongozi wa chama na jumuiya zake katika kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga Februari 20, 2025.
Wanachama wa CCM, viongozi wa chama na jumuiya zake
katika kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wilaya ya Shinyanga
Mjini, Mzee Giti Boniphace, akiwahimiza wazazi na walezi kuhakikisha watoto
wanapata haki yao ya elimu katika kata ya Ndembezi.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi
CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Zulfa Hassan akizungumza.
Katibu Elimu na Malezi jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Richard Mseti akizungumza katika kata ya Ndembezi.
Viongozi mbalimbali baada ya kuwasili katika daraja
la Chibe – Old Shinyanga lenye urefu wa mita 45 linalojumuisha barabara,
kalvati na daraja likigharimu jumla ya shilingi milioni 475.
Viongozi mbalimbali baada ya kuwasili katika daraja
la Chibe – Old Shinyanga lenye urefu wa mita 45 linalojumuisha barabara,
kalvati na daraja likigharimu jumla ya shilingi milioni 475.
Diwani wa kata ya Chibe, Mhe. John Kisandu, akitoa
maelezo kwa Viongozi mbalimbali kuhusu daraja
la Chibe – Old Shinyanga lenye urefu wa mita 45 linalojumuisha barabara,
kalvati na daraja likigharimu jumla ya shilingi milioni 475.
Diwani wa kata ya Chibe, Mhe. John Kisandu, akitoa
maelezo kwa Viongozi mbalimbali kuhusu daraja
la Chibe – Old Shinyanga lenye urefu wa mita 45 linalojumuisha barabara,
kalvati na daraja likigharimu jumla ya shilingi milioni 475.
Mjumbe
wa kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga mjini ambaye pia ni Mjumbe wa
Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhandisi
James Jumbe, akizungumzia ujenzi wa daraja kubwa la Chibe ambapo amesema ni
sehemu ya kazi nzuri zinazofanywa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan katika
kuhakikisha miundombinu ya barabara inakuwa mizuri ili kuwezesha kukua kwa
uchumi.
Mjumbe wa kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga
mjini ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi CCM
wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhandisi James Jumbe, akizungumza na wanachama wa
CCM, viongozi wa chama na jumuiya zake katika kata ya Chibe Manispaa ya
Shinyanga Februari 20, 2025.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi CCM Wilaya ya
Shinyanga mjini Mzee Fue Mrindoko, akizungumza na wanachama wa CCM, viongozi wa
chama na jumuiya zake katika kata ya Chibe Manispaa ya Shinyanga Februari 20,
2025.
Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini
ikitembelea na kukagua ujenzi wa Daraja la Ibinzamata Makaburini Februari 20,
2025.
Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini
ikitembelea na kukagua ujenzi wa Daraja la Ibinzamata Makaburini Februari 20,
2025.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wilaya ya Shinyanga Mjini, Mzee Giti Boniphace, akiwahimiza wazazi na walezi kuhakikisha watoto wanapata haki yao ya elimu katika kata ya Ibinzamata.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi
Wilaya ya Shinyanga Mjini Bwana Daniel Kapaya akizungumza.
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi
CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Zulfa Hassan akizungumza.
Mjumbe wa kamati ya Siasa ya CCM Wilaya ya Shinyanga
mjini ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi CCM
wilaya ya Shinyanga Mjini, Mhandisi James Jumbe, akizungumza na wanachama wa
CCM, viongozi wa chama na jumuiya zake katika kata ya Ibinzamata Manispaa ya
Shinyanga Februari 20, 2025.
Post a Comment